KUNGUNI 2010
Member
- Apr 27, 2014
- 27
- 1
warioba usitiswe na mtu yeyote yule walitaka uwe fisad kama wao endelea kuonyesha ushupavu wako
Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba amewasaliti,mfukuzeni. Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba na Tume yake 'wamepika' Rasimu kwa chuki na hila zao na kuacha maoni ya wananchi kama mnavyodai,mfukuzeni chamani mwenu. Kama kweli mnaamini kuwa mnahitaji muda wa kutosha wa kumkashifu,kumtusi,kumsimanga na kumkebehi Jaji Warioba ndani ya chama chenu,Bungeni na kwingineko,mtimueni chamani kwa kumvua uanachama wake.
Mkifanya hivyo itakuwa poa. Mtakuwa na kila nafasi na muda wa kusema mtakayo juu yake. Wafuatiliaji wa siasa za nchi hii mnatuchosha. Tunawaona ni wa ndimi-mbili kuigiza kumponda Jaji Warioba wakati mnaye chamani.Na mnamheshimu kama Kada mkongwe na mtiifu kwa chama. Kama mmeweza kumfukuza Mansoor wa Kiembesamaki hivi karibuni,mnashindwa nini kwa Jaji Warioba.
Kama hamuwezi,mwacheni Jaji Warioba asimamie anachokiamini. Asimamie Maoni ya Wananchi aliyoyakusanya na Tume yake toka sehemu mbalimbali za nchi hii na kuyaainisha katika Rasimu. Msiendelee na kuonyesha mchezo wa kuigiza.
Mkataba ungevunja Muugano maana ingekuwa sawa na ilivyo East Africa Community. Na hadidu rejea zilisema Muungano uboreshwe na sio kuvunjwa.
Hivyo namna pekee ya kudumisha Muungano na kuondokana na kero za miaka 50 ni serikali 3, pendekezo ambalo linakubalika Zanzibar (badala ya serikali 2).
NDANI YA CCM MWENYE AKILI NI MWENYEKITI BASI. SIKU JEYKEY AKIBADILI MSIMAMO ( NAAMINI ATABADILI TU KWANI UINGEREZA NA MAREKANI WALISHASEMA MAONI YA WANANCHI YAFUATWE BASI NAO WAO WATAFUATA TU) NA WENGINE WOTE WATAIMBA SANTURI HIYO YA JEYKEY....NDANI YA VIKAO WAJUMBE HUWA WANAPELELEZA SANA KUJUWA NINI MSIMAMO WA MWENYEKITI ILI KUEPUKA KUTOFAUTIANA NAYE...
KUMBUKA KWENYE KIPINDI CHA JENERALI ON MONDAY....MTAZAMAJI MMOJA ALISIKITIKA SANA KUHUSU MATUSI,KEJELI NA MIPASHO KWENYE BUNGE LA KATIBA. JENERALI ALISEMA ."....HIVYO NDIVYO VIKAO VYA CCM VINANYO ENDESHWA, NIMEYASHUHUDIA SANA NA KWA UHAKIKA HALI HUWA HIVYO NDANI YA VIKAO..."
JAJI WARIOBA KWENYE DK 45 (ii) ALISEMA RAIS ALIPEWA HABARI NA TAARIFA YA KILA HATUA YA MCHAKATO WA KATIBA NA MAUDHUI YA RIPOTI NZIMA. SASA NINI ANACHOKIFANYA SASA????
devagy...naona una hasira na kila anaye kwenda tofauti na wewe...mimi nimeripoti nilichosikia.sasa hebu nionyeshe ni wapi nimesama mambo ya mbowe na lissu?. Marehemu jaji nyalali alipotoa ripoti yake mbowe na lissu hawakuwa wanajulikana kwenye siasa za nchi hii lakini naye alisema serikali tatu. White paper ya jaji kisanga nayo serikali tatu, jaji warioba haye serikali tatu. Je nao ni wanachama wa chadema? Mwakyembe mwanafunzi wa llm naye alisema serikali tatu je naye ni mwanachadema? Tufike mahali tukubali muungano wetu una matatizo ya kimsingi sio hizo changamoto na kero zinazo ripotiwa na serikali yetu.
Mbowe lissu na wengine wenye mawazo tofauti nao ni watz na wana uhuru wa kuwa na mawazo tofauti na mtu yeyote. Na kila anayekuwa na mawazo tofauti si cdm wala mpinzani ndo ubinadamu huo, ninachopinga mimi ni matusi, kejeli na mapovu yanayotolewa na baddhi ya wajumbe wa bunge wa ccm....katiba haiundwi hivyo