CAG aibua ufisadi wa kutisha NSSF

CAG aibua ufisadi wa kutisha NSSF

Bado kuna juhudi za kukwamisha ripoti hiyo, nimeona mbunge Ally Saleh kaandika kwenye akaunti yake ya Twitter kwamba kuna changamoto kwa wabunge kupata vitabu vyote 17 vya ripoti ya ukaguzi, mwenyekiti wa bunge nyoka wa makengeza amesema kwamba kuna gharama za kutoa nakala hizo ili kupata idadi hiyo ya vitabu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo gharama inafika 1.5 T?
 
Aisee ii haijawahi kutokea. Magu mwizi sana pesa zote hizi huishia CCM .

Najiuliza wale TISS ambao Rais Magifuli anajidai kawachomeka kia idara wanafanya kazi gani mbona hawafichui huu uozo??

Au na wao wpigaji tu.

umeamua kuropoka. kujifariji

2010???????

btw sio ndio CAG yupo na kaweka report wazi?

au CAG kapata wapi taarifa kwa akili zako fupi kama ndugai?
 
Mpaka sasa najiuliza kwa nini Spika alikuwa anakwamisha kwa maksudi kuanikwa kwa wizi huu

Katika ripoti ya CAG umeibuliwa ufundo wa hatari

Hasara katika Kununua Ardhi ya Sh. Bilion 4.17

CAG anasema..........Mfuko wa NSSF uliingia mikataba tarehe 16 Septemba 2010 na 12 Oktoba 2010 wa kununua ekari 277 (Muuzaji wa kwanza) na ekari 180 (Muuzaji wa pili) eneo la Kiluvya kwa Sh. bilioni 3.32 na Sh. bilioni 1.62, mtawalia. Kufuatia mapitio ya taarifa ya tathmini ya ekari 277 nilibaini kuwa thamani ya ardhi hiyo kwa
kipindi cha mwezi Oktoba 2010 ilikuwa Sh. milioni 416.40;
wakati makadirio ya thamani ya soko kwa ekari 180 ilikuwa Sh.milioni 720. Kwa hiyo, gharama ya ardhi iliyonunuliwa ilizidishwa kwa kiasi cha Sh. bilioni 2.90 na Sh. milioni 900 mtawalia na hivyo, kusababisha jumla ya hasara kuwa Sh.bilioni 3.80. Nilibaini pia kuwa, muuzaji wa kwanza aliripoti
mauzo yake kwa TRA kwa Sh. milioni 900 badala ya Sh. bilioni
3.32, kwa sababu hiyo kodi (stamp duty) ya Sh. milioni 24.24
haikulipwa.
Zaidi ya hayo, nilibaini hasara nyingine ya Sh. milioni 370
iliyotokana na NSSF kununua ekari 67.4 kwa muuzaji bandia
eneo la Nunge, Bagamoyo. Mahakama ya wilaya katika shauri
la madai shauri Na. 7 la 2003 na Mahakama Kuu katika Rufani
ya Madai ya shauri Na. 7 la 2006 ilibaini kwamba, muuzaji
hakuwa mmiliki wa ardhi ambayo iliuzwa kwa NSSF. Kwa
ujumla, NSSF ilipata hasara ya Sh. bilioni 4.17 katika kununua
ardhi na ililipa kiasi kidogo cha kodi (stamp duty) kwa Sh.
milioni 24.24.
Ninapendekeza kuwa Bodi ya Mfuko na Menejimenti ichukue
hatua stahiki kwa wale waliohusika katika mchakato mzima wa kununua ardhi iliyosababisha hasara hiyo ya Sh. bilioni 4.17

Watumishi kugawiwa mabilioni kununua hisa vodacom bila riba wala mikataba

CAG anasema..............
Mfuko ulitoa mkopo bila riba wa Sh. bilioni 1.65 kwa watumishi
na Sh. milioni 206 kwa wachangiaji (Members) wengine ili kununua hisa za Vodacom. Hata hivyo, hakukuwa na mikataba kati ya Mfuko na wanufaika hao. Pia, namna ya urejeshwaji wa mikopo iliyotolewa kwa wachangiaji wengine imebaki kuwa
mashakani. Mkopo uliotolewa kwa wachangiaji wengine
ulikuwa kinyume na mafao yaliyoelezwa katika sehemu ya
Sheria ya Pesheni ya NSSF ya mwaka 2015.
Kukosekana kwa mikataba kwa fedha zilizolipwa kwa ununuzi
wa hisa za Vodacom kati ya Mfuko na wanufaika wa mkopo
kunaweka mazingira ya wakopaji kutokurejesha mikopo hiyo.

