Liganga
Senior Member
- Jul 4, 2007
- 165
- 128
Baada ya muda mrefu sana wa kuwa pembeni nikitazama yanayojitokeza nimepata msukumo wa kutafakari kwa kina kazi iliyombele ya Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi.
Nikiitazama hali hii nakumbuka miaka ya 1934 pale Adolf Hitler na chama chake walipokamata madaraka ya Ujerumani.
Katika vuguvugu la kuchukua madaraka pale Ujerumani, Adolf na kundi lake waliunda mtandao mpana ulionea nchi nzima wakitumia ushawishi, nguvu na shurutisho kupamabana na wapinzani wao pamoja na serikali iliyokuwa madarakani.
Baada ya kufanikiwa kuwa chansela haikupita mda mrefu Adolf kubaini alikuwa na kibarua kigumu kudhibiti nguvu ya mtandao aliounda kuhakikisha ushindi wake.
Moja ya changamoto alizakabiliana nazo ni kile kikundi cha Sturmabteilung (SA) kilichokuwa chini ya uongozi wa Ernst Röhm. Kundi hili lilikuwa ni kubwa ukilinganisha na mengine likifikia idadi ya wafuasi zaidi ya milioni tatu.
Bwana Ernst Röhm binafsi hakuwa anaridhishwa na utendaji wa Adolf akiamini kuwa malengo ya kukamata madaraka yalikuwa hayajatekelezwa kwa ukamilifu na aliamini kuwa kunahitajika mapinduzi mengine.
Adolf binafsi alikuwa anatambua nguvu kubwa ya Ernst Röhm and jeshi kubwa la wafuasi milioni tatu nyuma yake. Haikuchukua mda ugomvi kuibuka kati yao na Ernst Röhm kuanza kumpinga Adolf na hata kuwatumia watu wa pembeni lakin wenye nguvu na ushawishi katika Ujerumani kupingana na Adolf.
Mnamo mwezi Julai 1934 Adolf alipoona uhai wa chama cha Nazi unatishiwa ikiwemo nguvu ya serikali yake, alifanya safari ya ghafla alfajiri kuelekea Bad Wiessee akiwa ameambatana na kikosi chake cha intelijensia kilichofaamika kama Schutzstaffel (SS). Siku hiyo ndio ilianza oparesheni MAALUM ya kuwashugulikia viongozi wote wa SA waliokuwa mstari wa mbele wa kuuvuruga uongozi wa Nazi na serikali ya Adolf.
Oparesheni hii maalum ilifahamika kama "The Night of the Long Knives".
Wanajamvi nimeona niwaletee hii historia.
Hii ni wiki nzuri ya kutafakari namana m/kiti atakavyokabili changamoto mbalimbali hadi kufikia Jumapili.
Nikiitazama hali hii nakumbuka miaka ya 1934 pale Adolf Hitler na chama chake walipokamata madaraka ya Ujerumani.
Katika vuguvugu la kuchukua madaraka pale Ujerumani, Adolf na kundi lake waliunda mtandao mpana ulionea nchi nzima wakitumia ushawishi, nguvu na shurutisho kupamabana na wapinzani wao pamoja na serikali iliyokuwa madarakani.
Baada ya kufanikiwa kuwa chansela haikupita mda mrefu Adolf kubaini alikuwa na kibarua kigumu kudhibiti nguvu ya mtandao aliounda kuhakikisha ushindi wake.
Moja ya changamoto alizakabiliana nazo ni kile kikundi cha Sturmabteilung (SA) kilichokuwa chini ya uongozi wa Ernst Röhm. Kundi hili lilikuwa ni kubwa ukilinganisha na mengine likifikia idadi ya wafuasi zaidi ya milioni tatu.
Bwana Ernst Röhm binafsi hakuwa anaridhishwa na utendaji wa Adolf akiamini kuwa malengo ya kukamata madaraka yalikuwa hayajatekelezwa kwa ukamilifu na aliamini kuwa kunahitajika mapinduzi mengine.
Adolf binafsi alikuwa anatambua nguvu kubwa ya Ernst Röhm and jeshi kubwa la wafuasi milioni tatu nyuma yake. Haikuchukua mda ugomvi kuibuka kati yao na Ernst Röhm kuanza kumpinga Adolf na hata kuwatumia watu wa pembeni lakin wenye nguvu na ushawishi katika Ujerumani kupingana na Adolf.
Mnamo mwezi Julai 1934 Adolf alipoona uhai wa chama cha Nazi unatishiwa ikiwemo nguvu ya serikali yake, alifanya safari ya ghafla alfajiri kuelekea Bad Wiessee akiwa ameambatana na kikosi chake cha intelijensia kilichofaamika kama Schutzstaffel (SS). Siku hiyo ndio ilianza oparesheni MAALUM ya kuwashugulikia viongozi wote wa SA waliokuwa mstari wa mbele wa kuuvuruga uongozi wa Nazi na serikali ya Adolf.
