CCM inafanya kampeni kizamani!

CCM inafanya kampeni kizamani!

Magufuli na Kikwete,tuseme CCM kwa kifupi kutumia ujenzi wa barabara kutafutia kura ni sehemu ya uelewa mdogo.
Wakati ni kweli kwamba barabara ni jambo la msingi sana lakini kura kwanza hazitolewagi kama pongezi au zawadi,pili hamna kundi katika jamii linalofaidika lenyewe tu binafsi na barabara.Hapa naomba nieleweke vizuri,wanafunzi pamoja kuwa wananufaika na barabara lakini wanajali zaidi gharama za elimu,ubora wa elimu na ajira.
Wafanyabiashara pamoja na kuwa wanafaidika na barabara wanajali zaidi kodi,upatikanaji wa mikopo na unafuu wa huduma za fedha.
Vivyo hivyo kwa makundi mengine.Barabara ni hoja ya ujumla sana,think tank ya kampeni ya CCM inapaswa kufikiri zaidi.
 
Maisha yanaenda yakibadilika kila siku,tekinoloji nayo inabadilika na hata uwezo wa watu wa kutazama mambo unabadilika.

Katika chaguzi zilizopita CCM haikuwa na kazi kubwa sana.Watu ambao hata bila kufanyiwa kampeni waliipigia kura CCM walikuwa wengi.Upinzani ulikuwa umegawanyika na haukuwa na wafuasi wengi sana.Ilikuwa rahisi sana kwa CCM kuhujumu,kudhulumu na kushinda hata kwa single moja tu ya kapteni Komba.

Jambo ambalo CCM hawajaweza kulimeng'enya ni kwanza kutambua athari ya muungano wa vyama vya upinzani na Pili athari ya Vigogo waliokuwa CCM waliohamia upinzani.

Mambo haya mawili yamebadili upepo katika uwanja wa kampeni na CCM ilipaswa kutambua hili.
Kwanza Muunganiko wa Upinzani umewafanya wafuasi wa upinzani kuwa kitu kimoja na kuzungumza lugha moja na hili limeongeza mara dufu wapiga kura wa mgombea wa upinzani wenye maamuzi tayari~decided voters.
Pili kuhamia upinzani kwa waliokuwa vigogo wa CCM kumeimega CCM kwa sehemu kubwa na waliomegeka ni wapiga kura wenye maamuzi tayari.

Ni kukosa kufikiri tu kutamfanya mgombea yoyote kati ya Lowasa na Magufuli wajinadi kwa wafuasi wachache ambao kimsingi ni wafia chama wa Act na TLP.

Kwenye kampeni za kisasa,vyama na wagombea huweka mikakati mingi juu ya wapigakura ambao hawajafanya maamuzi~undecided voters.

Swali linakuja,Wapiga kura ambao hawajafanya maamuzi ni wapi katika uchaguzi huu?
Jibu liko dhahiri; ni wanachama waliobakia CCM na wapiga kura wachache wasio na vyama.
Kampeni za toroka uje,vuka mto,ulipo tupo zinawalenga wapigakura waliobakia CCM.
Sera za elimu bure,riba kwa mkulima na nyingine zinawalenga wapigakura wasio na vyama zaidi!
Hii inaitwa "targeting in campaign".

CCM inauza sera za jumla jumla kwa watu wote.Unaweza kurusha jiwe kwenye kundi la ndege elfu usipate hata mmoja.

CCM haijui wafuasi wake kindakindaki wamebaki wangapi na wala imlenge nani,hii ni hatari kubwa.
Kampeni za tshirt,wali na kofia ni kampeni za kizamani.

Uchambuzi huu umetulia SANA...mtu kama @Simiuyetu hawezi soma hapa maana unachoma moyo....

CCM ni sikio la kiufa halisikii daawa
 
Kampeni za kisasa ndio hazina ilani, eti!

Ndugu yangu,fungua macho uangalie,kampeni za CCM zimeanza kama mtu anayeendesha gari usiku bila taa,huwaga hawezi ona hatari iliyo mbele kwa muda sahihi.
Kwanza tu,Magufuli anakosa sifa ya kiuongozi ya kushawishi mabadiliko,sasa hivi watu wana kiu ya kiongozi anayeweza kutingisha taasisi na magufuli hanukii wala harufu hiyo.
Alafu tuseme tu kweli,Kikwete aliboronga na hii inamfanya asiwe mtu sahihi wa kumnadi Magufuli kwenye majukwaa.Anabana wigo wa kura.Brother toroka uje,better late than never.
 
