CCM ijisahihishe sasa

CCM ijisahihishe sasa

Nicolas J Clinton Gabone

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2014
Posts
892
Reaction score
536
CHAMA CHA MAPINDUZI KIJISAHIHISHE

Comrades, tunakabiliwa na sura mpya na yenye mvutano mkubwa katika siasa za Tanzania. Muda mrefu migogoro ya kisiasa ilikuwa kati ya CCM na vyama vya upinzani. Lakini kwa sasa, hali imebadilika, mvutano mkubwa ni kati ya CCM na wananchi wenyewe. Jambo hili linaashiria mwanzo wa mabadiliko makubwa ya kifikra na kisiasa katika Taifa letu.

Maoni ya wananchi kwa viongozi wa serikali, ikiwemo mifano ya matamshi ya wazi yaliyojitokeza mbele ya Antony Mtaka, yanaonesha kuwa tatizo halionekani tena kuwa sehemu nyingine, bali ni CCM yenyewe. Chama kilichojikita kwenye misingi ya ukombozi kimekuwa sasa chanzo cha mgawanyiko, kutokana na maamuzi na vitendo vinavyolinda maslahi ya wachache ndani ya mfumo, huku wengi wakiachwa bila kusikilizwa.

Kutokana na kupungua kwa uhalali wa kisiasa kwa CCM mbele ya wananchi, inaonekana chama kinachagua kulinda nafasi yake kwa kushinikiza vyombo vya sheria na demokrasia, kukandamiza wakosoaji wa serikali na kudhoofisha uwezo wa vyama vya upinzani. Ni wazi kwamba mfumo unaotegemea ufisadi wa kisheria na matumizi ya nguvu, badala ya uhalali wa kijamii, hauwezi kuhimili shinikizo la muda mrefu.

Kufungwa kwa viongozi wa juu wa CHADEMA kwa tuhuma nzito za ugaidi na uaini, huku chama kikizuiwa rasilimali na uhuru wa kisiasa, ni ishara ya utekelezaji wa mkakati mpana, kuweka mazingira magumu ambayo upinzani unakuwa dhaifu kabla ya uchaguzi wa baadae. Hii ni dalili ya Taifa linaloingia kwenye siasa za hofu na udikteta badala ya siasa za ushindani wa hoja.

Kadiri CCM inavyozidi kuminya wananchi nafasi ya kueleza maoni yao, ndivyo chama kinavyojizidishia ugumu wa kuendelea kuaminika. Endapo mwenendo huu hautarekebishwa na/au kama mapinduzi ya haraka ya uchumi na maendeleo ya watu havitaonekana kwa macho ndani ya muda mfupi, msingi wa uhalali wa chama utazidi kuyumba, mfumo wa vyama vingi utadhoofika na mpishano na mgawanyiko wa kijamii utaongezeka kwa kasi. Katika kipindi cha miaka 5–10 ijayo, hofu ya CCM kupoteza madaraka inaweza kuwa kubwa kuliko uwezo wa chama kujirekebisha na kujisahihisha.

Historia ya kisiasa duniani inatuthibitishia jambo moja muhimu, nguvu inaweza kuchelewesha mabadiliko, lakini haiwezi kuyazuia milele. Wananchi wanapotambua na kukataa dhuluma, mabadiliko ya kisiasa yanakuwa lazima ya kutokea na mara nyingi yanatokea kwa kasi ambayo watawala hawakuwa wameitarajia au kujiandaa.

CCM IJISAHIHISHE KAMA HAIJACHELEWA
 
Kwa sasa wamekata kabisa kale ka "imani kidogo" kalikokuwa kamebakia kwao.

Hata wale wafia chama wanaona kabisa mambo hayako sawa!
 
kiburi na ubinafsi wa viongozi wa CCM umelifikisha taifa hapa tulipofika leo laana ya mwenyezi Mungu iwe juu yao na vizazi vyao
 
Ni kwasababu CCM bado inafanya siasa kama wako mwaka 1990.

