CCM ina cha kuogopa, siyo Membe au Lissu

CCM ina cha kuogopa, siyo Membe au Lissu

jellyFish

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2013
Posts
316
Reaction score
127
CCM haikosi usingizi kwa harakati za ACT na CHADEMA, ila nadhani itatikisika kwa hoja zao zaidi zinazolenga kuonesha na kutatua shida za wananchi. CCM ijiandae kupoteza kura kwa makundi yafuatayo km haitakua na majibu.

(1) Kundi la watumishi wa umma; kundi hili lina hasira ya kutoongezewa mishahara, kurefushiwa muda wa kupanda madaraja na majibu ya kejeli kuwa km unaona mshahara mdogo, acha kazi, kuonekana matajiri na watoto wao kutopata mikopo elimu ya juu, kuwaondoa watoto wao kwenye bima za afya wangali wapo vyuoni.

(2) Kundi la wanafunzi wa vyuo. Kundi hili linaumizwa kwa kukosa mikopo na hata wale waliopata mikopo wanatakiwa kulipa riba zaidi ya 80%. yaani ktk kila TZS 100 ulizokopa, utalipa TZS 180. bora ungekopa benki.

(3)Kundi la vijana, kundi hili lina hasira ya kutoweza kuajiriwa na kujiajiri. Ndio kundi hatari zaidi na lenye hasira kuu. Kundi hili halisikilizi execuses, halina uvumilivu. Huwezi kujitetea kuwa unanunua ndege kwanza, wenyewe wanataka kufanya kazi na kupata fedha.

HIVYO, makundi yote niliyoyataja ukiongeza na la wafanyabiashara wana uwezo ku influence wapiga kura wengine. unaweza kuona CCM inakosa usingizi maeneo gani.

CCM waombe wapinzani wasitembee na hizo hoja pia waombe Membe na Lissu wagombee ili wagawanyishe kura, vinginevyo, uchaguzi utakua mgumu mno kwa CCM kuliko ule wa 2015.

CCM ikiwa na majibu mujarrab kwa makundi hayo, itakua na uhakika wa ushindi.
 
1597737673466.png
 
CCM haikosi usingizi kwa harakati za ACT na CHADEMA, ila nadhani itatikisika kwa hoja zao zaidi zinazolenga kuonesha na kutatua shida za wananchi. CCM ijiandae kupoteza kura kwa makundi yafuatayo km haitakua na majibu..
Hongera kwa hoja Nzuri. Niongeze tubkndi la wastaafu ambao bado wanataabika. Mtu mfumo na Serikali wanajua mwezi ujao watumishi x wanastaafu, lakn monthly penseni na burungutu anafuatilia kwa MIKOPO zaidi ya miezi 6 HD miaka 2, had anadhoofu afya na akili. Majibu ya yaleyale subiri.

Pia wale watumishi wa fyeti fake nao sijui wanamambo gani huko waliko. Hapa Serikali Si tu ine na Majibu, Bali UTEKELEZAJI wake na kubadili hii hali ya kusumbuliwa.
 
Na sasa kuna wale watumishi waliothubutu kugombea nafasi za ubunge, limekuwa ni tatizo kubwa badala ya FURAHA ya kuthubutu kuitumikia nchi kwa nafasi nyingine.

Wamekosa mishahara, Nalo Serikali ije na UTEKELEZAJI Hasa kwa waliofuata taratibu za ruhusa kupokea mishahara yao ili familia nipate haki. Tujenge umoja badala ya kuongeza matengano
 
Ongezea kundi la wakulima.. kukosekana kwa soko la mazao. (Korosho)
 
Back
Top Bottom