Since ile day walivotangaza ile team yao ya kampeni,nilishaona udhaifu mkubwa sana kwenye ile team,team mbovu ambayo haisemi sera kazi kumtajataja lowassa,sasa ndio wananchi wanachotaka kusikia,team mbovu ni mbovu tu
 
Ndugu yangu,fungua macho uangalie,kampeni za CCM zimeanza kama mtu anayeendesha gari usiku bila taa,huwaga hawezi ona hatari iliyo mbele kwa muda sahihi.
Kwanza tu,Magufuli anakosa sifa ya kiuongozi ya kushawishi mabadiliko,sasa hivi watu wana kiu ya kiongozi anayeweza kutingisha taasisi na magufuli hanukii wala harufu hiyo.
Alafu tuseme tu kweli,Kikwete aliboronga na hii inamfanya asiwe mtu sahihi wa kumnadi Magufuli kwenye majukwaa.Anabana wigo wa kura.Brother toroka uje,better late than never.
Mfanyabiashara kama mbowe na mwenzie lowassa wamesha fanya biashara nyingi sana tangu ujana wao haswa mbowe na mali zake za kurithi hao watu kili kitu kwao ni dili kama ww unapoletewa dili hata la vitu vya wizi na unalikurupikia tu ki mtaani mtaani! Katika dili za kiujanja ujanja mbowe kesha uza chama hiyo kwake ni top deal kachukua vyake sshv anasikilizia kuuza nchi na jiiizi la kimataifa! Kama huyo mwingine ana mali na biashara zake nzuri tu mbali na wizi bado angeendelea kuishi vzr ila sijui kwann watu wa aina hii hawaridhikagi! Na katika dili hili wakiliweza wao ni ma expert wa kimataifa!
 
Since ile day walivotangaza ile team yao ya kampeni,nilishaona udhaifu mkubwa sana kwenye ile team,team mbovu ambayo haisemi sera kazi kumtajataja lowassa,sasa ndio wananchi wanachotaka kusikia,team mbovu ni mbovu tu
 
Magufuli na Kikwete,tuseme CCM kwa kifupi kutumia ujenzi wa barabara kutafutia kura ni sehemu ya uelewa mdogo.
Wakati ni kweli kwamba barabara ni jambo la msingi sana lakini kura kwanza hazitolewagi kama pongezi au zawadi,pili hamna kundi katika jamii linalofaidika lenyewe tu binafsi na barabara.Hapa naomba nieleweke vizuri,wanafunzi pamoja kuwa wananufaika na barabara lakini wanajali zaidi gharama za elimu,ubora wa elimu na ajira.
Wafanyabiashara pamoja na kuwa wanafaidika na barabara wanajali zaidi kodi,upatikanaji wa mikopo na unafuu wa huduma za fedha.
Vivyo hivyo kwa makundi mengine.Barabara ni hoja ya ujumla sana,think tank ya kampeni ya CCM inapaswa kufikiri zaidi.

Kaka uchambuzi wako umemakinika! Nimesema vizuri.
 
Kuna vitu vya ajabu sana kutoka kwenye timu ya campaign ndani ya CCM na maandalizi yao ya awali; hawa jamaa wameingia kwenye huu uchaguzi wakiwa na advantage kubwa sana kutokana na ziara ya Kinana.

Ukiangalia vitu ambavyo umati unashangalia vikiongolewa ndio vilevile kinana alivyo itimisha watanzania wamegusia kwenye ziara zake, social justice ambapo wafanyakazi wa serikari wamekuwa wakilalamikiwa sana kiutendaji na unyasasaji, income distribution, na kupunguziwa mzigo wa ugumu wa maisha kwa kodi luluki wanazopewa wajasiriamali wadogo wadogo.

Sasa sielewi kwanini CCM aikutumia kipindi hiko walau kuonyesha kujali kama chama cha siasa kabla ya uchaguzi, leo hii kitu kile kile alichokuja nacho Kinana, Lowassa ndio anakitumia tena kwa dakika zisizo zidi tano na kupigiwa makofi. Swala la social justice litakuwa na uzito sana mijini maana huko ndio watu inabidi waishi kwa ujasiriamali sasa kama masokoni wananyanyaswa, kodi zimejaa, gharama za maisha kuongezeka hivi unatarajia watu bado waseme CCM oyee.