Oparesheni hii maalum ilifahamika kama "The Night of the Long Knives".
Wanajamvi nimeona niwaletee hii historia.
Hii ni wiki nzuri ya kutafakari namana m/kiti atakavyokabili changamoto mbalimbali hadi kufikia Jumapili.
Hii kazi pia kwa kiasi fulani inafanana na namana m/kiti wa wakati ule alivyokabiliana na changamoto za kumpata mrithi wa Karume mwaka 1972.
Kanali Seif Bakari alikuya ndiye mwenye nguvu, ndiye kipenz cha wengi, ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kutekeleza kwa vitendo sera za utawala wa hayati Abeid Karume.
M/kiti aliibuka na hoja nzito za kumkataa Kanali Bakari na kumpendekeza Alhaj Aboud Jumbe
Hii kazi pia kwa kiasi fulani inafanana na namana m/kiti wa wakati ule alivyokabiliana na changamoto za kumpata mrithi wa Karume mwaka 1972.
Kanali Seif Bakari alikuya ndiye mwenye nguvu, ndiye kipenz cha wengi, ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kutekeleza kwa vitendo sera za utawala wa hayati Abeid Karume.
M/kiti aliibuka na hoja nzito za kumkataa Kanali Bakari na kumpendekeza Alhaj Aboud Jumbe
Pia nguvu ya m/kiti kumudu changamoto ilijidhiirisha tena mwaka 1984, pale alipoitisha kikao cha dharura Dodoma kuchukua hatua dhidi ya yaliyokuwa yanajili Visiwani.
Pale Dodoma paliwaka moto, makundi mawili kutoka visiwani yakipambana, moja kumzamisha Alhaj Jumbe na lingine kuhakikisha anabaki imara.
Pamoja na kukosa urais mwaka 1972, Kanali Bakari alikuwa miongoni wa waliopambana kuhakikisha Jumbe haanguki.
M/kiti alifanikiwa kuendesha kikao kilichozimia kumvua mdaraka yote ndani ya serikali na chama alhaj Jumbe.
M/kiti hakuishia hapo, alihakikisha aliyekuwa m/sheria mkuu wa visiwan wakati ule, raia wa Ghana, anapewa notisi ya kuondoka nchini ndani ya masaa 24.
Waziri Kiongozi Ramadhani Haji yeye alipelekwa kizuizini.
Waziri wa Nchi Bw. Aboud Talib nae pia alitiwa kizuizini.
Aliyepata kuwa jaji mkuu, Bw. Dourado nae alitiwa kizuizini.
Kanali Bakari, mtetezi mkuu wa Alhaj pale Dodoma nae alielekezwa kizuizini
Hatimaye na Rais Aboud Jumbe nae alipelekwa kizuizini.
Hatua hizi zilichukuliwa ikiwa ni jitihada mahusus za kudhibiti na kuweka sawa hali ya hewa kule visiwani.
Jambo hili liliacha taswira ya upeo na nguvu ya m/kiti wa chama.
Kwa mara nyingine tena siasa za visiwani zilimpa m/kiti changamoto kwenye mbio za kumpata mrithi wake 1985.
Chama kilidhibit idadi ya wagombea kuwa WATATU tuu.
Wakipambana;
- Alhaji Hassan Mwinyi
- Bw. Rashid M. Kawawa
- Dk. Salim H. Salim
Vita ilikuwa ni kali pale mpambano ulipobaki kwa wawil tuu baada ya Bw. Kawawa kujitoa.
Rejea historia kujua kilichojiri, lakin m/kiti safari hii alishindwa aliyokusudia.
Nguvu ya kambi ya Mzee Talib, Mzee Natepe, Mzee Haji, Mzee Bomani na Bi Mongella iliibuka mshindi baada ya Alhaj H. Mwinyi kupata ushindi wa kuwa rais wa pili wa Tanzania.
Waliokuwa kikaoni wanaelewa kazi ilivyokuwa ngumu, ushawishi mkumbwa ulifanyika na hoja zilivyosukwa vyema.
Hoja kuu ikiwa kidemokrasi na kiuongozi si vyema kumwacha Alhaj Hassan Mwinye aliyekuwa rais wa visiwan na kumpitisha Dk. Salim aliyekuwa waziri mkuu kuwa rais wa pili wa Tanzania.
Kwa hoja ya mtiririko wa MAMLAKA na succession (kupeana vijiti) ilikuwa ni busara kuacha achukue Alhaj Mwinyi. Hapo m/kiti hakuwa na uwezo wa kupinga bali kukubali hoja hiyo.