Tatizo unafikiri kwa kutumia vidole , awe CCM au CUF hujuma inayofanywa ni moja tu ,watu wasiomjua huyu Othaman ndio wataomshangaa, wale tunaofuatilia mijadala hii kwa muda mrefu he always speak his mind which is very rarely to our modern politicians. ajiandae na lolote lile hata kwenda jela labda kwa kukutwa na documents au hata bomu nyumbani kwake. wazanzibari wenye uchungu na nchi wote wako jela, wamefikishwa mahakamani na wengine wameshafunguliwa kesi, wanatafutwa na polisi na wengine wameshafungwa jela. Ila uhuru wa kweli hupatikana kwa mapambano WaZanzibari walipambana kupata uhuru wao na wataendelea kupambana kuulinda Uhuru wao ,
Vipi Tanganyika mlipambana kupata uhuru ?? NOPE ! ndio maana mmeshikwa na butwaa .mnashangaa watu wanafanya Ikulu sehemu ya biashara namadili makubwa mkisubiri ccm iwaletee maendeleo na matunda ya uhuru.mtasubiri sana ,wametoa posho kubwa ili kuzidi kuuzika uhuru wa Mtanganyika na sasa hawataki kusikia neno Tanganyika ni maagizo kutoka kwa waganga wao wameambiwa kama tanganyika itazuka basi ndio mwisho wenu ,pingeni uweni fanyeni kila kitu lakini msikubali jina Tanganyika bora hata muite Tanzania Bara na ndio wanachokifanya miccm kila kwenye Tanganyika wanaita Tanzania bara.