CCM, mnadhani mmepata huenda mmepatikana.

CCM, mnadhani mmepata huenda mmepatikana.

Status
Not open for further replies.

Mwanaukweli

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2007
Posts
4,789
Reaction score
1,732
Juliana Shonza na Mtela Mwampamba walijiunga na CCM tarehe 12 Februari 2013 na kupokelewa na Kamati Kuu ya CCM. Hii ilikuwa ni baada ya wao kufukuzwa Uanachama wa BAVICHA na CHADEMA. Tukio hilo lilionesha kuwa ni kubwa sana kwa CCM na ikaonekana CCM wamepata vijana watakaoisaidia kukijenga chama.
700794081.jpg


Mara moja Nape Nnauye akawachukua vijana hao na kuanza kuzunguka nao, wakifanya siasa za kuzungumza mabaya ya CHADEMA na uongozi wa juu wa CHADEMA. Mlengwa mkubwa wa kampeni hizo alikuwa Dr. Slaa.

Siasa za kuchafuana huwa zinaweza kuzaa matunda mazuri pale ambapo zinajikita kwenye ukweli. Chama cha siasa kikijenga hoja zake kwa kutumia uongo, na baadaye kikagundulika kuwa kimetumia uongo, watu walio waadilifu wanaotafuta kuunga mkono wanasiasa wenye dira inayoweza kuendeleza nchi wanakwazika. Wale wasiopenda kujihusisha na 'Ulaghai' huamua kujitenga na waongo hao. Wanasiasa hao hujikuta wamebaki na makundi ya watu ama wenye uelewa mdogo, au washabiki kupindukia kiasi wanakuwa na upofu wa kuona kasoro ndani ya chama, au wale wanaofaidika kwa namna fulani (wachumia tumbo).
Juliana Shonza alianzisha shutuma za mpango wa Dr. Slaa kumuua Zitto Kabwe ambazo zilidakwa na gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013.
quote_icon.png
By Juliana Shonza

KUHUSU BEN SAANANE NA KUTUMIKA KUMUUA ZITTO KABWE

Wana jf, Nakili wazi hili swala lilitokea mnamo mwezi wa 5 mwaka 2012 tukiwa Lunch time hotel external kwenye mazungumzo ya kawaida(ambavyo ben saanane anaita ni vikao vya kuhujumu chama). Siku ya tukio tukiwa meza moja na Ben Saanane mkono wake wa kushoto alifunga bandeji akidai ameumia mkono(nakumbuka). Kwa babati mbaya sana katika maongezi yale Ben alilewa pombe (alikuwa anakunywa bia(kilimanjaro). Kulewa kwake pombe alijisahau na kutoa bahasha ya kaki yenye fedha, ndani ya bahasha ile wakati wa kutoa fedha alipe huduma ya chakula na vinywaji alidosha karatasi ya nailoni ndogo ikiwa na unga mwekundu ndani.

Tulimuuliza ni nini hicho akadai ni kuberi,na kuing'ang'ania tusifungue(aliyekiokota ni mwampamba).Lakini Mwampamba aligoma kumpa na kudai lazima ifunguliwe pale pale.

Ben saa nane akiwa katika hali yake ya kulewa alifura kwa hasira kutaka arudishiwe ilekaratasi,haliiliyopelekea uvunjifu wa amani pale lunch time hotel.Mwampamba aliondoka na mzigo ule kwa kukimbia nao, usiku ule Ben alitafutana na mwampamba hadi nyumbani kwake(temeke) akidai huo mzigo(ikumbukwe mwampamba na mm nimeishi kwake na nikaka yangu) . Lakini katika hali ya kusikitisha ben aliomba mzigo ule usiende mbali na kuahidi atasema kweli kile ni nini.

Ben saanane alikili wazi kwamba ile ni sumu lakini anapeleka nyumbani kwa ajili ya kuulia panya, Swala hili halikuishia usiku ule,ben hakufanikiwa kupata mzigo ule kesho yake asubuhi(jumapili) alikwenda kumsihi mwampamba ampatie mzigo.

Sharti lilikuwa aseme ni nini kwasababu huwezi kuwa na sumu eneo la starehe kama pale hotelini huku akisisitiza kuonana na zitto ambaye alisafiri usiku ule kwenda marekani bila kuonana na yeyote kati yetu?

Ndipo Ben saanane akakili ile ni sumu akilenga kumpatia zitto akiwa ametumwa na Dr.slaa.Tulihamaki kusikia kile kitu(hapa tulikua tabata reli stand tukisubiri usafi).Nilimuuliza uthubutu wake wa kufanya kitu kama hicho na kwanini afanye unyama huo,akadai ametumwa Kisa kikiwa ni zitto kumsakama dr.slaa ndani ya vikao vya chama.

