CCM bado ni chama cha kijamaa?

CCM bado ni chama cha kijamaa?

huwezi kukuta mambo ya hovyo kama hayo ndani ya familia ya kijamaa ya CCM, ndio maana inafahamika kwamba CCM ni ya waTanzania wote.
Tabaka tawala ndani ya CCM hupenda watu hoyahoya kama wewe, yaani watu wasiojua kuwa chama cha siasa hujengwa juu msingi wa Falsafa, Itikadi na sera na siyo kupuyanga kipropaganda!

Ubaguzi wa CCM upo kati ya Koo zinazomiliki CCM na wana CCM wakuja. Na ndiyo maana wenye chama chao husema kuwa CCM ina wenyewe.
 
ndio maana baadhi ya waropokaji wanaofadhiliwa na mabwenyenye ya magharibi hivi sasa wanasota korokoroni kwasababu walipoteza uelekeo right?🐒
Kuropokwa na kuropoka kupo Kwa yule aliyesema CHADEMA inakusanya hela ili inunue virusi vya Mpox na Ebola!
 
Tabaka tawala ndani ya CCM hupenda watu hoyahoya kama wewe, yaani watu wasiojua kuwa chama cha siasa hujengwa juu msingi wa Falsafa, Itikadi na sera na siyo kupuyanga kipropaganda!

Ubaguzi wa CCM upo kati ya Koo zinazomiliki CCM na wana CCM wakuja. Na ndiyo maana wenye chama chao husema kuwa CCM ina wenyewe.
CCM ni familia ya matabaka yote bila ubaguzi. Ndio maana hata kwenye Harambee ya juzi, hata shilingi 50 ilipokelewa kwa unyenyekevu mkubwa na kwa heshima ya kiwango cha juu sana.

Na huo ndio ujamaa wa kisasa na sio kuropoka ropoka tu kama vyama vingine vilivyo poteza uelekeo kwa kuendekeza ubaguzi na upendeleo 🐒
 
Kuropokwa na kuropoka kupo Kwa yule aliyesema CHADEMA inakusanya hela ili inunue virusi vya Mpox na Ebola!
Chadema ilishajifia kibudu kitambo tu gentleman, huenda kuna chadema masalia kwa sasa.

ubinafsi na ubaguzi wa viongoz wake uliisambaratisha chadema 🐒
 
Marajiri ndio waajiri na walipa kodi wakubwa

Mtu kukataa michango yao anakuwa kichwani hazimo

Kuwa tajiri sio kosa
Unadhani tajiri atakupa tu bilioni kadhaa bure bila kujua jinsi ya kuzirudisha?!
Hakuna pesa ya bure duniani humu!
 
Ujamaa "wa kisasa" unaweka kodi kubwa, hasa kwa matajiri na kutoa huduma nyingi kwa wananchi free au kwa bei ndogo. CCM inaelekea au inatoka huko kadri siku zinavyoenda?
 
Yes,
ni chama cha kijamaa tena ni ule ujamaa wa kisasa kabisa, wenye umoja zaidi, udungu zaidi, uwazi zaidi, usawa zaidi na usie thubutu kumuacha binadamu hata moja nje ya familia hii pana na madhubuti sana ya CCM kijamii, kisiasa na hata kiuchumi.

Kazi na utu, tusonge mbele pamoja bila chuki bali umoja na mshikamano wa kitaifa na kimataifa.
Hiyo ndio CCM gentleman chini ya Dr.Samia Suluhu Hassan 🐒
Hata Singasinga na Magabacholi wengine nao ni Wakulima?
 
Niliangalia ile harambee yao na jinsi wanavyoendesha chama chao, nikajiuliza kama CCM bado kina sifa ya kuendelea kuitwa chama Cha kijamaa...

CCM bado ni chama cha wakulima na wafanyakazi ama ndiyo kimeshakuwa chama cha MABEPARI na wafanyabiashra?

Ubeberu umetamalaki CCM😄😆😀
Kwanini uangalie CCM wewe MChadema ? hagaikeni na lichama lenu mfu achana na chama dume chama dola.
 
Kwanini uangalie CCM wewe MChadema ? hagaikeni na lichama lenu mfu achana na chama dume chama dola.
Kwa ivo umekaa ukawaza cha kuandika ndiyo ukaishia kuandika hiki ulichoandika?
 
Ujamaa "wa kisasa" unaweka kodi kubwa, hasa kwa matajiri na kutoa huduma nyingi kwa wananchi free au kwa bei ndogo. CCM inaelekea au inatoka huko kadri siku zinavyoenda?
Siyo kweli... Ujamaa na mabepari hawakai chungu kimoja. Kwani siasa ya ujamaa nini?
 
Wakomunisti na mabepari ndiyo hawakai pamoja. Bahati mbaya kwa kiswahili Socialims na communism vyote ni ujamaa.
Democrats ni watu wafuata siasa za kijamaa (Leftists) jee wanakaa pamoja na mabepari wa Republican?

Hizi siasa zina misingi tofauti kabisa isiyochangamana. Ukomunist ni aina ya mfumo wa kuendesha ujamaa na wenyewe ni mfumo unatokana na watu wanaofuata misingi ya kuendesha ujamaa iliyowekwa na V.I Lenin.

Sasa chama chenye mchanganyiko wa mabepari na wajamaa ndiyo itikadi yake utaiitaje?
 
Democrats ni watu wafuata siasa za kijamaa (Leftists) jee wanakaa pamoja na mabepari wa Republican?

Hizi siasa zina misingi tofauti kabisa isiyochangamana. Ukomunist ni aina ya mfumo wa kuendesha ujamaa na wenyewe ni mfumo unatokana na watu wanaofuata misingi ya kuendesha ujamaa iliyowekwa na V.I Lenin.

Sasa chama chenye mchanganyiko wa mabepari na wajamaa ndiyo itikadi yake utaiitaje?
Social democrats ni mchanganyiko wa ujamaa na ubepari.
 
Niliangalia ile harambee yao na jinsi wanavyoendesha chama chao, nikajiuliza kama CCM bado kina sifa ya kuendelea kuitwa chama Cha kijamaa...

CCM bado ni chama cha wakulima na wafanyakazi ama ndiyo kimeshakuwa chama cha MABEPARI na wafanyabiashra?

Ubeberu umetamalaki CCM😄😆😀
Wewe mara ya maisha kusikia CCM ni chama cha kijamaa lini?
 
Back
Top Bottom