"Ccm haitakubali ikishindwa"

"Ccm haitakubali ikishindwa"

juvenile davis

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2015
Posts
4,752
Reaction score
4,475
Leo nikiwa nimetulia,anakuja jamaa mmoja ambae tunafahamiana,,sijajua itikadi yake(yaani sijui chama chake),,ila maongezi yake mara nyingi ni kama yupo mwanaccm,,leo ananiuliza namna hii
JAMAA:ndugu yangu Lowasa atashindaaa?
MIMI:tukimpigia kura kwa wingi atashinda,kwa nini asishinde tukimchagua??
JAMAA:aaahh,ccm hawatakubali,(nikawa kimya)
JAMAA:ccm hawatakubali kuachia madaraka(kwa mara ya pili kaongea kauri hiyo).
Sasa nikashindwa kumuelewa kwa kweli,ikabidi nishindwe cha kumjibu zaidi nikampuuzia tu,maana sielewi aliniuliza akitaka nimpe majibu gani??
 
hiyo inajulikana kuwa hawatakubali kirahisi.

Nguvu ya umma usiifanyie mzaha kabisa
 
Leo nikiwa nimetulia,anakuja jamaa mmoja ambae tunafahamiana,,sijajua itikadi yake(yaani sijui chama chake),,ila maongezi yake mara nyingi ni kama yupo mwanaccm,,leo ananiuliza namna hii
JAMAA:ndugu yangu Lowasa atashindaaa?
MIMI:tukimpigia kura kwa wingi atashinda,kwa nini asishinde tukimchagua??
JAMAA:aaahh,ccm hawatakubali,(nikawa kimya)
JAMAA:ccm hawatakubali kuachia madaraka(kwa mara ya pili kaongea kauri hiyo).
Sasa nikashindwa kumuelewa kwa kweli,ikabidi nishindwe cha kumjibu zaidi nikampuuzia tu,maana sielewi aliniuliza akitaka nimpe majibu gani??
wataachia tu kama wanajipenda ,tume ya uchaguzi itende haki tu
 
Si unamsikia mgombewa wao anasema mkifanya mabadilko nchi itakuwa kama libya....inamaana wameshapanga wakishindwa wanakinukisha....Mabadiliko kwa watanzania ni mpango wa Mungu....Mjini watu wanakuambia hata wangesema Lowasa ni Msomali....Tungempigia yeye ccm waondoke kwanza..alf ndo tungeenza kujadili huo usomali...kwa hiyo awe fisadi asiwe fisadi kura na Mamvi..
 
Hilo hata mim nimeliwaza, wakishindwa wanaweza leta machafuko, maana wanawaza hii nchi niyaccm
 
Wataachia,hata wajeda wanalijua hilo.
 
Nan afe kwaajili ya mamvii..wana mabdiliko tutawaenzi kwa kuwawekea sikukuu ila zaidi ya hapo.aje lowassa aje magufuli maisha hayabdiliki kichwa chako Ndo nyenzo ya kujibadilisha
 
Nan afe kwaajili ya mamvii..wana mabdiliko tutawaenzi kwa kuwawekea sikukuu ila zaidi ya hapo.aje lowassa aje magufuli maisha hayabdiliki kichwa chako Ndo nyenzo ya kujibadilisha

Ignorance and stupidity at its best level.
 
Leo nikiwa nimetulia,anakuja jamaa mmoja ambae tunafahamiana,,sijajua itikadi yake(yaani sijui chama chake),,ila maongezi yake mara nyingi ni kama yupo mwanaccm,,leo ananiuliza namna hii
JAMAA:ndugu yangu Lowasa atashindaaa?
MIMI:tukimpigia kura kwa wingi atashinda,kwa nini asishinde tukimchagua??
JAMAA:aaahh,ccm hawatakubali,(nikawa kimya)
JAMAA:ccm hawatakubali kuachia madaraka(kwa mara ya pili kaongea kauri hiyo).
Sasa nikashindwa kumuelewa kwa kweli,ikabidi nishindwe cha kumjibu zaidi nikampuuzia tu,maana sielewi aliniuliza akitaka nimpe majibu gani??

