CCM imekufa mikononi mwa wanaCCM

CCM imekufa mikononi mwa wanaCCM

Mssassou

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
1,537
Reaction score
597
Hapa ilipo CCM inapumulia mashine yaani iko ICU lakini 25.Oktoba.2015 itakufa.Dalili za kifo ziko nyingi lkn Mimi nitataja mambo yaliyosababisha CCM kufa.

1. Rushwa na ufisadi uliokithiri .

2. Maisha kuwa magumu kwa watanzania kila kukicha.

3. Kukata baadhi ya majina wanaopendwa na watanzania kugombea nafasi ya urais mfano Edward Lowassa na Prof Mwandosya.

4. Baadhi ya vigogo na wanachama mchana kuwa CCM usiku kuwa chama kingine.

5. Kushindwa kufanya na kupata mabadiliko ndani ya CCM.
 
CCM Mbona Wakipata 30% ya Kura Ni ndoto za Mchana.

CCM walishashindwa mapema tu,Kilichobaki wanapromote wasanii tu.
 
Kife Tu maana hakuna namna nyingine. Magufuli mwenyewe kawa mgombea binafsi Ata ahadi anazozitoa Ni zake toka kichwa na nyingine Ni copy n paste kutoka ukawa wala sio ilani ya ccm tusitegemee kuna jipya au cha kutekelezeka kwenye hyo ilani ya ccm. Huu Ni wakati watanzania tufanye mamuzi ya busara na sahihi twende na lowassa kwa mabadiliko ya kweli na uhakika.
 
Hapana tusiiombee kifo Bali ije upya na kuwa thabiti ili kuunda upinzani making bunge lijalo. Baada ya kushindwa uchaguzi huu lazima watajitathimini na kuondoa " mizoga" ( nimetumia neno hilo makusudi) kama Nape na kuwa chama imara kinachoweza kuichachafya serikali ya Ukawa pale itakapo jisahau na kwenda hovyo.
 
Back
Top Bottom