Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Hofu imetanda kwa baadhi ya wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Nyankanga, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara, (wajumbe) baada ya uwepo wa fununu za kuenguliwa kwa mtia nia wa nafasi ya udiwani katika Kata hiyo Bw. Emmanuel Musuya, aliyeongoza katika kura za maoni na kurejeshwa jina la mtia nia mwingine aliyeshika nafasi ya pili jambo ambalo baadhi ya wajumbe hawakubaliani nalo.