Inaonekana hawana strategies tena, wanajaribu kupambana na nyakati lakini nyakati inawakataa.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI KIJISAHIHISHE

Comrades, tunakabiliwa na sura mpya na yenye mvutano mkubwa katika siasa za Tanzania. Muda mrefu migogoro ya kisiasa ilikuwa kati ya CCM na vyama vya upinzani. Lakini kwa sasa, hali imebadilika, mvutano mkubwa ni kati ya CCM na wananchi wenyewe. Jambo hili linaashiria mwanzo wa mabadiliko makubwa ya kifikra na kisiasa katika Taifa letu.

Maoni ya wananchi kwa viongozi wa serikali, ikiwemo mifano ya matamshi ya wazi yaliyojitokeza mbele ya Antony Mtaka, yanaonesha kuwa tatizo halionekani tena kuwa sehemu nyingine, bali ni CCM yenyewe. Chama kilichojikita kwenye misingi ya ukombozi kimekuwa sasa chanzo cha mgawanyiko, kutokana na maamuzi na vitendo vinavyolinda maslahi ya wachache ndani ya mfumo, huku wengi wakiachwa bila kusikilizwa.

Kutokana na kupungua kwa uhalali wa kisiasa kwa CCM mbele ya wananchi, inaonekana chama kinachagua kulinda nafasi yake kwa kushinikiza vyombo vya sheria na demokrasia, kukandamiza wakosoaji wa serikali na kudhoofisha uwezo wa vyama vya upinzani. Ni wazi kwamba mfumo unaotegemea ufisadi wa kisheria na matumizi ya nguvu, badala ya uhalali wa kijamii, hauwezi kuhimili shinikizo la muda mrefu.

Kufungwa kwa viongozi wa juu wa CHADEMA kwa tuhuma nzito za ugaidi na uaini, huku chama kikizuiwa rasilimali na uhuru wa kisiasa, ni ishara ya utekelezaji wa mkakati mpana, kuweka mazingira magumu ambayo upinzani unakuwa dhaifu kabla ya uchaguzi wa baadae. Hii ni dalili ya Taifa linaloingia kwenye siasa za hofu na udikteta badala ya siasa za ushindani wa hoja.

Kadiri CCM inavyozidi kuminya wananchi nafasi ya kueleza maoni yao, ndivyo chama kinavyojizidishia ugumu wa kuendelea kuaminika. Endapo mwenendo huu hautarekebishwa na/au kama mapinduzi ya haraka ya uchumi na maendeleo ya watu havitaonekana kwa macho ndani ya muda mfupi, msingi wa uhalali wa chama utazidi kuyumba, mfumo wa vyama vingi utadhoofika na mpishano na mgawanyiko wa kijamii utaongezeka kwa kasi. Katika kipindi cha miaka 5–10 ijayo, hofu ya CCM kupoteza madaraka inaweza kuwa kubwa kuliko uwezo wa chama kujirekebisha na kujisahihisha.

Historia ya kisiasa duniani inatuthibitishia jambo moja muhimu, nguvu inaweza kuchelewesha mabadiliko, lakini haiwezi kuyazuia milele. Wananchi wanapotambua na kukataa dhuluma, mabadiliko ya kisiasa yanakuwa lazima ya kutokea na mara nyingi yanatokea kwa kasi ambayo watawala hawakuwa wameitarajia au kujiandaa.

CCM IJISAHIHISHE KAMA HAIJACHELEWA
CCM lazima ibaki kama chauma
 
Ni kwasababu CCM bado inafanya siasa kama wako mwaka 1990.

Inaonekana hawana strategies tena, wanajaribu kupambana na nyakati lakini nyakati inawakataa.
hawasikilizi walijua watz wajinga tumewatekenya... CCM hawajawahi kuona Rais anauliwa na bunduki mbele za watu wakajisahau
 
Chanzo kikubwa kabisa ni ubinyaji wa demokrasia na utekaji wa wazi wazi huku ukibebwa kama ngao ya kukijikinga dhidi ya hasira za wananchi
 
Ccm hata ijirekebishe kwa sasa haiwezi kukubalika tena kwani hiki si kizazi cha ccm. Kwa ujumla ni chama kinachopishana na nyakati.
 
Ni chama mfu!
Hakikubaliki,kimeiba uchaguz na zaid ya yote wameua watu zaidi ya 800!

Shit hole!
 
Back
Top Bottom