Hakika nchi hii inaliwa.
Midomo ya Watanzania wote ifungwe,na Magufuli aendelee kutumbua.Magufuli tumbua baba tumbua.Ila kwa uozo huu alioibua CAG,Magufuli Rais wangu sitakuelewa kama bado mahakama ya mafisadi itakuwa na upungufu wa wateja.No wonder Ndugai alikuwa anakwamisha uwakilishwaji wa report ya CAG bungeni,sijui ilikuwa conspiracy?
 
Sikiliza ewe mdau, hakuna anayepingana na majukumu ya CAG bali ni anakosa uungwana ktk kauli, anatakiwa atofautishe kati ya lugha za kiprofessional na lugha za wanasiasa. Na ikumbukwe kilichofanyika ktk ukaguzi ni maelekezo ya serikali.
You very smart... wewe umeuelewa ukweli
CAG na Bunge wanatakiwa kufanya kazi pamoja..
Ukiita Bunge dhaifu then fanya peke yako...
Amegeuzwa mfungaji bora aliyelewa sifa wenzako 10 wanamsusia uwanja.. Kila mtu ana umuhimu wake. Na kama bunge kuna madhaifu Yes.. tumia professional language at least mnahitajiana kufanya kazi pamoja
Bila Bunge CAG ataendelea kuwanenepesha wapenda udaku ila hatolisaidia taifa koz hana meno/nguvu zaidi ya kuandika taarifa. Bunge/PAC ndio wenye kutendea kazi taarifa zake...
Spika na CAG waweke pembeni ego wafanye kazi pamoja kwa faida ya Taifa
 
CAG hakufanya ukaguzi wa mwaka 2010, Ukaguzi wa mwaka huu ni wa Kuanzia July 2017 hadi Juni 2018 Msituchanganye
 
You very smart... wewe umeuelewa ukweli
CAG na Bunge wanatakiwa kufanya kazi pamoja..
Ukiita Bunge dhaifu then fanya peke yako...
Amegeuzwa mfungaji bora aliyelewa sifa wenzako 10 wanamsusia uwanja.. Kila mtu ana umuhimu wake. Na kama bunge kuna madhaifu Yes.. tumia professional language at least mnahitajiana kufanya kazi pamoja
Bila Bunge CAG ataendelea kuwanenepesha wapenda udaku ila hatolisaidia taifa koz hana meno/nguvu zaidi ya kuandika taarifa. Bunge/PAC ndio wenye kutendea kazi taarifa zake...
Spika na CAG waweke pembeni ego wafanye kazi pamoja kwa faida ya Taifa
Spika yupi unamzungumzia? huyuhuyu hopeless?
 
