Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,466
Kwa heshima kubwa sana, naomba ajitokeze mwenye busara au wenye busara ndani ya CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO. Ayaweke chini makundi yanayosigishana, kundi la ZZK na kundi lingine ambalo sijui nani kinara, wazungumze migogoro yao yote wayamalize. Tumekuwa tukishuhudia hivi vitimbi kwa miaka minne sasa au zaidi na kila siku ugomvi huu na mvutano huu unachanganya wanachama.
Kama hakuna uwezekano wa kumaliza ugomvi huu ambao unatuchosha sisi wanachama, Viongozi wakuu simameni hadharani mseme mmeshindwa kudhibiti vitimbi ndania ya chama. Hatuwezi kuendesha chama kwenye mitandao na ghilba. Kila mwenye hasira kuaznisha balaa kila siku.
Hakuna taasisi duniani inaendeshwa eti tu kwasababu mnakubaliana au mnapendana la hasha ni kwasababu ya kila mtu kufuata sheria na kuadhibiwa na sheria alizo apa kuzifuata. Leo mitandao ndio sehemu ya viongozi wa chama kufanya maamuzi. sio sahahihi kila mtu ana facebook, tweet, JF ila sijaona wenye busara waliopewa madaraka wakaanza kulalamika kwenye mitandao au kushutumiana kwenye mitandao, ikifa huko watu makini wanajiuzulu au kutafuta suluhu.
Tumechoka na vituko, kiongozi yeyote anayeleta mtafaruku na kiongozi mwenzeke wanaokutana kwenye vikao tunavyolipia kwa gharama zetu hafai kabisa kuwa mwakilishi wa watu. Ukishindwa kuelewana na watu chini ya mia mnaotakiwa kutuongazo kweli itawezekana?
Kaeni chini zunguzmzeni, acheni kutuchanganya.
Chief Mkwawa -Busara iliombwa na wenye hekima. Hekima huombwa kwa Mungu huzaliwi nayo.
Kama hakuna uwezekano wa kumaliza ugomvi huu ambao unatuchosha sisi wanachama, Viongozi wakuu simameni hadharani mseme mmeshindwa kudhibiti vitimbi ndania ya chama. Hatuwezi kuendesha chama kwenye mitandao na ghilba. Kila mwenye hasira kuaznisha balaa kila siku.
Hakuna taasisi duniani inaendeshwa eti tu kwasababu mnakubaliana au mnapendana la hasha ni kwasababu ya kila mtu kufuata sheria na kuadhibiwa na sheria alizo apa kuzifuata. Leo mitandao ndio sehemu ya viongozi wa chama kufanya maamuzi. sio sahahihi kila mtu ana facebook, tweet, JF ila sijaona wenye busara waliopewa madaraka wakaanza kulalamika kwenye mitandao au kushutumiana kwenye mitandao, ikifa huko watu makini wanajiuzulu au kutafuta suluhu.
Tumechoka na vituko, kiongozi yeyote anayeleta mtafaruku na kiongozi mwenzeke wanaokutana kwenye vikao tunavyolipia kwa gharama zetu hafai kabisa kuwa mwakilishi wa watu. Ukishindwa kuelewana na watu chini ya mia mnaotakiwa kutuongazo kweli itawezekana?
Kaeni chini zunguzmzeni, acheni kutuchanganya.
Chief Mkwawa -Busara iliombwa na wenye hekima. Hekima huombwa kwa Mungu huzaliwi nayo.