boyayoparuparu
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 343
- 82
Kila mtu anaenunua umeme, amelazimishwa kuchangia asilimia tatu kuigharamia EWURA na asilimia moja kuigharamia REA, inakuwaje mteja bila ridhaa yake achangie kuendesha makampuni yanayoanzishwa na serikali??!! Tunaendelea kufanywa wajinga huku wengine wakiendelea kuunga mkono bila kutafakari mzigo ambao CCM inawatwisha wananchi, bila tafakari na pengine kwa uwezo mdogo wa kutafakari mambo au kwa kujali maslahi binafsi wasanii wanaiunga mkono CCM, pesa hizi pengine ndizo wanazopewa CCM ili kufanikisha kampeni yao inayotumia pesa nyingi sana, tunanyonywa sana, hata mteja akiomba kuunganishiwa umeme anaambiwa anunue nguzo na vifaa vingine,ambavyo baadae tanesco wanavitumia hivyo hivyo kuongezea wateja na mapato bila aibu, namuomba MUNGU aifute kabisa CCM, angalia toka kampeni imeanza tumepandishiwa gharama za simu, hata chocolate ya Bakhresa imepanda, anaeunga mkono CCM atafakari kwanza.