CCM Ni Disaster, Lakini CHADEMA ni Catastrophe!!!!!!

CCM Ni Disaster, Lakini CHADEMA ni Catastrophe!!!!!!

martyr2012

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2012
Posts
603
Reaction score
245
Wanajamvi, ninasikitishwa na mambo yanayoendelea hapa TZ na hasa kwenye vyama vya siasa. CCM ikiwa ni chama dola kimeonyesha kuchoka kabisa katika kuisimamia serikali. Matokeo yake:
  • Ufisadi mkubwa wa fedha za walipa kodi wa TZ,
  • Usimamizi mbovu wa raslimali za nchi
  • Kugawa raslimali za nchi kwa wageni ambao wanavuna bila kuacha faida kwa wenye raslimali
  • Kukua kwa tabaka la viongozi matajiri walioifisidi nchi na kujitajirisha wenyewe na familia zao.
  • Nchi kukosa muelekeo kabisa pamoja na utajiri aliotuajaalia Mungu na hatimaye waTZ kukata tamaa.

Njia mojawapo ya kuiondoa hali hii ni kubadilisha serikali kwa kuiweka madarakani serikali ya chama mbadala. Tatizo nilinalo sasa na nina imani si mimi tu ni wengi ni chama gani au kiongozi gani? Wakati wengi wakifikiria kuipa nafasi CHADEMA, logic zote zinakataa kutokana na ukweli ufuatao:
  • CHADEMA ni chama cha kimla
  • Haina demokrasia
  • Viongozi wa CHADEMA kwenye ngazi ya Taifa hawana uweledi wa kuiongoza nchi.
  • Hawana mpango mkakati wa kuiendeleza nchi na raslimali zake bali wanaishi kwa matukio tu. hivyo watakapoingia madarakani watatumia crisis management strategy ili kukabili tukio moja la msimu tu. Likiisha watasubiri jingine au serikali itakuwa 'mfu'
  • Ni watu wasiotii sheria na wangependa kupindisha sheria kwa manufaa yao.
  • Wana tuhuma za ubadhirifu wakiwa wana 'kifuko' kidogo cha ruzuku ya chama vipi tukiwapa HAZINA ya Taifa?

Wanajamvi tuyajadili mambo haya si kwa jazba bali kwa kupata mustakbali nzuri wa nchi yetu. Mimi si mwanachama wa CCM wala CDM wala chama chochote. ni Mtanzania ambaye nitaathirika kutokana na sera za chama kitakacho shika dola. Tusilete MATUSI tujadili hoja. Wakatabahu
 
Hivi kati ya disaster na catastrophe ipi ni hatari zaidi?
 
Mleta uzi una akili sana......yaani wenye akili wanaona katika kona uliyoonea.......
 
Ur urguments seem objective but the allegations may not be conclusive esp. for CDM are just based on conjecture
 
Kaka umenene vyema maana hujaegemea popote ila tukipima hapa mi naona tungewapa chadema maana pamoja na kwamba viongozi wa ngazi za taifa hawana weledi mkubwa wa kuliongoza taifa lakini wanaushirikiano na walioko ngazi za chini wenye utashi mkubwa na mimi kikubwa ninacho kiona hapa ccm wakindelea kuwepo madarakani hakika tusahau kusikia ama kuona baadhi ya rasilimali
 
Wanajamvi, ninasikitishwa na mambo yanayoendelea hapa TZ na hasa kwenye vyama vya siasa. CCM ikiwa ni chama dola kimeonyesha kuchoka kabisa katika kuisimamia serikali. Matokeo yake:
  • Ufisadi mkubwa wa fedha za walipa kodi wa TZ,
  • Usimamizi mbovu wa raslimali za nchi
  • Kugawa raslimali za nchi kwa wageni ambao wanavuna bila kuacha faida kwa wenye raslimali
  • Kukua kwa tabaka la viongozi matajiri walioifisidi nchi na kujitajirisha wenyewe na familia zao.
  • Nchi kukosa muelekeo kabisa pamoja na utajiri aliotuajaalia Mungu na hatimaye waTZ kukata tamaa.

