CCM inatafuta huruma ya wazungu!!

CCM inatafuta huruma ya wazungu!!

Borakufa

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2011
Posts
1,503
Reaction score
390
Baada ya kuona mambo yamewabana kona zote katika kampeni za uchaguzi mkuu ujao(25.10.2015) na ili kuhakikisha wanabaki madarani kwa njia yoyote ile,katibu mkuu wa chama cha mapindizi ndugu,kanal Abulahman Omary Kinana (Bingwa wa propaganda)ametupia makala katika mtandao wa The Hill wa usa ili kutafuta nafuu pale watakapoanza kulikoroga kura zisipotosha.

Makala hiyo ambayo ameipa jina la ''Tanzania haiwezi kuruhusiwa kuwa uwanja mpya wa magaidi'' Kanal kinana amemunganisha mgombea urais kupitia chama cha CHADEMA na mashekh wa zanzibar (uamsho)ambao wako kizuizini kwa tuhuma za ugaidi.

Katika makala yake kanal Kinana anawadhibitishia wamarekani na dunia kuwa wale masheikh wa znz ni magaidi na wana mahusiano na magaidi wa boko harama wa huko afrika magharibi/kaskazini.

Eti kwa kuwa mh.Lowasa alisema,kama akishinda kiti cha urais atapitia mashauri ya hao masheikh ili kuona kama haki inatendeka, kanal Kinana anawaambia wazungu kuwa Lowasa kuwa rais ni hatari sababu atawaachia magaidi ambao wamekuwa wakiwamwagia watalii tindikali znz, kuchoma makanisa na kuwauwa mapadre.

Nimechoka sana!

Chanzo cha habari ni: Gazeti la Mwanahalisi ambalo limeanza kutolewa tena leo baada ya kufungiwa zaidi ya miaka 3.
Lakini unaweza pia kuchungulia huko The Hill ili uone wauza pembe za ndovu wanavyo mwogopa EL.

 
mfa maji haishi kutapa tapa! wameishiwa mbinu hao!!
 
Kinanaà simpendi!!!!!

Huyu mtu hamwogopi mungu kabisa roho yake itakuwa nyeusi kama lami. Kawahukumu akina Farid masikini ili tu chama chake kifanye kinavyotaka kwenye uchaguzi ujao.
 
Ilitupiwa hapa hiyo makala siku za nyuma naona kama haikuweza ku-hit. It was too low wengi wakaipuuza na bila shaka hata wazungu watakuwa wameipuuza pia.
 
ccm inabidi iondoke kwa nguvu ya umma na nguvu ya ziada
 
Wamechelea sanaaa.....sisi malofa wapumbavu na mbumbumbu tumeshafanya mabadiriko.
HATURUDI NYUMA KATIKA KUWAONDOA MADARAKANI MAJIZI HAYO
 
Kwahiyo huko The Hill wanapiga kura.. wamejaribu kumchongea kwa wanachi hapa wameshindwa... hahaa ccm bila wahisani ni sawa na bodaboda bila dereva
 
Kwahiyo huko The Hill wanapiga kura.. wamejaribu kumchongea kwa wanachi hapa wameshindwa... hahaa ccm bila wahisani ni sawa na bodaboda bila dereva

Bodaboda bila dereva ni pikipiki
 

Attachments

  • 1442838836531.jpg
    1442838836531.jpg
    13.9 KB · Views: 243
Du twaweza wametoa utwafitwa uliotwafitiwa haha
 
Wazungu wameshawajua CCM inside out.
Wanajua wao ndio chanzo cha umasikini uliokithiri.
 
Back
Top Bottom