CCM: Adui namba moja Tanzania

CCM: Adui namba moja Tanzania

Msittu

Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
7
Reaction score
36
Kwa mizania yoyote ile, msingi wa kipimo cha mitazamo kwamba adui namba moja wa Tanzania kwa sasa ni CCM kitasalia kuwa ni falsafa ya chama hicho kikongwe.

Ukiacha falsafa yake, umri na uchama tawala ni nadharia nyingine muhimu ya ustawi wa uadui. Kushindwa kuiishi falsafa kumeunda falsafa mbadala kwa gharama ya Umma na sio wanachama wake. Gharama hizo ndio chanzo cha uadui.

Umri umebeba mambo mengi ndani yake ila kubwa ni uzazi na vizazi. CCM kwa kipindi chake imefanikiwa kuwa na uzao na kujenga vizazi ambavyo kwa namna moja ama nyingine vimezaliwa na hulka na utashi binafsi. Sifa hizo mbili zimekifanya kizazi hiki kuwa na hisia tofauti na wazazi wake pamoja na Ndugu. Huo ni msingi mwingine wa uadui.

Uchama tawala ni sehemu nyingine muhimu ya uadui. Kwa hisani ya demokrasia hili limewezekana. Utawala wa ilani, mali, watu, mitazamo na hisia zao ni msingi mkuu wa uadui.

Mwisho ni utaasisi. Hili huwenda matokeo yake yakawa bayana siku za usoni, mwenendo wa chama kukosa mamlaka ya kitaasisi umekifanya kisiwe na undugu na taasisi nyingine za kisiasa kwa ustawi wa siasa. Mtengano huo ndio unaotanua mitazamo ya uadui, matumizi ya dola ndani ya taasisi ya kisiasa ni utawala sio uongozi tena. Matokeo ya utawala huonekana bayana kwa watawaliwa kama ilivyo kwa uongozi yanavyo onekana kwa wanao ongozwa.

Ni mtazamo wa uadui utakao jenga urafiki. Adui ni rafiki wa kudumu.
 
hilo linajulikana wao ndio waliuza loliondo Leo wanatafuta kiki,wameingia mikataba ya hovyo na barick kimya kimya Leo kelele utadhani wamevumbua kitu kumbe hata mtoto hawezi kuingia mikataba ya kutoa mchanga Nchini na kupeleka nje...
 
Napingana na imani hii..

Adui namba moja wa taifa letu ni watu waoga, wanafiki na wenye kujikombakomba machoni pa wenye mamlaka!
Haya ni matokeo yaliyojengwa na adui. Matokeo ya kuwepo uadui uliotokana na uwepo wa adui siyo msingi wa tatizo. Tatizo kubwa ni kuwepo adui, ambaye hataki jamii imwone kama ndiyo adui, anataka jamii imwone kama ndiyo mkombozi wa jamii aliyoiangamiza
 
Boss Msittu Adui namba moja wa Tanzania ni Mwananchi na Mtanzania. Au kwa lugha nyepesi, Adui namba moja wa Tanzania ni Mimi, Wewe mleta mada, yule na yeye na wale.

Kwani CCM imewekwa na Madarakani na Mawe? Tatizo ni moja tu, Mwananchi bado tupo usingizini tena wa Pono. Wananchi bado hatujajua Haki zetu. Wananchi wengi hawajui Sheria na Katiba ya Nchi.

Marehemu Mwalimu alisema Adui namba moja wa Tanzania ni Ujinga na Maradhi na Umasikini.

Uzuri ninaouona ni kuwa Wananchi wanaanza kuamka, bado vijijini. Hii mitandao imesaidia sana. Pili Upinzani pamoja na udogo wao, wamefanya na wanafanya kazi kubwa sana. Bila upinzani wa kweli na madhubuti hakuna Maendeleo.

Kwa mizania yoyote ile, msingi wa kipimo cha mitazamo kwamba adui namba moja wa Tanzania kwa sasa ni CCM kitasalia kuwa ni falsafa ya chama hicho kikongwe.

Ukiacha falsafa yake, umri na uchama tawala ni nadharia nyingine muhimu ya ustawi wa uadui. Kushindwa kuiishi falsafa kumeunda falsafa mbadala kwa gharama ya Umma na sio wanachama wake. Gharama hizo ndio chanzo cha uadui.

Umri umebeba mambo mengi ndani yake ila kubwa ni uzazi na vizazi. CCM kwa kipindi chake imefanikiwa kuwa na uzao na kujenga vizazi ambavyo kwa namna moja ama nyingine vimezaliwa na hulka na utashi binafsi. Sifa hizo mbili zimekifanya kizazi hiki kuwa na hisia tofauti na wazazi wake pamoja na Ndugu. Huo ni msingi mwingine wa uadui.

Uchama tawala ni sehemu nyingine muhimu ya uadui. Kwa hisani ya demokrasia hili limewezekana. Utawala wa ilani, mali, watu, mitazamo na hisia zao ni msingi mkuu wa uadui.

Mwisho ni utaasisi. Hili huwenda matokeo yake yakawa bayana siku za usoni, mwenendo wa chama kukosa mamlaka ya kitaasisi umekifanya kisiwe na undugu na taasisi nyingine za kisiasa kwa ustawi wa siasa. Mtengano huo ndio unaotanua mitazamo ya uadui, matumizi ya dola ndani ya taasisi ya kisiasa ni utawala sio uongozi tena. Matokeo ya utawala huonekana bayana kwa watawaliwa kama ilivyo kwa uongozi yanavyo onekana kwa wanao ongozwa.

Ni mtazamo wa uadui utakao jenga urafiki. Adui ni rafiki wa kudumu.
 
Back
Top Bottom