"With friends like these who needs enemies?. CCM wanajimaliza wenyewe na adui yao mkubwa ni wao wenyewe wala sio upinzani.
Guninita amefanya nini la maana kwenye hili jiji la Dar? Mafuriko yametokea Dar, Magufuli bila kujali ni x'mas alikuwa barabarani akisimamia ukarabati wa madaraja, Guninita na wenzake walikuwa wapi? Kwa nini Guninita hakumtaka Waziri wa Ulinzi awaombe radhi wakazi wa Dar kutokana na milipuko ya mabomu licha za waziri ahadi kwamba hayatarudia? Watu wamepoteza maisha, kwanini Guninita hakujitokeza kwenye vyombo vya habari na kudai msahama wa waziri wa ulinzi?
Nahiisi wabunge wa Dar wamoena ngoma nzito wakaamua kujificha kwenye hii ngozi ya 'ccm-mkoa wa Dar' ili wamkomoe Magufuli. Juzi Magufuli amesema anataka kivuko kijitegemee lakini pia anataka kutumia kiasi cha fedha kitakachopatikana ili kujenga vifuko vingine ili kupunguza tatizo la usafiri Dar. Sasa Guninita analeta porojo gani hapa? Hili tatizo limekuzwa na hawa hawa wabunge wa ccm -Dar. Na ni aibu kubwa kuona hawa mufilisi wakiendeleza ngonjera kwenye vyombo vya habari kwa mambo yaliyo wazi kabisa. Mbali na Magufuli ccm wana waziri gani mwingine mchapa kazi? Wassira? Kawambwa? Ngeleja?
Magufuli usirudi nyuma wafanye wanalotaka lakini usirudi nyuma kabisa kabisa. Na kwa Guninita na wenzake, wahanga wa mafuriko bado hawana mahali pa kukaa, huko wanakopelekwa hakuna chochote ni viwanja vitupu sijui watalala wapi hadi watakapojenga nyumba! Je, mnaoliona hilo au kila kukicha mnawaza namna ya kushambuliana?
Mmeshindwa kusimamia maamuzi yenu ya siku tisini sasa mnataka pa kutokea!