Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
CCM Mbeya Mjini yajipanga kukomboa jimbo 2015
Imeandikwa na Na Joachim Nyambo, Mbeya; Tarehe: 8th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 80; Jumla ya maoni: 0
BAADA ya kupoteza ushindi katika Kata 14 na hata Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapa kimeanza mikakati ya kuhakikisha kinajipanga upya ili kurejea katika sura yake ya awali itakayowafanya wananchi kurejesha imani.
Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wilayani hapa, Athanas Kapunga aliyasema hayo Alhamisi alipokuwa anatoa maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wa viongozi wa chama hicho uliowajumuisha pia wenyeviti na makatibu wa mashina, madiwani pamoja na viongozi
wa mitaa wanaotoka kwenye chama hicho.
Kapunga alisema wameona hakuna sababu ya chama ngazi ya wilaya kuanza kujihusisha na migogoro inayoonekana kuibuka katika ngazi ya za juu, wakati katika ngazi yao hawajashughulikia ile inayoonekana kukitafuna chama.
Tumeona tuanze kwanza kutatua yale yanayokizorotesha chama katika ngazi yetu. Maana hayo ndiyo yaliyofanya tukapoteza jimbo na baadhi ya kata katika uchaguzi mkuu wa mwaka
2010. Ukweli ni kuwa Wana- CCM wenyewe ndiyo waliohusika kuligawa jimbo kwa wapinzani. Sasa hatutaki haya yaendelee tukabaki kushabikia migogoro ya juu, alisema.
Alibainisha kuwa makundi na kugeukiana ndiko kulikoifanya CCM iuone mwaka jana kuwa mwaka mbaya, lakini hali hiyo inapaswa kuchukuliwa kama fundisho kwa wanachama kuhakikisha wanajipanga na kuwa na umoja unaolenga kulinda maslahi ya chama chao.
Kapunga ambaye pia ni mstahiki Meya wa jiji la Mbeya, ameitaja mikakati ya kukirejeshea heshima chama kuwa ni pamoja na kuhakikisha vikao vya mara kwa mara vinafanyika katika ngazi za kata na mitaa ili wajumbe na wanachama kupeana taarifa za utekelezaji wa majukumu ya kila mmoja.
Alisema hatua nyingine ni kuhakikisha wanachama wanakuwa wafuatiliaji wa mambo yanayoendelea kwenye maeneo yao ikiwemo utatuzi wa kero za wananchi pamoja na kuufahamisha uongozi wa juu wa chama juu ya kero zinazozikabili jamii zinazowazunguka.
Alisema wanachama kuacha uoga wa kutaja yale yaliyotekelezwa na serikali ikiwa ni katika utekelezaji wa Ilani ya chama ni jambo jingine ambalo litakisaidia chama kwa kiasi kikubwa
kwa wananchi kujua nini kimefanywa na kipi bado, lakini lini kitatekelezwa.
Katika uchaguzi wa mwaka jana, msanii wa muziki wa kizazi kipya, Joseph Mbilinyi `Mr II au `Sugu alinyakua ubunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baada ya kumshinda mpinzani wake wa karibu, Benson Mpesya wa CCM.
Imeandikwa na Na Joachim Nyambo, Mbeya; Tarehe: 8th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 80; Jumla ya maoni: 0
BAADA ya kupoteza ushindi katika Kata 14 na hata Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapa kimeanza mikakati ya kuhakikisha kinajipanga upya ili kurejea katika sura yake ya awali itakayowafanya wananchi kurejesha imani.
Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wilayani hapa, Athanas Kapunga aliyasema hayo Alhamisi alipokuwa anatoa maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wa viongozi wa chama hicho uliowajumuisha pia wenyeviti na makatibu wa mashina, madiwani pamoja na viongozi
wa mitaa wanaotoka kwenye chama hicho.
Kapunga alisema wameona hakuna sababu ya chama ngazi ya wilaya kuanza kujihusisha na migogoro inayoonekana kuibuka katika ngazi ya za juu, wakati katika ngazi yao hawajashughulikia ile inayoonekana kukitafuna chama.
Tumeona tuanze kwanza kutatua yale yanayokizorotesha chama katika ngazi yetu. Maana hayo ndiyo yaliyofanya tukapoteza jimbo na baadhi ya kata katika uchaguzi mkuu wa mwaka
2010. Ukweli ni kuwa Wana- CCM wenyewe ndiyo waliohusika kuligawa jimbo kwa wapinzani. Sasa hatutaki haya yaendelee tukabaki kushabikia migogoro ya juu, alisema.
Alibainisha kuwa makundi na kugeukiana ndiko kulikoifanya CCM iuone mwaka jana kuwa mwaka mbaya, lakini hali hiyo inapaswa kuchukuliwa kama fundisho kwa wanachama kuhakikisha wanajipanga na kuwa na umoja unaolenga kulinda maslahi ya chama chao.
Kapunga ambaye pia ni mstahiki Meya wa jiji la Mbeya, ameitaja mikakati ya kukirejeshea heshima chama kuwa ni pamoja na kuhakikisha vikao vya mara kwa mara vinafanyika katika ngazi za kata na mitaa ili wajumbe na wanachama kupeana taarifa za utekelezaji wa majukumu ya kila mmoja.
Alisema hatua nyingine ni kuhakikisha wanachama wanakuwa wafuatiliaji wa mambo yanayoendelea kwenye maeneo yao ikiwemo utatuzi wa kero za wananchi pamoja na kuufahamisha uongozi wa juu wa chama juu ya kero zinazozikabili jamii zinazowazunguka.
Alisema wanachama kuacha uoga wa kutaja yale yaliyotekelezwa na serikali ikiwa ni katika utekelezaji wa Ilani ya chama ni jambo jingine ambalo litakisaidia chama kwa kiasi kikubwa
kwa wananchi kujua nini kimefanywa na kipi bado, lakini lini kitatekelezwa.
Katika uchaguzi wa mwaka jana, msanii wa muziki wa kizazi kipya, Joseph Mbilinyi `Mr II au `Sugu alinyakua ubunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baada ya kumshinda mpinzani wake wa karibu, Benson Mpesya wa CCM.