Mpaka sasa najiuliza kwa nini Spika alikuwa anakwamisha kwa maksudi kuanikwa kwa wizi huu
Katika ripoti ya CAG umeibuliwa ufundo wa hatari
Hasara katika Kununua Ardhi ya Sh. Bilion 4.17
CAG anasema......
Mfuko wa NSSF uliingia mikataba tarehe 16 Septemba 2010 na 12 Oktoba 2010 wa kununua ekari 277 (Muuzaji wa kwanza) na ekari 180 (Muuzaji wa pili) eneo la Kiluvya kwa Sh. bilioni 3.32 na Sh. bilioni 1.62, mtawalia. Kufuatia mapitio ya taarifa ya tathmini ya ekari 277 nilibaini kuwa thamani ya ardhi hiyo kwa kipindi cha mwezi Oktoba 2010 ilikuwa Sh. milioni 416.40; wakati makadirio ya thamani ya soko kwa ekari 180 ilikuwa Sh.milioni 720. Kwa hiyo, gharama ya ardhi iliyonunuliwa ilizidishwa kwa kiasi cha Sh. bilioni 2.90 na Sh. milioni 900 mtawalia na hivyo, kusababisha jumla ya hasara kuwa Sh.bilioni 3.80.
Nilibaini pia kuwa, muuzaji wa kwanza aliripoti mauzo yake kwa TRA kwa Sh. milioni 900 badala ya Sh. bilioni 3.32, kwa sababu hiyo kodi (stamp duty) ya Sh. milioni 24.24 haikulipwa.
Zaidi ya hayo, nilibaini hasara nyingine ya Sh. milioni 370 iliyotokana na NSSF kununua ekari 67.4 kwa muuzaji bandia eneo la Nunge, Bagamoyo. Mahakama ya wilaya katika shauri la madai shauri Na. 7 la 2003 na Mahakama Kuu katika Rufani ya Madai ya shauri Na. 7 la 2006 ilibaini kwamba, muuzaji hakuwa mmiliki wa ardhi ambayo iliuzwa kwa NSSF.
Kwa ujumla, NSSF ilipata hasara ya Sh. bilioni 4.17 katika kununua ardhi na ililipa kiasi kidogo cha kodi (stamp duty) kwa Sh. milioni 24.24.
Ninapendekeza kuwa Bodi ya Mfuko na Menejimenti ichukue hatua stahiki kwa wale waliohusika katika mchakato mzima wa kununua ardhi iliyosababisha hasara hiyo ya Sh. bilioni 4.17

Watumishi kugawiwa mabilioni kununua hisa Vodacom bila riba wala mikataba
CAG anasema....
Mfuko ulitoa mkopo bila riba wa Sh. bilioni 1.65 kwa watumishi na Sh. milioni 206 kwa wachangiaji (Members) wengine ili kununua hisa za Vodacom. Hata hivyo, hakukuwa na mikataba kati ya Mfuko na wanufaika hao. Pia, namna ya urejeshwaji wa mikopo iliyotolewa kwa wachangiaji wengine imebaki kuwa mashakani.
Mkopo uliotolewa kwa wachangiaji wengine ulikuwa kinyume na mafao yaliyoelezwa katika sehemu ya Sheria ya Pesheni ya NSSF ya mwaka 2015.
Kukosekana kwa mikataba kwa fedha zilizolipwa kwa ununuzi wa hisa za Vodacom kati ya Mfuko na wanufaika wa mkopo kunaweka mazingira ya wakopaji kutokurejesha mikopo hiyo.

Hakika nchi hii inaliwa.
Maranyingi nilikuwa naandika kuhusu mfumo wa NSSF kuwa hoi kifedha kiasi cha kushindwa kuwalipa wastaafu, jambo ambalo liliifanya NSSF iwalipe kila baada ya makusanyo ya mwezi! Walioifilisi NSSF wanajulikana kwani wanadai walikopa ila hawalipi! NSSF imesahau wajibu wake kwa wastaafu na kuwa mradi wa kuneemesha serikali na wajanja! NSSF haina uwezo wa kuongeza viwango vya pensheni.
 
Bado kuna juhudi za kukwamisha ripoti hiyo, nimeona mbunge Ally Saleh kaandika kwenye akaunti yake ya Twitter kwamba kuna changamoto kwa wabunge kupata vitabu vyote 17 vya ripoti ya ukaguzi, mwenyekiti wa bunge nyoka wa makengeza amesema kwamba kuna gharama za kutoa nakala hizo ili kupata idadi hiyo ya vitabu

Sent using Jamii Forums mobile app
Prof. Mussa Juma Assaad meshasema kwamba gharama ya vitabu ilikuwa kubwa kwa iyo ipo kwy Pdf zinapatikana zotee
Technology hatari sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni kweli kuna haja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani naye
 
Back
Top Bottom