Njia mojawapo ya kuiondoa hali hii ni kubadilisha serikali kwa kuiweka madarakani serikali ya chama mbadala. Tatizo nilinalo sasa na nina imani si mimi tu ni wengi ni chama gani au kiongozi gani? Wakati wengi wakifikiria kuipa nafasi CHADEMA, logic zote zinakataa kutokana na ukweli ufuatao:
  • CHADEMA ni chama cha kimla
  • Haina demokrasia
  • Viongozi wa CHADEMA kwenye ngazi ya Taifa hawana uweledi wa kuiongoza nchi.
  • Hawana mpango mkakati wa kuiendeleza nchi na raslimali zake bali wanaishi kwa matukio tu. hivyo watakapoingia madarakani watatumia crisis management strategy ili kukabili tukio moja la msimu tu. Likiisha watasubiri jingine au serikali itakuwa 'mfu'
  • Ni watu wasiotii sheria na wangependa kupindisha sheria kwa manufaa yao.
  • Wana tuhuma za ubadhirifu wakiwa wana 'kifuko' kidogo cha ruzuku ya chama vipi tukiwapa HAZINA ya Taifa?

Wanajamvi tuyajadili mambo haya si kwa jazba bali kwa kupata mustakbali nzuri wa nchi yetu. Mimi si mwanachama wa CCM wala CDM wala chama chochote. ni Mtanzania ambaye nitaathirika kutokana na sera za chama kitakacho shika dola. Tusilete MATUSI tujadili hoja. Wakatabahu

Mwanajamvi kama mimi siwezi kusoma ujinga na uharo huu nikajadili .If only it was possible I would have placed this topic in the trash ila sema hakuna button ya kuruhusu hilo .
 
Hongera umeongea hoja nzuri kila chama kina mambo ya kurekebisha, lakini huwezi amini kuna vyama havitaki kukosolowa ukivikosoa basi kama hawajakutukana wataishia kukwambia hoja yako haina msingi mimi nilishawahi kujiuliza kwanini wanachama au washabiki wa vyama vya siasa tena wengine hata hawalipwi mshahara yaani ni wabishi kupindukia nyekundu wao wanalazimisha ni vyeupe. Nimekubali ushabiki au imani juu ya jambo fulani ukizidi sana hupunguza uwezo wa kufikiri.
 
Haya ni mapungufu amabayo vyama vingi vya siasa havina budi kuangalia kiundani kwani kufuata ideology ya chama pekee bila utekelezaji wa lengo ni sawa na kuipotosha jamii hisika ambayo hutumia nguvu, jitihada na imani kubwa kwa vyama hivi.....hivyo basi ni wazi kuwa vyama vyote vijilekebishe kama vitataka tuvipe imani ya kuongoza nchi...Nawasilisha!
 
kuna hoja mbili katikati ya mistari yako,nashukuru kwa kutumia muda wako vizuri(if only)kuweka upembuzi huu hapa,hoja yako ya kwanza uliyoielekeza zaidi kwa ccm,ni hoja ya KUONA,KUFIKIRI,NA KUJIRIDHISHA, hoja ya pili inayoielekea chadema ina base kwenye HISIA na HOFU zaidi,unaposema !tukiwapa nchi SI wata-----! Hapo unakuwa umeweka utabiri zaidi kuliko upembuzi,je siku nikikuonyesha mambo mazuri ambayo yamefanywa na ccm utabadili mtazamo wako kuwahusu? Je unajua pia kuwa kabla hali haijafikia hapa ccm pia WALIHISI kuwa njia wanayoipitia ndiyo sahihi? sasa je hisia unadhani zinaweza kutufikisha kwenye conclusive point bila kuacha shaka yoyote(HOFU?) Tumefika hapa kwa uongozi wa kihisia,tusiongozwe tena kutoka hapa kwa hisia,kama dereva ameshindwa kulimudu gari,na anapiga kelele za kuomba msaada ili gari lisiteketee na abiria wote ndani,walio nje ya gari wanaojua kuwa wana uwezo wa kuliokoa gari hawapaswi tena kuanza kutishana na kuulizana we wa wapi!! Ccm ina mapungufu,chadema ina yake,Tlp,Cuf,Nccr,kadhalika,tukitafuta chama kisicho na doa tutalazimika kubadili mfumo ili tuishi bila vyama,tukiishi bila vyama tutatafuta namna ya kuishi bila viongozi(for no one is,or will be righteous) sisi tunaoyaona haya ndiyo wenye dhamana isiyo na hofu ya kuwapanga na kuwapangua walioko mbele ya vyama hivi,tuiambie ccm mara mbili,ikishindwa tuiweke chadema au nccr etc,tusisubiri kupata kisicho na doa,tuvisafishe vilivyopo,vilivyooza au visivyosafishika tuvitupe mbali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom