CCM lazima ife ili Watanzania waendelee

CCM lazima ife ili Watanzania waendelee

JUST

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2010
Posts
552
Reaction score
236
ndugu wanaJF,

kama kweli tunaipenda nchi yetu tajiri yenye asali na maziwa basi ni busura kukubaliana kwa pamoja kuwa ili ustawi wa wananchi uweze kumea vizuri ni lazima CCM ife kwa sababu zifuatazo:

1. imekuwa na tabia ya kuingia kwenye mikataba ya kunyonya nchi na wananchi wake.

2. imekuwa na tabia ya kukusanya kodi kwa masikini na kuwaacha matajiri

3. imekuwa ikitoa upendeleo kwa nafasi za tenda,ajira kwa ndugu, jamaa na marafiki zao wasio kuwa na vigezo huku watoto wa wakulima wakiachwa hali wanavigezo vyote.

4. imekuwa ikiwatosa watoto wa wakulima kwa nafasi za kisiasa ndani ya chama na kuwapa ndugu, jamaa na marafiki zao.

5. mbaya zaidi imewaadaa watanzania kwa ahadi nyingi nzuri za matumaini bila ya kutekelezwa kwa miaka 51

6. imesababisha matabaka ya kielimu kwa kuruhusu uwepo wa shule za msingi za pesa nyingi na kwa lugha ya watu(waingereza na wengine) ambazo mtanzania wa kawaida ukimuacha masikini anashindwa kuwapeleka na mbaya zaidi wameziita kayumba na za juu yake kata.

7. imeacha kupima viwanja na kusababisha bei ya viwanja kukuzwa bila sababu ili hali ardhi yetu ni kubwa kuzidi nchi ya kenya na uganda kwa pamaoja. hali hii imesababisha wenye viwanja kuwa ni wale wale wanaoiba kodi zetu pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao.

8. imeuwa viwanda na reli na kuruhusu ndugu, jamaa na maraki zao kugeuza viwanda maghala na kufanya barabara mbadala wa reli ili malori yao yatumike. hali hui ndio moja ya vyanzo vya mfumuko wa bei unaomuumiza mwananchi.


kwa kweli mambo ni mengi hatua ya kuchukua ni kukipumzisha kwa amani tu kupitia sanduku la kura.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo katika kijiji cha Saza Jimbo la Songwe Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya baada ya kunyakua kiti cha Mwenyekiti wa kijiji na vitongoji vyote sita vya kijiji hicho.

Msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Weston Njeje, akizungumza na NIPASHE jana kutoka Chunya alisema mgombea wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Saza kupitia CCM, Philipo Mwakitalima, ameshinda kwa kupata kura 367 na kumshinda mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Robert Nselu, aliyeambulia kura 19.


Kwa stahili hii CCM itakufa????????
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo katika kijiji cha Saza Jimbo la Songwe Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya baada ya kunyakua kiti cha Mwenyekiti wa kijiji na vitongoji vyote sita vya kijiji hicho.

Msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Weston Njeje, akizungumza na NIPASHE jana kutoka Chunya alisema mgombea wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Saza kupitia CCM, Philipo Mwakitalima, ameshinda kwa kupata kura 367 na kumshinda mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Robert Nselu, aliyeambulia kura 19.


Kwa stahili hii CCM itakufa????????

hongera kwa ushindi huo japo unanipa mashaka sababu umekumbwa na vurugu lakini unakubaliana na sababu hizi au unazikataa?
 
Kife mara ngapi mkuu! Sema ni Lazima kizikwe ili watanzania waendelee.....,
 
ndugu Domy kufa si mpaka tuone pumzi imetoweka kwa sasa naona imewekewa mashine ya oksijeni baada ya kuwa mahututi sasa ni nani wa kuzima mashine ili tuzike?
 
Ccm itakufaje wakati inapambana na vyama vidhaifu vyenye kwashakoo ya ukabila na udini kama cuf na chadema
 
Ccm itakufaje wakati inapambana na vyama vidhaifu vyenye kwashakoo ya ukabila na udini kama cuf na chadema


sawa lakini je unakubaliana na matatizo niliyoyataja hapo mwanzo wa mada?
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo katika kijiji cha Saza Jimbo la Songwe Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya baada ya kunyakua kiti cha Mwenyekiti wa kijiji na vitongoji vyote sita vya kijiji hicho.

Msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Weston Njeje, akizungumza na NIPASHE jana kutoka Chunya alisema mgombea wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Saza kupitia CCM, Philipo Mwakitalima, ameshinda kwa kupata kura 367 na kumshinda mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Robert Nselu, aliyeambulia kura 19.


Kwa stahili hii CCM itakufa????????
rhebu msikie kamanda nassari
Uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa 9 ya mamlaka ya mji mdogo USA River wilayani Arumeru. Mitaa yote ilikuwa chini ya CCM. Leo baada ya Uchaguzi CHADEMA 6, CCM 3. Kwa maana nyingine CDM itaongoza mamlaka ya mji mdogo Usa River.
CCM walileta mawaziri, kwa CDM nikakomaa na Makamanda wenzangu the underdogs lakini hatimaye imedhihirika uongo hauwezi kuushinda ukweli.

TULIANZA NA MUNGU, TUTAMALIZA NA MUNGU.
 
Yote amesama ya ukweli kuhusu CCM lakini Yupi au Chama gani kinaweza kuboresha maisha ya Wananchi wao na kuacha Rafiki anateseka na Jembe kijiji.Hongera kwa kusababisha Kifo cha CCm kwahiyo Mazishi lini?
 
jitahidi kueneza sumu, ila angalia isije kukudhuru mwenyewe, mana waswahili walisema 'chanda chema.......
 
Yote amesama ya ukweli kuhusu CCM lakini Yupi au Chama gani kinaweza kuboresha maisha ya Wananchi wao na kuacha Rafiki anateseka na Jembe kijiji.Hongera kwa kusababisha Kifo cha CCm kwahiyo Mazishi lini?
maziko rasmi ya ccm ni 2015.kaburi la ccm litafunikwa kwa zege
 
Angalia usije kutangulia wewe kufa kabla ya CCM chama makini.
 
Angalia usije kutangulia wewe kufa kabla ya CCM chama makini.
hata akitangulia haina maana kuwa alichokisemasio kweli mkuu.
kwa undani ni kama mguu uliopata kansa alafu daktari anakwambia waukate, mgonjwa akifikiria maisha bila mguu atasema hapana lakini hiyo ndio dawa japo chungu. Ukweli daima uuma

 
Siku tutakayoanza maisha bila CCM, ni siku ambayo kila mtz ataamini na kuelewa kuwa kumbe inawezekana.....

Inawezekana kwenye kila kitu, mtazamo wa watu juu ya siasa kuwa sio mchezo kama inavyoaminishwa itakuwa bayana...

Na ndio siku hili taifa litaanza kujengwa rasmi mbali na unafiki na hii funika funika inayoendelea saiv kwenye sekta zote...

Tuzidi kuisogelea hiyo siku tu......
 
rhebu msikie kamanda nassari
Uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa 9 ya mamlaka ya mji mdogo USA River wilayani Arumeru. Mitaa yote ilikuwa chini ya CCM. Leo baada ya Uchaguzi CHADEMA 6, CCM 3. Kwa maana nyingine CDM itaongoza mamlaka ya mji mdogo Usa River.
CCM walileta mawaziri, kwa CDM nikakomaa na Makamanda wenzangu the underdogs lakini hatimaye imedhihirika uongo hauwezi kuushinda ukweli.


TULIANZA NA MUNGU, TUTAMALIZA NA MUNGU.

No more comments!! Hebu leta na statistics za Moshi!
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo katika kijiji cha Saza Jimbo la Songwe Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya baada ya kunyakua kiti cha Mwenyekiti wa kijiji na vitongoji vyote sita vya kijiji hicho.

Msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Weston Njeje, akizungumza na NIPASHE jana kutoka Chunya alisema mgombea wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Saza kupitia CCM, Philipo Mwakitalima, ameshinda kwa kupata kura 367 na kumshinda mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Robert Nselu, aliyeambulia kura 19.


Kwa stahili hii CCM itakufa????????......

Itakufa tu! Si hujuma na hadaa walizoanza kufanya kabla? Ili kudhoofisha upinzani!
 
Back
Top Bottom