KING ASSENGA
JF-Expert Member
- Oct 8, 2016
- 929
- 1,494
- Thread starter
- #41
SarataniSijasoma, vipi Pendo ni muhanga wa ajali bukoba?
SarataniSijasoma, vipi Pendo ni muhanga wa ajali bukoba?
Asante mkuuDah mko vzr kwenye mashahiri umelipatia haswa
Kuaandika kwa hisia Kali ndio maana linagusa moyoNi nzuri hili shairi
Na wee ulilipatia haswaaa goodKuaandika kwa hisia Kali ndio maana linagusa moyo
Itapendeza kama atachukua nafasi ya Pendo kumuondolea huzuni mwambaNa wee ulilipatia haswaaa good
Pole sana mkuu,kifo tumeumbiwa sisi lakini hakizoeleki kamwe,cha muhimu na sisi tulio hai tujifanyie maandalizi ya siku yetu ikifika.......Saratani
Duniani si pa kwetu,sisi sote wapitajiNaulazimisha mtima, uikubali hatima,
Mikono nikiachama , isilishikize tama ,
Japo chozi aandama , ujasiri najipima
Niseme si langu fungu , haujakubali mtima
Sasa nimeamiani , kwa maulana twarudiDuniani si pa kwetu,sisi sote wapitaji
Moyo jipe wanakwetu, uvumilivu wako mtaji
Ndiye mfariji kwetu,hakika tavikwa taji
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia
Hakika Sasa yatosha,kufuru Mola utaja
Uchungu unapotosha,Sababu nyingi kutaja
Utulivu Sasa onesha,Lia panapo haja
Hakika atakalo Mola,binadamu hawezi zuia
Tuunge zetu nia,da Pendo muombea
Huku kitumainia, Siku moja kutania
Moyoni aminia,Dua zetu kutimia
Hakika atakalo mola,binadamu hawezi zuia

Pole Sana! Hongera kwa kuendeleza Sanaa ya ushairi!Ni juzi tulikuwako, kwa karamu yakufana
Ikiwa bathdei yako, Da! Pati ya kuagana
Ukanita Niko ,Niko, Ati hatuta achana
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Siamini umeenda, hatutaonana tena
Yote tuliyoyatenda, hayatarudia tena
Popote tulipo kwenda, hatuwezi fika tena
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Siamini hutofika, kawaida kusalimu
Kwa utani tukicheka, Dah! Hilo tabasamu
Malengo yakipangika, mbeleni ndoa muhimu
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Ukapanga lake jina, la mtoto tukijaliwa
Kwa wakike Rihanna, wa kiume majaliwa
Ni mipango mingi sana, tulopanga maridhawa
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Umeniacha na kidonda, kutwa kucha ninakonda
Giza nene limetanda, moyo wangu ulipenda
Pendo leo umeenda, Najua sio kwa kupenda
Ni seme si langu fungu, haujakubali mtima
Moyo wajawa uchungu, hauijui hatima
Kwaheri', Mapenzi yangu, yamebakia yatima
Nisamehe sana Mungu, nizitoapo lawama
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Ukaandika wosia, nifikie mazikoni
Eti niache kulia, siwezi huo mtihani
We ukiniandikia, pendo ulilia nini?
Mama yote kanitonya, kweli tulipendana
Nenda salama pendo, sisahau abadani
Ulinifunza upendo, uliozidi uzani
Umeacha pengo, pendo, Mpaka nije kwa manani
Kwaheri' mpenzi, Tutaonana baadae
Unaona au kuelewa aje?Ni shairi ?? Au
Pendo wako ame rest in peace !Unaona au kuelewa aje?
Usihukumu maana hukumu ni juu ya Mungu peke yake, hakuna aliye mkamilifu katika hii dunia, Mungu wetu ni mwingi wa rehema na ni mwepesi wa kusamehe.Kwa hiyo Pendo amekufa akiwa katika status ya "uasherati".
Maana yake, kutokana na maelezo yako mwenyewe, wewe na marehemu mlikuwa hamjafunga ndoa, ila mlikuwa mnafanya "uasherati".
Kumbuka imeandikwa, "wazinzi na waasherati hawatauona Ufalme wa MUNGU kamwe".
Hakuna ajuaye siku ya kufa, hivyo basi ni vema sana kila aliye hai sasa hivi akajitahidi sana kuishi maisha ya usafi.
Usiogope kufa, bali, ogopa sana kufa ukiwa na DHAMBI!!!!!
Mwenye masikio na asikie.
Samahani mkuu weka picha ya pendo tupate kumjua inawezekana ni ndug yanguNi juzi tulikuwako, kwa karamu yakufana
Ikiwa bathdei yako, Da! Pati ya kuagana
Ukanita Niko, niko, Ati hatuta achana
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Siamini umeenda, hatutaonana tena
Yote tuliyoyatenda, hayatarudia tena
Popote tulipo kwenda, hatuwezi fika tena
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Siamini hutofika, kawaida kusalimu
Kwa utani tukicheka, Dah! Hilo tabasamu
Malengo yakipangika, mbeleni ndoa muhimu
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Ukapanga lake jina, la mtoto tukijaliwa
Kwa wakike Rihanna, wa kiume majaliwa
Ni mipango mingi sana, tulopanga maridhawa
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Umeniacha na kidonda, kutwa kucha ninakonda
Giza nene limetanda, moyo wangu ulipenda
Pendo leo umeenda, Najua sio kwa kupenda
Ni seme si langu fungu, haujakubali mtima
Moyo wajawa uchungu, hauijui hatima
Kwaheri', Mapenzi yangu, yamebakia yatima
Nisamehe sana Mungu, nizitoapo lawama
Niseme si langu fungu, haujakubali mtima
Ukaandika wosia, nifikie mazikoni
Eti niache kulia, siwezi huo mtihani
We ukiniandikia, pendo ulilia nini?
Mama yote kanitonya, kweli tulipendana
Nenda salama pendo, sisahau abadani
Ulinifunza upendo, uliozidi uzani
Umeacha pengo, pendo, Mpaka nije kwa manani
Kwaheri' mpenzi, Tutaonana baadae
Haya, wewe ambaye sio mzinzi na muasherati umeshawahi kuuona huo ufalme?Kwa hiyo Pendo amekufa akiwa katika status ya "uasherati".
Maana yake, kutokana na maelezo yako mwenyewe, wewe na marehemu mlikuwa hamjafunga ndoa, ila mlikuwa mnafanya "uasherati".
Kumbuka imeandikwa, "wazinzi na waasherati hawatauona Ufalme wa MUNGU kamwe".
Hakuna ajuaye siku ya kufa, hivyo basi ni vema sana kila aliye hai sasa hivi akajitahidi sana kuishi maisha ya usafi.
Usiogope kufa, bali, ogopa sana kufa ukiwa na DHAMBI!!!!!
Mwenye masikio na asikie.
Ni hatari sana , nyakat zote nzuri mlizokuwa nazo hazitafutika maishaniNdo mana huwa sifall in love NAOGOPA SANA KUMPOTEZA MTU NITAEMPENDA,sina hakika kama nitaweza kuvumilia uchungu wale..![]()
Nimemhukumu nani? Na nimetoa hukumu gani?Usihukumu maana hukumu ni juu ya Mungu peke yake, hakuna aliye mkamilifu katika hii dunia, Mungu wetu ni mwingi wa rehema na ni mwepesi wa kusamehe.