Buriani Pendo, Buriani mpenzi yangu

Buriani Pendo, Buriani mpenzi yangu

Pole sana mkuu,kifo tumeumbiwa sisi lakini hakizoeleki kamwe,cha muhimu na sisi tulio hai tujifanyie maandalizi ya siku yetu ikifika.......
Narudia tena kukupa pole mkuu
 
Naulazimisha mtima, uikubali hatima,
Mikono nikiachama , isilishikize tama ,
Japo chozi aandama , ujasiri najipima
Niseme si langu fungu , haujakubali mtima
Duniani si pa kwetu,sisi sote wapitaji
Moyo jipe wanakwetu, uvumilivu wako mtaji
Ndiye mfariji kwetu,hakika tavikwa taji
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia

Hakika Sasa yatosha,kufuru Mola utaja
Uchungu unapotosha,Sababu nyingi kutaja
Utulivu Sasa onesha,Lia panapo haja
Hakika atakalo Mola,binadamu hawezi zuia

Tuunge zetu nia,da Pendo muombea
Huku kitumainia, Siku moja kutania
Moyoni aminia,Dua zetu kutimia
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia
 
Duniani si pa kwetu,sisi sote wapitaji
Moyo jipe wanakwetu, uvumilivu wako mtaji
Ndiye mfariji kwetu,hakika tavikwa taji
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia

Hakika Sasa yatosha,kufuru Mola utaja
Uchungu unapotosha,Sababu nyingi kutaja
Utulivu Sasa onesha,Lia panapo haja
Hakika atakalo Mola,binadamu hawezi zuia

Tuunge zetu nia,da Pendo muombea
Huku kitumainia, Siku moja kutania
Moyoni aminia,Dua zetu kutimia
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia
Sasa nimeamiani , kwa maulana twarudi
Tupo tuu mapitoni, upendo na uwe jadi
Saidia wa shidani, bila kujali idadi
Tumekosa nini Kifo , watuacha tu wakiwa

Kwake tuu maulana , ipo siku tutarudi
Ungetupa kuagana, kifo acha makusudi
Wabeba na wema sana, hata wale maridadi
Tumekosa nini kifo, watuacha tu wakiwa

Tunaamka alfajiri, na kuwasha telephoni
Twaambiwa yalojiri, kila siku ni msibani
Kifo achaga kiburi, kweli vilio huvioni
Tumekosa nini kifo , watuacha tu wakiwa
 
Ni juzi tulikuwako, kwa karamu yakufana
Ikiwa bathdei yako, Da! Pati ya kuagana
Ukanita Niko ,Niko, Ati hatuta achana
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Siamini umeenda, hatutaonana tena
Yote tuliyoyatenda, hayatarudia tena
Popote tulipo kwenda, hatuwezi fika tena
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Siamini hutofika, kawaida kusalimu
Kwa utani tukicheka, Dah! Hilo tabasamu
Malengo yakipangika, mbeleni ndoa muhimu
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Ukapanga lake jina, la mtoto tukijaliwa
Kwa wakike Rihanna, wa kiume majaliwa
Ni mipango mingi sana, tulopanga maridhawa
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Umeniacha na kidonda, kutwa kucha ninakonda
Giza nene limetanda, moyo wangu ulipenda
Pendo leo umeenda, Najua sio kwa kupenda
Ni seme si langu fungu, haujakubali mtima

Moyo wajawa uchungu, hauijui hatima
Kwaheri', Mapenzi yangu, yamebakia yatima
Nisamehe sana Mungu, nizitoapo lawama
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Ukaandika wosia, nifikie mazikoni
Eti niache kulia, siwezi huo mtihani
We ukiniandikia, pendo ulilia nini?
Mama yote kanitonya, kweli tulipendana

Nenda salama pendo, sisahau abadani
Ulinifunza upendo, uliozidi uzani
Umeacha pengo, pendo, Mpaka nije kwa manani
Kwaheri' mpenzi, Tutaonana baadae
Pole Sana! Hongera kwa kuendeleza Sanaa ya ushairi!
 