Swala hili lilifika mbali kwa kuwekeana mipaka ya kula vyakula mahotelini na kutoshirikiana tena katika ushikaji wetu
kama masalia.

Lengo la Juliana Shonza lilikuwa kuchonganisha viongozi wa juu wa CHADEMA (Katibu Mkuu na Makamu wake) na kuchafua taswira ya Katibu Mkuu kwa umma.

Leo hii Zitto mwenyewe amekanusha tuhuma hizo kuwa si za kweli https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/424280-siri-ya-kuuwawa-zitto-uwongo.html. Jibu la Zitto linaweza kuwekwa kifupi kwa ujumbe wa twitter aliotuma Zitto mwenyewe:

Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe 2h Mtanzania leo imeandika habari 'Siri ya kuuwawa Zitto yafichuka'. Habari hii sio ya kweli. Sijawahi kukutana na Ben Saanane hata siku moja 3:09 AM - 27 Mär 13 ·


Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe 2h Pia sijawahi kufika na wala siijui Hotel ya Lunch Time Mabibo. Ninaomba Mtanzania wathibitishe na vyanzo vyao habari hiyo 3:11 AM - 27 Mär 13 ·

Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe 2h Siamini kabisa kwamba Katibu Mkuu CHADEMA anaweza panga kuniuwa mie. Hana sababu kufanya hivyo. 3:12 AM - 27 Mär 13·
Juliana Shonza anaonekana ni muongo, na kwa kuwa anawakilisha CCM, propaganda za CCM zinaanza kuthibitika kuwa zinatumia uongo pia.

ANGALISHO
Japo uongozi uliopo sasa wa CCM una vijana Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, Lusinde, HKigwangallah n.k), ambao wako tayari kutumia propaganda za majitaka, bado kuna wazee wenye busara: Mangula, Msekwa, Salim, Warioba n.k. ambao sina hakika kama wanafurahia mwenendo wa chama kuanza kuonekana WAONGO.

Wazee kwa vijana, busara itumike ili hao WALIOFUKUZWA CHADEMA, wasiwe chanzo cha kuharibika kwa Taswira ya Chama machoni pa watu wenye hekima zao.

Uongo unaweza kuleta faida za muda mfupi lakini unaweza kusababisha madhara ya muda mrefu.

CCM, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba wamepokewa ndani ya chama baada ya kufukuzwa CHADEMA. Kuweni waangalifu kama kweli mmepata au mmepatikana.
 
Last edited by a moderator:
Nikiwa katika upekuzi wangu ndani ya mitandao ya kijamii nimefanikiwa kupita katika facebook wall ya MTELA MWAMPAMBA na aliyoyaandika yamenistua na kuanza kunifanya kumuogopa. Katika kipindi cha nyuma pale ambapo alifanya makosa makubwa ya kukihujumu chama cha chadema akiwa na mwenzie Shonza, Mchange na baadhi ya vijana wengine, niliendelea kumdharau na kumuona ni mtu ambaye hana maana, lakini pia niliamini kuwa hana madhara yeyote kwa chama wala kiongozi wa chama.

Lakini sote tutakuwa mashahidi hapa kuwa tangu kutokea kwa sakata hilo mwishoni mwa mwaka jana, mambo yameanza kwenda kombo kwa kasi ya hali ya juu, hasa kwa siri mbalimbali kuvuja na kuondoka kwa staha ya chama mbele ya jamii. Hali iliyopelekea tahamaki kwa viongozi na wanachama pia.

Mtakubaliana na mimi kuwa yanayoendelea hivi sasa ndani ya chama yanatokana na kuondolewa kwa vijana hawa ambao kumbe walikuwa na siri nyingi na wameshiriki katika mambo mengi kiasi kwamba kila siku zinavyozidi kwenda yanaibuliwa mambo mapya na kuvuja kwa tuhuma mbalimbali.

Kilichonistua sasa ni juu ya Kijana huyo ambae mara ya kwanza niliamini kabisa kuwa ni masalia aliyekuwa anatumika na wanaCCM kuihujumu Chadema, na akiwa target yake kubwa ni Dr. Slaa alivyoanza kugeuza upepo kwa mtu ambae amedai kuwa ni rafiki yake wa karibu ndani ya chadema na kutoa maneno mazito juu yake.

Nitanukuu baadhi ya maneno hayo ambayo yapo katika wall ya mtela:

Kwa anayenifahamu na kuifahamu Chadema na Viongozi wake atakubaliana na ukweli kuwa MIMI, MTELA MWAMPAMBA nilikuwa karibu zaidi na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe.

