CCM ni maarufu kuliko wagombea wote

CCM ni maarufu kuliko wagombea wote

magode

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2014
Posts
2,204
Reaction score
3,338
Salaam
Wanabody..!
Kumekuwa na kauli nyingi za kuwatisha wanaccm na kuwaaminisha wananchi kuwa eti kuna mwanaccm bora zaidi kuliko mwingine..! Haya ni matusi kwa chama ambacho ni kikongwe hapa nchini na Africa kwa ujumla.

Nataka kuwaondoa shaka wanachama,wapenzi,wakereketwa na washabiki wa chama cha mapinduzi,kuwa ccm ni maarufu zaidi kuliko hao wagombea wote wa nafasi ya juu kabisa ktk Taifa letu.

CCM ina katiba yake,ina kanuni na taratibu za kupata wagombea wake ktk nafasi zote za uongozi.

Wagombea wote wa nafasi ya urais,huo umaarufu wanaojidai nao wameupata ndani ya ccm na wanaendelea kuwa maarufu ndani ya ccm. Nje ya ccm hawana lolote..!

Atakayeteuliwa,hatateuliwa kutokana na umaarufu wake,atateuliwa kwa kufuata sifa na vigezo vilivyowekwa na si umaarufu wa mtu.

Namaliza kwa kusema,kila mgombea ajiandae kisaikolojia km anavyoonekana kujiandaa waziri mkuu Mizengo Pinda,huyu ndo mgombea ambae hana pressure kwa matokeo yoyote yale..! Atakayesimamishwa na CCM hata km hajulikani kabisa,kuanzia sekunde ya kwanza ya kutangazwa kwake,kila mtu atataka amjue..!!


Kidumu chama cha mapinduzi.
 
Tunataka wanachama wamuwe wenyewe sio kikundi kidogo chenye visasi ni kura tu sio kukatwa mtu
 
Tunataka wanachama wamuwe wenyewe sio kikundi kidogo chenye visasi ni kura tu sio kukatwa mtu

tengenezeni chama chenu sio ccm ninayojua kuwa sio kila mtu anaingiza mkono ndani ya kapu,nyerere angeweka ccm kwa namna hiyo ingekuwa imaekufa zamani
 
lowasa amekaa nje ya ccm miaka 7 na ccm bado ipo na hata kwenye vikao vya chama alikuwa ni msikilizaji anamtishia nani
 
lowasa anatishia kuona kama watamuogopa lakn baada ya wenye akili zao kumaliza kazi yao atakuwa mwanachama mtiifu ndani ya ccm,kama ni wakuondoka angeondoka mwaka 1995
 
akikatwa lowasa patachimbika by kingunge ngombale mwiru...

Alikatwa malecela akiwa na ushawishi NEC na mkutano mkuu Wa ccm na cc pia maana alikua mjumbe Wa cc tena akiwa makamu mwenyekiti wa ccm taifa,itakua lowassa ambae ni mjumbe tu Wa NEC tena Wa kupitia wilayani,hayumo hata kwenye kamati kuu.ccm hata ikimsimamisha nape itashinda tu,lowassa akienda upinzani yes ataipa changamoto ccm lakini hawezi kushinda sema atawapatia wabunge wapinzani
 
Tunataka wanachama wamuwe wenyewe sio kikundi kidogo chenye visasi ni kura tu sio kukatwa mtu

Yani we ni kiazi kweli kila mmmoja aking'ang'ania mtu anayemtaka aende ikulu patakuwa na marais wangapi acha vigezo vifuatwe kwa wagombea wote
 
Salaam
Wanabody..!
Kumekuwa na kauli nyingi za kuwatisha wanaccm na kuwaaminisha wananchi kuwa eti kuna mwanaccm bora zaidi kuliko mwingine..! Haya ni matusi kwa chama ambacho ni kikongwe hapa nchini na Africa kwa ujumla.

Nataka kuwaondoa shaka wanachama,wapenzi,wakereketwa na washabiki wa chama cha mapinduzi,kuwa ccm ni maarufu zaidi kuliko hao wagombea wote wa nafasi ya juu kabisa ktk Taifa letu.

CCM ina katiba yake,ina kanuni na taratibu za kupata wagombea wake ktk nafasi zote za uongozi.

Wagombea wote wa nafasi ya urais,huo umaarufu wanaojidai nao wameupata ndani ya ccm na wanaendelea kuwa maarufu ndani ya ccm. Nje ya ccm hawana lolote..!

Atakayeteuliwa,hatateuliwa kutokana na umaarufu wake,atateuliwa kwa kufuata sifa na vigezo vilivyowekwa na si umaarufu wa mtu.

Namaliza kwa kusema,kila mgombea ajiandae kisaikolojia km anavyoonekana kujiandaa waziri mkuu Mizengo Pinda,huyu ndo mgombea ambae hana pressure kwa matokeo yoyote yale..! Atakayesimamishwa na CCM hata km hajulikani kabisa,kuanzia sekunde ya kwanza ya kutangazwa kwake,kila mtu atataka amjue..!!


Kidumu chama cha mapinduzi.

sawa sawia
 
Tunataka wanachama wamuwe wenyewe sio kikundi kidogo chenye visasi ni kura tu sio kukatwa mtu
Mkuu nselembwe kufanya uteuzi wa jina moja kwenye kundi la watu 40 au zaidi wenye sifa inahitaji busara zaidi kuliko kura km unavyofikiri. CCM wanamfumo mzuri sana wa kufanya hiyo kazi. Nakuhakikishia haki itatendeka,hakuna atakayeonewa. Na labda nikuambie,ndani ya ccm hakuna kushinda wala kushindwa! Huko wanatafuta mwenzao atakayepeperusha bendera ya kijani kushindana na UKAWA na vyama vingine.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu umenena vema. Hao wanaotoa kauli za vitisho kwa chama ni mbwa vibogoyo tu, wanabweka ili kujihami tu lakini hawana madhara.
 
... Toka ln chama chakavu kikawa maarufu
Mkuu KIBARAone ukiacha ushabiki kidogo tu na kuamua kusema ukweli,huwezi kukwepa ukweli kwamba ccm ni maarufu zaidi kuliko watangaza nia wote! Halafu kitu ambacho hukielewi,hao wanaosema ni maarufu ni kwa sababu wamo humo ndani ya ccm,wakitoka hata habari zao ili ziandikwe watalazimika kuhonga. Kwa jinsi ccm ilivyo maarufu,vikao vya uteuzi vikiishaanza,kwenye vyombo vyote vya habari hiyo ndo itakuwa habari..!! CCM hata wakiamua ugombee wewe,utajulikana siku hiyo hiyo ingawa suala la kushinda uchaguzi ni jambo jingine.
 
Last edited by a moderator:
Alikatwa malecela akiwa na ushawishi NEC na mkutano mkuu Wa ccm na cc pia maana alikua mjumbe Wa cc tena akiwa makamu mwenyekiti wa ccm taifa,itakua lowassa ambae ni mjumbe tu Wa NEC tena Wa kupitia wilayani,hayumo hata kwenye kamati kuu.ccm hata ikimsimamisha nape itashinda tu,lowassa akienda upinzani yes ataipa changamoto ccm lakini hawezi kushinda sema atawapatia wabunge wapinzani
Mkuu hata wabunge anaweza kuwapunguza,record ya lowassa si nzuri sana,akiondoka ccm na ccm wakaamua kumshambulia,chama atakachoenda kitapunguza idadi kubwa sana ya wabunge.
 
Back
Top Bottom