Kwa upande wao wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kupitia kundi la vijana, walisema kuwa watamlinda kwa gharama yoyote Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete pamoja na kuhakikisha kuwa anapata kura zote za ‘ndiyo.' Mbali na hilo, vijana hao walisema kuwa watafanya kila njia kumsaka mtu aliyetengeneza vipeperushi hivyo vinavyosambazwa dhidi ya mwenyekiti wao, Rais Jakaya Kikwete.
Wajumbe hao saba kati ya kumi waliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dodoma na kutoa tamko hilo, huku wakieleza kuwa hawatalala hadi watakapoona mwenyekiti wao akiibuka na ushindi wa kishindo.
"Sisi ndiyo jeshi la chama. Itakuwa ni aibu kama mwenyekiti wetu atakuwa akidhalilishwa kwa kupata kura chache, ilhali nasi tupo. Lazima kuwaaibisha watu wa aina hiyo na kuwasaka popote walipo. Tunaomba vijana wenzetu watuamini kuwa tuko Dodoma kufanya kazi hiyo," alisema Jery Silaa kwa niaba ya wenzake.
chama gani ambacho nafasi ya uenyekiti hugombaniwa kidemokrasia?? Kitaje!!
Nacho ni chama cha siasa!?Chama chetu cha kuweka na kukopa
Nacho ni chama cha siasa!?
Mimi nimelielewa jibu lako!!Swali lako la awali umelielewa?
wewe unafahamu maana ya uhaini au umbea tu?
Kwa hiyo fomu huwa ni kiini macho tu ila anayetakiwa kuwa Mwenyekiti anakuwa ameshajulikana?Lakin hawa Jamaa wameizid, Wenzao hutoaga hata fomu..
chama gani ambacho nafasi ya uenyekiti hugombaniwa kidemokrasia?? Kitaje!!
kila kitu uhaini.je,tutafika?
Huu ndiyo ukweli ndugu yangu kwetu sisi waafrika ambao siasa ni njia ya kufanikiwa kimaisha hiyo hali ya kuchagua Mwenyekiti wa chama cha siasa kidemokrasia bado sana, ingawa kila mmoja wetu huona ni "demokrasia" pale yule anayemuunga Mkono "anapochaguliwa" kuwa Mwenyekiti.Democratic na Republican vya Marekani lakini kwa waafrika wagaganga njaaa baaaaaaaaaaaaado sana
Hawajampinga Rais, wamempinga Mwenyekiti wa Magamba