CCM sasa ikubali mahitaji ya Wazanzibari wengi

LUS0MYA

JF-Expert Member
Aug 4, 2011
862
1,097
Nimejaribu kufuatilia siasa za Zanzibar na kubaini mambo yafuatayo;

1.Wazanzibari wengi wanahitaji Muundo wa serikali ya mkataba na sio serikali mbili au tatu.Wazanzibari hawa wapo ndani ya CCM na CUF.

2.Baada ya kuunda SUK wazanzibari wamekuwa wamoja katika kudai masilahi yao ndani ya Muungano na sio siri tena Wazanzibari wakiwemo wanaccm wanaamini kwa kupitia CUF maslahi yao katika muungano yatatatuliwa kwa haraka zaidi hasa kwa kuzingatia kuwa CCM kama chama kikongwe kuna mahafidhina wasiohitaji mabadiliko kwa kutumia mgongo wa mapinduzi ili kulinda masilahi yao.

3.Wazanzibari wengi wamegundua kuwa uhasama wa kisiasa baina ya vyama vikuu(CCM na CUF)ulirudisha nyuma kasi ya kudai haki katika Muungano na ilipoundwa SUK mahitaji yao mengi yametekelezwa katika kipindi kifupi sana na hata masuala ya haki ya mafuta yametatuliwa pamoja ilikuwa ni kilio cha wazanzibari miaka mingi.

4.Wazanzibari wengi hawaguswi na chama kipi kitaongoza serikali lakini wanafikiri ilani ya CUF imebeba mahitaji ya wazanzibari bila kuchujwa kulinganisha na ile ya CCM

5.Mgawanyo wa kura zilizotangazwa zilionyesha waziwazi mwelekeo wa mahitaji ya wazanzibari kwani CUF ilipata kura nyingi za wanaccm katika maeneo yote ya unguja na Pemba.
 
Kwanini kama ni wengi na wanaamini walimchagua wasirudie kufanya walichokifanya hawari? ama leo macho yao yamekuwa vipofu wanajisi hawatamwona vizuri jamaa yao na mandevu yake?
 
Kwanini kama ni wengi na wanaamini walimchagua wasirudie kufanya walichokifanya hawari? ama leo macho yao yamekuwa vipofu wanajisi hawatamwona vizuri jamaa yao na mandevu yake?

Rweye warudie kwa tume ipi mkuu ??????????!! Ya Jecha hii isiyotaka kuona mawazo mbadala ?! Ccm msiwe wabinafsi mmeshindwa. Uungwana ni pamoja na kukubali kushindwa
 
Naunga mkono hoja lazima alieshida apewe in jambo LA aibu kwa nchi inayofuata mfumo wa vyama Vinci halafu ikawa kigeugeu in aibu mm nasema haina haja ya vyama Vinci ikiwa chama kimoja kitakuwa na hati miliki ya nchi kwa kivuli cha mapinduzi.Mapinduzi yalikuwa Urusi na Leo upon ndembe ndembe inatakuwa mapinduzi ya John Okelo kumuondowa Shamte?
 
Kwanini kama ni wengi na wanaamini walimchagua wasirudie kufanya walichokifanya hawari? ama leo macho yao yamekuwa vipofu wanajisi hawatamwona vizuri jamaa yao na mandevu yake?

kwa nn urudiwe? kweli wewe bege
 
Kwanini kama ni wengi na wanaamini walimchagua wasirudie kufanya walichokifanya hawari? ama leo macho yao yamekuwa vipofu wanajisi hawatamwona vizuri jamaa yao na mandevu yake?

mwana ccm utamjua kwa uwezo wake
 
Kwanini kama ni wengi na wanaamini walimchagua wasirudie kufanya walichokifanya hawari? ama leo macho yao yamekuwa vipofu wanajisi hawatamwona vizuri jamaa yao na mandevu yake?

Upo tayari na tanganyika uchaguzi urudiwe?
 
Nimejaribu kufuatilia siasa za Zanzibar na kubaini mambo yafuatayo;

1.Wazanzibari wengi wanahitaji Muundo wa serikali ya mkataba na sio serikali mbili au tatu.Wazanzibari hawa wapo ndani ya CCM na CUF.

2.Baada ya kuunda SUK wazanzibari wamekuwa wamoja katika kudai masilahi yao ndani ya Muungano na sio siri tena Wazanzibari wakiwemo wanaccm wanaamini kwa kupitia CUF maslahi yao katika muungano yatatatuliwa kwa haraka zaidi hasa kwa kuzingatia kuwa CCM kama chama kikongwe kuna mahafidhina wasiohitaji mabadiliko kwa kutumia mgongo wa mapinduzi ili kulinda masilahi yao.

3.Wazanzibari wengi wamegundua kuwa uhasama wa kisiasa baina ya vyama vikuu(CCM na CUF)ulirudisha nyuma kasi ya kudai haki katika Muungano na ilipoundwa SUK mahitaji yao mengi yametekelezwa katika kipindi kifupi sana na hata masuala ya haki ya mafuta yametatuliwa pamoja ilikuwa ni kilio cha wazanzibari miaka mingi.

4.Wazanzibari wengi hawaguswi na chama kipi kitaongoza serikali lakini wanafikiri ilani ya CUF imebeba mahitaji ya wazanzibari bila kuchujwa kulinganisha na ile ya CCM

5.Mgawanyo wa kura zilizotangazwa zilionyesha waziwazi mwelekeo wa mahitaji ya wazanzibari kwani CUF ilipata kura nyingi za wanaccm katika maeneo yote ya unguja na Pemba.
Hayatuhusu, Zanzibar ni Nchi!
 
Back
Top Bottom