Kwa kuwa LENGO langu si KUFITINISHA wala KUJIHUSISHA NA CHAMA CHAKE, Nitabainisha (kwa Ufupi) namna ninavyomfahamu ZITTO ZUBER KABWE, tena ikibidi nitabainisha kinagaubaga na wazi wazi (kama italazimu kufanya Hivyo) kiasi Umma ubaini ni nani ZITTO ZUBER KABWE ndani ya Chama: mjenzi, nguzo, mhimili ama mhujumu Chama. Nafanya hivyo kwa lengo la kutetea maslahi ya Kitaifa, maana watu hawa wanabeba nembo na sura ya Utaifa, na ni ubaya ulioje watu wasio na DHATI ya kiutawala kuaminiwa katika Utawala.

Ni kwa msukumo huo ninajikuta ninao wajibu wa kuwabainishia UMMA juu ya mambo hayo manne ambayo ZITTO ameyasema.(Kwa maana sitaeleza lini na wapi nimekutana na ZITTO.,sitaeleza tunafahamiana kiasi gani na tuliwahi kupanga lipi na wapi, sitasema tulifanikiwa mangapi na kushindwa mangapi, sitaeleza “sura halisi” ya ZITTO ninayoifahamu mimi kuliko mtu yeyote mwingine katika Chadema (ILA NASISITIZA KUWA NITAFANYA HIVYO TU PALE ITAKAPOBIDI)

Kwa maana yote yanayoendelea Chadema yanatokana na Mvutano na Kadhia ya CHUKI na VISASI baina ya Makatibu wawili wa Chama hiko, hata kuondoka kwangu na wengine ni kafara ya jambo hilo. Kuna mambo si sahihi kuyaeleza kiundani na hadharani kwa sababu tuliambizana na kupanga kwa Usiri na Kuaminiana, hatujafikia hatua hiyo ya kuuvunja hata Uaminifu tuliopeana kwa Viapo ila kama tutaendelea na maneno ya namna hii na UZANDIKI, ipo siku tutayasema.

. Ni wazi kuwa tumehojiwa katika vikao kadhaa ndani ya Chadema na kote hakuna ambako tulitaja jina lako wala kukuhusisha na chochote kuhusu sisi. Usijiachie sana katika mazungumzo yako, wakati mwingine neno huweza kuzaa yale usiyoyatarajia.
Karata yako ya mwisho inayo-determine maisha yako kama mwanachadema iko mikononi mwetu, Please brother, Don’t mess with your last poker chip, u will lose the game.

Kauli yangu Moja ya Ushuhuda inamaliza Uhai wako ndani ya Chadema., I know you’re smart brother, don’t get crossed., straighten your words..!

Kuwa makini, AND THIS IS SERIOUS…!

Ni kwa maneno haya nimeanza kumuogopa mwampamba lakini kama haitoshi amedai anazo meseji mbalimbali kutoka kwa Slaa na Josephine ambazo zinaelezea taarifa nyeti juu ya kinachoendelea chadema na amenukuu moja ya sms ya JOSEPHINE aliyosema imetumwa tarehe 22/07/2012.

Mimi nimeanza kumuogopa kwa maana haya si tu yanatoa vitisho kwa mtu lakini ni hatari kwa afya ya chama ikiwa kila kukicha siri za vikao vya ndani vya chama vinaweza kutoka nje tena kwa mtu kama mwampamba, ambae anaropoka popote na kwa yeyote kama alivyosema katika wall yake kuwa,
ZITTO na viongozi wengine wanajua nini kimesemwa kuhusiana na Sakata letu ndani ya Kamati Kuu iliyopita na Jinsi hoja hiyo ilivyosababisha Kikao hiko kutahamaki pindi mwenyekiti alipoizima, lakini anafahamu kuwa Kikao Cha Kamati Kuu ijayo kitamjadili yeye (ZITTO) na SHIBUDA na BEN ni miongoni mwa watu watakao toa Ushuhuda wa aliyoyatenda ZITTO katika CHADEMA na juu ya anayoyasema yeye BEN katika mitandao ya Kijamii

WE ARE NO LONGER SAFE..,kuna mirija ya habari na upashikuna bado unaendelea ndani ya Chadema ukiongozwa na masalia walioondoka na baadhi waliobaki.,TUCHUKUE HATUA KWA UANGALIFU, na TUCHUKUA HATUA SASA.
 
Debe tupu haliachi kupiga kelele.Njaa inamsumbua huyo Dogo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom