CCM: Kutoka kuchekeana hadi kutishana

CCM: Kutoka kuchekeana hadi kutishana

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Naendelea kuamini kuwa CCM ni mfumo ulioshindwa katika utawala wa nchi hii. CCM kama chama kimekuwa na tabia ya kulindana na kuchekeana hata pale viongozi wa umma na wa kichama wanapokiuka sheria na taratibu za nchi na chama. Wapo viongozi wa umma waliokumbwa na kashfa za wizi/ufisadi wakiwa madarakani. CCM ikaishia kuwashurutisha waachie ngazi na mambo yakaishia hapo.

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kushtaki akabaki kimya na viongozi husika wakaendelea kutesa uraiani.

Leo hii katika mchakato wa kumpata mgombea wao,makada wa CCM wanatishana. Wanatishana kwakuwa makada hao wanajiona na kuaminisha wananchi kuwa wao ni watu safi kwakuwa tu hakuna kumbukumbu ya mashtaka dhidi yao. Kule kuchekeana na kulindana ndiko kunakowafanya makada hao watambe sasa na kutishia hata uhai wa chama.

Eti hadi mtuhumiwa wa ufisadi leo anakitisha chama chake? DPP angeshamaliza kazi kwa kumburuza mahakamani leo hii asingekuwepo hapo kutishia kuwa akikatwa jina patachimbika.

Nasema tena na tena CCM ni mfumo ulioshindwa na hauwezi tena kutupa Rais mwenye mapenzi mema kwa watanzania. Naye ataanzia kwenye kulindana na kuchekeana na kuishia hapa kwenye kutishana. Muda wa maadiliko ya kimfumo ni huu watanzania wenzangu.
 
wacha waparuane kila kitu kina mwisho wake. hili jumba letu la dhahabu ccm ndo linapukutika hivyo kila mtu anajizolea chake mwisho wa yote halitakaliwa na mtu hata mmoja. litakuwa gofu soon.
 
wacha waparuane kila kitu kina mwisho wake. hili jumba letu la dhahabu ccm ndo linapukutika hivyo kila mtu anajizolea chake mwisho wa yote halitakaliwa na mtu hata mmoja. litakuwa gofu soon.

Na iwe hivyo,hakuna namna nyingine
 
Petro E. Mselewa nashangaa eti na wewe ni mwanasheria! mwanasheria gani asiyejua kumpeleka mtu mahakamani lazima uwe na evidence zinazokidhi mahitaji kisheria na sio kisiasa.
Ni kesi ngapi serikali imepeleka mahakamani na ikashindwa kwa sababu zinazofanana na hizo? ama kweli sio kila mwanasheria anayeelewa sheria.
 
Last edited by a moderator:
......pamba nyeupe anautishia mfumo uliomlea!!!!!!! umemkuza, unamjua, ukiamua kummaliza anaisha!!!! najua hata yeye anajua hili, ila anacheza na watanzania wajinga, ambao ni wengi kwa idadi, lakini jinsi wakati unavyokwenda wanapungua, naamini wakati ukifika watatoa dozi kupitia sanduku la kura!!!
 
Twaweza sikia mjumbe wa mkutano mkuu kamzaba Kofi mwenyekiti na tukaambiwa tusiingilie hayo ni mambo yao ya ndani na kukua kwa democracy ndani ya chama.
 
Chama Cha Mapinduzi kimeshindwa kutumia uwingi wake katika bunge la jamhuri ya muungano kuisimamia serikali itekeleze maazimio mbalimbali yaliyofikiwa katika skendo mbalimbali za kifisadi. Na kuishia kupiga kelele muda wa skendo na baadae kuwaachia wezi wakuu wakitanua mtaani.

Si hivyo chama kimeshindwa kutekeleza maazimio waliyojiwekea ndani ya chama kuhusiana na mafisadi, ile KUJIVUA GAMBA iliishia ngonjera majukwaani. Katika hali kama hii CCM hawana kibali wala mamlaka yakutuambia wanaweza kutokomeza ufisadi, wizi na rushwa.
 
ccm ni genge la mafisadi. mwenye mtandao mkubwa ndani ya chama huchaguliwa kuwa kiongozi.
 
Wakati ni ukuta,mikono ya wanaccm inauma sasa kwa kujaribu kupambana nao.
 
Petro E. Mselewa

Una mtazamo mzuri, ila mkuu amini kuna watanzania wendawazim wa. Kiwango cha ajabu! Hawatakuelewa na hawatataka kusikia ulichoandika
 
Last edited by a moderator:
hata mnara wa babeli ulianguka,
Yes it is true.

Hakuna chochote kilichokuwa na mwanzo hapa duniani kikakosa kuwa na mwisho.

Most likely now than ever before, CCM inaelekea kuvifuata vyama vyenzake vikongwe vya KANU cha Kenya, UNIP ya Zambia na MCP cha Malawi kule vilikokwenda ambako vilishindwa kurejea kwenye 'system' na badala yake vimepotea milele.
 
Twaweza sikia mjumbe wa mkutano mkuu kamzaba Kofi mwenyekiti na tukaambiwa tusiingilie hayo ni mambo yao ya ndani na kukua kwa democracy ndani ya chama.
ushahidi huu hapa .
 

Attachments

  • attachment-10.jpeg
    attachment-10.jpeg
    9.5 KB · Views: 2,183
  • attachment-2.jpeg
    attachment-2.jpeg
    4.4 KB · Views: 2,169
Learned brother,

Amini nakwambia, hata nyoka mwenye makengeza ambaye wamekuwa wakimlinda na kumtetea, atakuja kuwatesa sana CCM.
 
Back
Top Bottom