Jamaa walikuwa na muda sana wakujua uchaguzi huu unahusu nini kwa jamii, labda kwa sababu bado asilimia 70 yetu ni wakulima hiko ndio kitaisaidia CCM. Lakini siasa za kuwaambia watu sijui kuchagua upinzani nchi itavurugika huko ni kujiongopea watu wanataka mabadiliko na wasipoyapata CCM watayatafuta kwengine.

Aiwezekani shirika la nyumba lipandishe kodi kwa asilimia zaidi ya 250 hiyo hela mtu anatoa wapi, au bei ya chakula ipande kwa asilimia 200 hiyo nyongeza watu wanatoa wapi, people are tired. Na Kinana aliwaambia jamani watu wanasema hivi sasa sijui hii kampeni iliandaliwa vipi, kwa sasa kikubwa ni mazoea tu ya sehemu zingine ndio kitakachowapa watu ushindi ikifika hatua watu wanaweza mkubali ata mtu mgonjwa kama Lowassa ujue change is inevitable.

Bado naamini CCM itashinda lakini the message is clear watu wamechoka madharau na wanajua wakifanya makosa wanamiaka mitano mengine ya mateso kuna kila sababu ya kuweka vijana ndani ya CCM kuna watu wamekaa juu sana wamesahau chini kuna nini ata pale audit wanayofanya wenyewe inapowapa majibu bado kuyadharau.
 
Magufuli na Kikwete,tuseme CCM kwa kifupi kutumia ujenzi wa barabara kutafutia kura ni sehemu ya uelewa mdogo.
Wakati ni kweli kwamba barabara ni jambo la msingi sana lakini kura kwanza hazitolewagi kama pongezi au zawadi,pili hamna kundi katika jamii linalofaidika lenyewe tu binafsi na barabara.Hapa naomba nieleweke vizuri,wanafunzi pamoja kuwa wananufaika na barabara lakini wanajali zaidi gharama za elimu,ubora wa elimu na ajira.
Wafanyabiashara pamoja na kuwa wanafaidika na barabara wanajali zaidi kodi,upatikanaji wa mikopo na unafuu wa huduma za fedha.
Vivyo hivyo kwa makundi mengine.Barabara ni hoja ya ujumla sana,think tank ya kampeni ya CCM inapaswa kufikiri zaidi.
Kabisa walishaambiwa watafute namna ya kukutana na makundi mbali mbali na kuongea nao wao wanawaita mmoja ya wawakalishi wao katika kadamnasi za jumla aongelee faida za sera za CCM.
 
Mleta mada una akili sana. Umeandika vitu vya msingi sana, CCM wanafanya vitu kwa mazoea wakidhani watanzania watawachagua tu, kumbe hali sio shwari.

Tayari Magufuli amefanya kampeni katika mikoa 6(Dar, Katavi, Rukwa, Mbeya, Njombe na sasa yuko Songea) lakini Political atmosphere inamtisha sana Magufuli, hali ni tata sana.
Mood iliyopo kwa watu wanaohudhuria mikutano yake haitoi matumaini ya Ushindi kwa CCM hata kidogo, bahati mbaya Viongozi wa CCM hataki kukubali huu ukweli.

Nadhani Think tankers wa CCM na Magufuli ama ni wazee sana kisiasa(wamechoka), mambumbu wa siasa za kisasa au wamebweteka kama sio kukata tamaa.
 
Mleta mada una akili sana. Umeandika vitu vya msingi sana, CCM wanafanya vitu kwa mazoea wakidhani watanzania watawachagua tu, kumbe hali sio shwari.

Tayari Magufuli amefanya kampeni katika mikoa 6(Dar, Katavi, Rukwa, Mbeya, Njombe na sasa yuko Songea) lakini Political atmosphere inamtisha sana Magufuli, hali ni tata sana.
Mood iliyopo kwa watu wanaohudhuria mikutano yake haitoi matumaini ya Ushindi kwa CCM hata kidogo, bahati mbaya Viongozi wa CCM hataki kukubali huu ukweli.

Nadhani Think tankers wa CCM na Magufuli ama ni wazee sana kisiasa(wamechoka), mambumbu wa siasa za kisasa au wamebweteka kama sio kukata tamaa.

CCM imepanic mapema sana,na hii inaonyesha kuwa kadi yao ya ushindi waliyoweka chini ya kapeti ni goli la mkono!
Na hili ndilo linalonipa wasiwasi!!
Ukawa wamejipangaje kwa goli la mkono?
 
Back
Top Bottom