Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,529
- 41,045
Ni jambo linalofikirisha sana, na kushangaza, na kuzua maswali mengi.
CCM inayafanya haya kwa nia ya kumdanganya nani? Au wanafanya kwaajili ya kumfariji nani?
1) CCM, kwa sababu zisizofahamika, imeamua kuacha kufanya kampeni za uchaguzi, na kugeuza mikutano iliyostahili kuwa ya kampeni, kuwa matamasha ya muziki
2) CCM, sijui ni kwa kujitoa ufahamu au dhamira ya kuamsha ghadhabu ya wapiga kura, kwenye matamasha hayo, mara kadhaa wametoa vitisho kwa wapiga kura kuwa wasipowachagua wagombea wa CCM, baada ya uchaguzi, watajuta. Hayo yalitamkwa na mgombea wa Urais kwenye tamasha la muziki lililofanyika wilayani Magu. Kila mwenye akili alibaki midomo wazi.
3) Kule Geita, kwenye matamasha hayo ya muziki, mgombea wa Urais wa CCM, aliwaambia wapiga kura kuwa wamchague yeye kwa sababu ni msukuma mwenzao. Je, ina maana tuiso wasukuma hatustahili kumchagua?.
4) Pale Mwanza, siku hiyo ya tamasha la CCM, shule zote, wakuu wa shule walielekezwa na Mkuu wa mkoa, kuwa siku hiyo kusiwe na masomo. Wanafunzi wote wapelekwe viwanja vya Furahisha kwenda kumsikiliza mgombea wa Urais wa CCM. Pia waliambiwa wasivae sare za shule. Pia walimu na watumishi wengine, wahakikishe wanahudhuria
5) Pale Mwanza, mgombea wa Urais kupitia CCM aliongea kidogo sana. Kisha akasema, sitaki niongee sana kwa sababu najua mmekuja kucheza muziki! Kwa hiyo hata yeye anajua wale watu waliokuwepo hawakuja kumsikiliza yeye bali walikuja kuangalia mauno ya wasanii.
Watanzania mwaka huu ni wa hasara. Watu wanaenda kwenye mikutano ya CCM ili wakasikie sera za CCM zenye kutoa matumaini katika kuwapa unafuu wa maisha kupitia ajira, ukuuaji wa uwekezaji, ongezeko la mapato yao, uhakika wa elimu na tiba bora, sera za makazi mazuri, kuondokana na watu wasiojulikana ambao kazi yao ni kuua, kuteka, kuwapoteza watu, na kupiga risasi watu wanaomkosoa Rais na Serikali; cha ajabu wanaoneshwa viuno vya wasanii!!!
Cha kujiuliza, wanafanya haya yote kwa lengo gani? Je, bila ya wanafunzi, bila ya kuigeuza mikutano ya kampeni kuwa matamasha ya muziki, wanaamini hakuna atakayekwenda kumsikiliza mgombea? Kama watu hawana hamu ya kwenda kumsikikiza mgombea, na kwenye kampeni wanafuata muziki, watakuwa na hamu ya kwenda kumpigia kura? Au siku ya uchaguzi wasanii watasambazwa vituo vyote vya kupigia kura kwa nia ya kuwavuta wapiga kura ambao kila wanapoenda hamu yao ni kuona viuno vya wasanii?
CCM, chagueni hata eneo moja tu ambalo mnaamini CCM inaungwa sana mkono, mfanye mkutano wa kampeni japo mmoja ili watu wasikie sera badala ya kuonesgwa wasanii. Msipeleke wasanii wala msilazimishe watu kuhudhuria bali mkiweza muwashawishi. Hiyo itawapa kipimo kizuri cha uungwaji mkono, na mtagundua kasoro zenu kuliko kujifunika kichwa ili tu msione msiyotaka kuyaona.
CCM inayafanya haya kwa nia ya kumdanganya nani? Au wanafanya kwaajili ya kumfariji nani?
1) CCM, kwa sababu zisizofahamika, imeamua kuacha kufanya kampeni za uchaguzi, na kugeuza mikutano iliyostahili kuwa ya kampeni, kuwa matamasha ya muziki
2) CCM, sijui ni kwa kujitoa ufahamu au dhamira ya kuamsha ghadhabu ya wapiga kura, kwenye matamasha hayo, mara kadhaa wametoa vitisho kwa wapiga kura kuwa wasipowachagua wagombea wa CCM, baada ya uchaguzi, watajuta. Hayo yalitamkwa na mgombea wa Urais kwenye tamasha la muziki lililofanyika wilayani Magu. Kila mwenye akili alibaki midomo wazi.
3) Kule Geita, kwenye matamasha hayo ya muziki, mgombea wa Urais wa CCM, aliwaambia wapiga kura kuwa wamchague yeye kwa sababu ni msukuma mwenzao. Je, ina maana tuiso wasukuma hatustahili kumchagua?.
4) Pale Mwanza, siku hiyo ya tamasha la CCM, shule zote, wakuu wa shule walielekezwa na Mkuu wa mkoa, kuwa siku hiyo kusiwe na masomo. Wanafunzi wote wapelekwe viwanja vya Furahisha kwenda kumsikiliza mgombea wa Urais wa CCM. Pia waliambiwa wasivae sare za shule. Pia walimu na watumishi wengine, wahakikishe wanahudhuria
5) Pale Mwanza, mgombea wa Urais kupitia CCM aliongea kidogo sana. Kisha akasema, sitaki niongee sana kwa sababu najua mmekuja kucheza muziki! Kwa hiyo hata yeye anajua wale watu waliokuwepo hawakuja kumsikiliza yeye bali walikuja kuangalia mauno ya wasanii.
Watanzania mwaka huu ni wa hasara. Watu wanaenda kwenye mikutano ya CCM ili wakasikie sera za CCM zenye kutoa matumaini katika kuwapa unafuu wa maisha kupitia ajira, ukuuaji wa uwekezaji, ongezeko la mapato yao, uhakika wa elimu na tiba bora, sera za makazi mazuri, kuondokana na watu wasiojulikana ambao kazi yao ni kuua, kuteka, kuwapoteza watu, na kupiga risasi watu wanaomkosoa Rais na Serikali; cha ajabu wanaoneshwa viuno vya wasanii!!!
Cha kujiuliza, wanafanya haya yote kwa lengo gani? Je, bila ya wanafunzi, bila ya kuigeuza mikutano ya kampeni kuwa matamasha ya muziki, wanaamini hakuna atakayekwenda kumsikiliza mgombea? Kama watu hawana hamu ya kwenda kumsikikiza mgombea, na kwenye kampeni wanafuata muziki, watakuwa na hamu ya kwenda kumpigia kura? Au siku ya uchaguzi wasanii watasambazwa vituo vyote vya kupigia kura kwa nia ya kuwavuta wapiga kura ambao kila wanapoenda hamu yao ni kuona viuno vya wasanii?
CCM, chagueni hata eneo moja tu ambalo mnaamini CCM inaungwa sana mkono, mfanye mkutano wa kampeni japo mmoja ili watu wasikie sera badala ya kuonesgwa wasanii. Msipeleke wasanii wala msilazimishe watu kuhudhuria bali mkiweza muwashawishi. Hiyo itawapa kipimo kizuri cha uungwaji mkono, na mtagundua kasoro zenu kuliko kujifunika kichwa ili tu msione msiyotaka kuyaona.