Kwa mtazamo yakinifu hii habari yako naona haijakamilika au umetoa maamuzi ya moja kwa moja kwa upande mmoja. Kama wewe ni Great Thinker ilifaa kumuhoji kwa maswali ambayo yeye binafsi anaamini kwa nini hawa jamaa zetu CCM hawataachia madaraka. Vinginevyo hii inakuwa stori tu kama za vijiweni zisizo na mashiko wala hoja. Yatupasa kujifunza kukabiliana na adui na namna gani ya kumtoa kwa kupata maelezo yakinifu kutoka kwao. Siasa sio uadui bali ni tofauti za sera
 
wataachia tu kama wanajipenda ,tume ya uchaguzi itende haki tu

Pamoja na kufikiria kuwa CCM hawatakubali kushindwa tufikirie pia uwezekano wa UKAWA kukubali kushindwa. Tume inaweza kufanya kazi yake vizuri kabisa, baada ya kutoa matokeo upande ulioshindwa unaweza kukataa matokeo. Upo ushahidi kuwa mwaka 1995 Dr. AL Mrema alidai kuwa Dr. BW Mkapa alishinda kwa kuiba kura, Mwaka 2005 Prof. IH Lipumba alidai kuibiwa kura zake na Dr. JM Kikwete na mwaka 2010 Dr. WP Slaa alidai kuwa kura zilichakachuliwa na kumpa ushindi Dr. JM Kikwete.

Kwa hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa, kura za CCM na UKAWA hazitatofautiana kwa zaidi ya 5%, upande wowote utakaoshindwa utaona mashaka. Lowassa na Magufuli wanayo nafasi kubwa sana ya kuondoa mashaka miongoni mwa wafuasi wao; hebu fikiria endapo UKAWA watashinda na Dr. JP Magufuli akawa mtu wa kwanza kumpongeza Mr. EN Lowassa; ni mfuasi gani wa CCM ataanzisha vurugu? Kwa upande wa pili hebu fikiria CCM wakishinda na Mr. EN Lowassa akawa mtu wa kwanza kumpongeza Dr. JP Magufuli ni mfuasi gani wa UKAWA ataanzisha vurugu?

Namsihi Magufuli na ninamsihi Lowassa watunze amani ya nchi hii kwa kukubali matokeo.

Mungu ibariki Tanzania, amina.
 
Wewe ndio utakuwa hujamuelewa mwenzako, kwani kwa bahati mbaya sana ukishakuwa Mwanaukawa unapoteza uwezo wa kutofautisha hasi na chanya.

Alichomaanisha mwenzako huyo ni kuwa Wana ccm hawatokubali kubaki nyumbani siku ya uchaguzi na kuacha nchi kuangukia kwenye mikono isiyo salama.

Na hii ni kwa manufaa yenu pia...hebu tafakari mmeachana na mzazi mwenzako, yeye ni mtumiaji dawa za kulevya, alafu anapambana yeye ndiye aishi na mwanenu mwenye miaka mitatu tu...ungemuachia mwanao ? na nani atakushangaa iwapo itatokea unapita njiani unaongea mwenyewe kwa kurudia rudia "hakyamungu sikubali"
 
Nawaomba CCM wafikirie uwezekano ma vitu viwili; kushinda au kushindwa. na wajiandae kati ya hayo mawili.
Muda mrefu ccm wamekuwa na imani kuwa kushinda ni lazima na kwamba kutokushinda kwao ni janga kwa taifa. Upinzani wameshindwa mara nyingi. Wote wanaohusika na uchaguzi wawe makini na wasimamie haki wazi wazi. hakutakuwa na fujo
 
Nan afe kwaajili ya mamvii..wana mabdiliko tutawaenzi kwa kuwawekea sikukuu ila zaidi ya hapo.aje lowassa aje magufuli maisha hayabdiliki kichwa chako Ndo nyenzo ya kujibadilisha

Wewe ndo una akili mgando..hv kweli kina Nyerere ; samora; mandela na wengineo wasingekomaa..na kuzitesekea nchi zao ingekuwaje kama wangekuwa na akili kama zako?..hizo ni akili za mtu anayependa kutafuniwa..akili za kivivu..by the way what is life without freedom. .and sharing the fruits of that freedom together as a national! Unaogopa kufa?..kwa hali ilivyo hasa kwa vijana. .imefikia kipindi uvumilivu utatushinda..ndo maana ni lazima tufanye mabadiliko!..mh EL tupo nyuma yako no matter what..tutakuwa pamoja to the end!
 
Leo mmmoja wao anasema...
Mkimchagua Magufuli nitalala usingizi mzuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom