BVR yaingia rasmi Kigoma kimya kimya

BVR yaingia rasmi Kigoma kimya kimya

Nicholaus Kilunga

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2014
Posts
1,188
Reaction score
570
BVR yaingia rasmi mkoa wa Kigoma na Kagera,zoezi kuanza rasmi 21/5/2015

Hivi unajua kuchagua na kuchaguliwa ni haki yako ya msingi?na kwamba maendeleo bora yako wewe,jamii.yako na taifa kwa ujumla yanategemea uamuzi wako katika kuchagua?amka acha uvivu wa kwenda kituoni,acha kujifanya bize mpaka ukose mda wa kujiandikisha ama kusimama kwenye foleni ya kujiandikisha,Tz ni yetu sote,acha ubinafsi wa kujifikiria wewe na kizazi cha leo,vpi kuhusu kesho?zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu kwa mikoa ya Kigoma na Kagera litaanza rasmi 21/5/2015,jitokeze wewe na jamaa zako mkajiandikishe,wahi mapema sana,Kupanga ni kuchagua mtanzania,panga kujiandikisha,chagua kupiga kura,
Sambaza ujumbe huu sambaza upendo
 
Zoezi la uandikishaji wa daftari la kundumu la mpiga kura wilaya Kibondo litakuwa kama ifuatavyo. Tarehe 21.5 hadi 27.5 itakuwa ktk kata za Kagezi, Kumsenga, Kizazi, Mkabuye na Itaba. Tarehe 29.5 hadi 4.6 itakuwa ktk Kata za Mabamba, Busunzu, Busagara na Nyaruyoba. Tarehe 6.6 hadi 12.6 itakuwa ktk Kata za Rugongwe, Rusohoko, Kitahana, Murungu na Bunyambo. Na tarehe 14.6 hadi 20.6 itakuwa ktk Kata za Bitare, Misezero, Biturana, Kumwambu na Kibondo mjini. Wahi kajiandikishe kwa kufuata ratiba hiyo.
 
ni jambo jema.baadhi ya maeneo nasikia vyama vya siasa vinazuiwa kuwatangazia wafuasi wao na wananchi kiujumla. hilo sio jambo jema hata kidogo.wana kigoma na mae.neo menhime jitokezrni kwa wingi.
 
Wambie viongozi wa vyama vya upinzani wahakikishe kila mwananchi anapewa taarifa ajiandikishe.
 
Nick naomba unieleze wilaya ya Kakonko wanaanza lini?
 
Dar sijui ni lini aisee..,Nina hamasa kubwa sana ya kujiandikisha
 
Back
Top Bottom