Burundi-mzozo wa katiba

Burundi-mzozo wa katiba

Inkoskaz

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
6,360
Reaction score
2,389
Mawaziri watatu kutoka chama cha UPRONA ambacho ni chama kikuu cha upinzani wamejiuzulu kutii maagizo ya kamati kuu ya chama chao kupinga mabadiliko ya katiba in favour of raisi Nkurunzinza
 
Ni aibu kwa rika jipya la viongozi wa Africa kuwa na uchu wa madaraka kama ilivyokuwa kwa rika la viongozi waasisi wakina Kamuzu Banda, Mobutu, Omar Bongo, Mugabe etc

Kwa rika hili la kina Nkurunziza, Kabila Jr na Rajoelina tulitegemea kupata kwao nafasi basi tutapata Africa mpya yenye muono mpya wa kujali demokrasia na ukomo wa madaraka kwa kuheshimu katiba lakini mambo ni yale yale. Hii ni laana!
 
Mawaziri watatu kutoka chama cha UPRONA ambacho ni chama kikuu cha upinzani wamejiuzulu kutii maagizo ya kamati kuu ya chama chao kupinga mabadiliko ya katiba in favour of raisi Nkurunzinza

Hayo mabadiliko ya katiba hayajapitishwa.Hivi mtu anaweza kujiuzulu kupinga kitu ambacho hakipo na hakijapitishwa na bunge.Unajiuzulu kwa kupinga mapendekezo au mawazo ya wengine ambayo hayajapitishwa na kuwa Katiba?

UPRONA ni chama kikongwe Burundi na kina watu makini nje ya kamati kuu naamini muafaka utapatikana tu.Ila uamuzi wa UPRONA kuagiza wateule wa raisi wajiuzulu kwa kitu ambacho hakijapita naona Kamati kuu ya UPRONA imeteleza na ni udikteta wa kutotenganisha kofia ya chama na serikali.Ieleweke hao mawaziri waliteuliwa watumikie warundi wote sio watumikie UPRONA tu.Kuwalazimisha wajiuzulu kumewakosesha warundi mawaziri wazuri tegemeo la warundi wengi waliokuwa wanaridhishwa na utendaji wao maana hawajajiuzulu kwa kashfa yeyote.UPRONA iangalie maslahi mapana ya warundi wote badala ya kujikita kwenye maslahi ya Chama tu.

Imani yangu warundi wana hekima na uwezo wa kulimaliza hili yataisha muda si mrefu.
 
Back
Top Bottom