Kwa hiyo Pendo amekufa akiwa katika status ya "uasherati".

Maana yake, kutokana na maelezo yako mwenyewe, wewe na marehemu mlikuwa hamjafunga ndoa, ila mlikuwa mnafanya "uasherati".

Kumbuka imeandikwa, "wazinzi na waasherati hawatauona Ufalme wa MUNGU kamwe".

Hakuna ajuaye siku ya kufa, hivyo basi ni vema sana kila aliye hai sasa hivi akajitahidi sana kuishi maisha ya usafi.

Usiogope kufa, bali, ogopa sana kufa ukiwa na DHAMBI!!!!!

Mwenye masikio na asikie.
Usihukumu maana hukumu ni juu ya Mungu peke yake, hakuna aliye mkamilifu katika hii dunia, Mungu wetu ni mwingi wa rehema na ni mwepesi wa kusamehe.
 
Ni juzi tulikuwako, kwa karamu yakufana
Ikiwa bathdei yako, Da! Pati ya kuagana
Ukanita Niko, niko, Ati hatuta achana
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Siamini umeenda, hatutaonana tena
Yote tuliyoyatenda, hayatarudia tena
Popote tulipo kwenda, hatuwezi fika tena
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Siamini hutofika, kawaida kusalimu
Kwa utani tukicheka, Dah! Hilo tabasamu
Malengo yakipangika, mbeleni ndoa muhimu
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Ukapanga lake jina, la mtoto tukijaliwa
Kwa wakike Rihanna, wa kiume majaliwa
Ni mipango mingi sana, tulopanga maridhawa
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Umeniacha na kidonda, kutwa kucha ninakonda
Giza nene limetanda, moyo wangu ulipenda
Pendo leo umeenda, Najua sio kwa kupenda
Ni seme si langu fungu, haujakubali mtima

Moyo wajawa uchungu, hauijui hatima
Kwaheri', Mapenzi yangu, yamebakia yatima
Nisamehe sana Mungu, nizitoapo lawama
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima

Ukaandika wosia, nifikie mazikoni
Eti niache kulia, siwezi huo mtihani
We ukiniandikia, pendo ulilia nini?
Mama yote kanitonya, kweli tulipendana

Nenda salama pendo, sisahau abadani
Ulinifunza upendo, uliozidi uzani
Umeacha pengo, pendo, Mpaka nije kwa manani
Kwaheri' mpenzi, Tutaonana baadae
Samahani mkuu weka picha ya pendo tupate kumjua inawezekana ni ndug yangu
 
Kwa hiyo Pendo amekufa akiwa katika status ya "uasherati".

Maana yake, kutokana na maelezo yako mwenyewe, wewe na marehemu mlikuwa hamjafunga ndoa, ila mlikuwa mnafanya "uasherati".

Kumbuka imeandikwa, "wazinzi na waasherati hawatauona Ufalme wa MUNGU kamwe".

Hakuna ajuaye siku ya kufa, hivyo basi ni vema sana kila aliye hai sasa hivi akajitahidi sana kuishi maisha ya usafi.

Usiogope kufa, bali, ogopa sana kufa ukiwa na DHAMBI!!!!!

Mwenye masikio na asikie.
Haya, wewe ambaye sio mzinzi na muasherati umeshawahi kuuona huo ufalme?
 
Ndo mana huwa sifall in love NAOGOPA SANA KUMPOTEZA MTU NITAEMPENDA,sina hakika kama nitaweza kuvumilia uchungu wale..
 
Ndo mana huwa sifall in love NAOGOPA SANA KUMPOTEZA MTU NITAEMPENDA,sina hakika kama nitaweza kuvumilia uchungu wale..
Ni hatari sana , nyakat zote nzuri mlizokuwa nazo hazitafutika maishani
 
Back
Top Bottom