screpa
JF-Expert Member
- Sep 10, 2015
- 10,792
- 15,693
Mmexico anayeaminika kuwa ni no1 pound-4-pound duniani kwa sasa leo atapanda ulingoni kutwangana na Kovalev; bingwa anayeshikilia mkanda wa WBO kwenye uzito wa Light Heavyweight. Endapo Canelo atafanikiwa kushinda pambano hili anatazamiwa kujivunia heshima kubwa sana kwenye boxing kwani amelazimika kupanda uzito kutoka uzito wake halisi 'middleweight' kwenda kwenye 'light heavyweight' ili kumchalenji bingwa huyo, kitu ambacho kimeonekana ni uthubutu wa hali ya juu 'risky'.