Bungeni Hakuna First Aid (Huduma ya Kwanza)

Bungeni Hakuna First Aid (Huduma ya Kwanza)

PastorPetro

Senior Member
Joined
Feb 25, 2008
Posts
189
Reaction score
37
Wana JF, nimesikitika sana kusika habari ya kifo cha Mbunge wa Chambani Pemba, Mh. Salim Hemed Khamis. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahala pema peponi. Amin.

Kwa kweli nimeshutuka kuona picha ya Mh. akibebwa na wenzake, kicha huko, miguu kule. Pia nimesoma habari katika gazeti la Nipashe kuhusu jinsi wabunge wenzake walivyojaribu kumhudumia alipopatwa na matatizo, eti walimpepea. Jamani, hivi Bunge la Tanzania haina watu wa First Aid ambao wanakaa pale wakati wa mikutano? Hakuna Ambulance? Mwaka 2013, kuna watu walipitia kozi Red Cross, wange saidia! Yaani kubebwa vibaya inaweza kuzidisha ugonjwa au kufanya hali iwe mbaya zaidi.

Serikali inawanunulia magari ya fahari ya bei mbaya! Je, itakuwa shilingi ngapi kuweka watu wa First Aid Bungeni? :A S 39:
 
Wana JF, nimesikitika sana kusika habari ya kifo cha Mbunge wa Chambani Pemba, Mh. Salim Hemed Khamis. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahala pema peponi. Amin.

Kwa kweli nimeshutuka kuona picha ya Mh. akibebwa na wenzake, kicha huko, miguu kule. Pia nimesoma habari katika gazeti la Nipashe kuhusu jinsi wabunge wenzake walivyojaribu kumhudumia alipopatwa na matatizo, eti walimpepea. Jamani, hivi Bunge la Tanzania haina watu wa First Aid ambao wanakaa pale wakati wa mikutano? Hakuna Ambulance? Mwaka 2013, kuna watu walipitia kozi Red Cross, wange saidia! Yaani kubebwa vibaya inaweza kuzidisha ugonjwa au kufanya hali iwe mbaya zaidi.

Serikali inawanunulia magari ya fahari ya bei mbaya! Je, itakuwa shilingi ngapi kuweka watu wa First Aid Bungeni? :A S 39:

Ni kweli inasikitisha kuona mtu, tena Mhe Mbunge, anahudumiwa kienyeji hivyo. Sio suala la kuwa na watu wa First Aid Bungeni tu, bali dhana ya maisha bora kwa kila mbongo inaelekeza (kama isingekuwa ni usanii) huduma kama hii kusambazwa kwa wananchi wote kwa kununua ambulances nyingi (badala ya mashangigi mengi ambayo hayawasiadii hata wanaoyatumia kuokoa maisha yao) na kujenga vituo vya huduma ya kwanza ambapo kila kituo kitakuwa na ambulance na wataalamu wa huduma ya kwanza kumhudumia na kumkimbiza hospitalini kila mwananchi anayepatwa na matatizo kama hayo. Hayo ndio maisha bora kwa kila mtanzania (public service, public service) sio kutujengea vikwanguaanga kila pembe ya jiji na kujaza mishangingi barabarani wakati mtu, tena mhe mbunge akiwa kazini, hawezi kupatiwa huduma ya kwanza iliyo bora. Shame on us bongolanders!!!!
 
First Aid??? kila mbunge ana readings zake before overdue unawahi zako Apollo.

Let mhe RIP
 
Ngoja nijikumbukiye mambo ya nchi yangu.

Kuna siku magari ya kuzima moto yalitembelea pale Magogoni; kisa pasi imesahauliwa na moto ukawaka hapakuwa na namna ya kuudhibiti bali kuruhusu magari ya zimamoto yakiongozwa na ya makampuni ya binafsi.

Waweza tafakari usalama wa taifa hili; ruhusu macho yako kuangaza; utaona mgorofa pembezoni mwa hospitali ya Matibabu ya Kansa. Uliza kama taratibu zinaruhusu mgorofa kama ule kujengwa eneo hilo. Tunza jibu hilo moyoni mwako huenda siku ya mwisho utasemezana na Muumba wako. Naye akusimuliye lengo la kuweka madini lukuki ndani ya taifa hili na kama anafurahia kuona watz wakiwa hohe hahe.

Pumza kwa amani.
Umetutoka sijui sikio la kufa litajifunza lolote kwa kifo chako.
 
Hivi Bungeni na sokoni Kariakoo wapi ni mazingira hatari?

Badala ya kutaka ambulance iwekwe standby sokoni Kariakoo wewe unataka iwekwe nje ya vyumba vya mikutano ya wabunge!!! Au kwa sababu wanaopata matatizo ya kiafya ghafla sokoni Kariakoo hawapigwi picha na kuwekwa kwenye blogs?
 
Wana JF, nimesikitika sana kusika habari ya kifo cha Mbunge wa Chambani Pemba, Mh. Salim Hemed Khamis. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahala pema peponi. Amin.

Kwa kweli nimeshutuka kuona picha ya Mh. akibebwa na wenzake, kicha huko, miguu kule. Pia nimesoma habari katika gazeti la Nipashe kuhusu jinsi wabunge wenzake walivyojaribu kumhudumia alipopatwa na matatizo, eti walimpepea. Jamani, hivi Bunge la Tanzania haina watu wa First Aid ambao wanakaa pale wakati wa mikutano? Hakuna Ambulance? Mwaka 2013, kuna watu walipitia kozi Red Cross, wange saidia! Yaani kubebwa vibaya inaweza kuzidisha ugonjwa au kufanya hali iwe mbaya zaidi.

Serikali inawanunulia magari ya fahari ya bei mbaya! Je, itakuwa shilingi ngapi kuweka watu wa First Aid Bungeni? :A S 39:

Siyo Bungeni tu Bali nchi nzima kila sehemu. Ukipata ajali unakufa kwa hiyo 'first aid' unayopewa na wale waitwao wasamalia wema. Nafikiri ingekuwa vyema masomo yafirst aid yanayotolewa na red cross yakawa ya lazima katika shule za msingi.
 
Hivi Bungeni na sokoni Kariakoo wapi ni mazingira hatari?

Badala ya kutaka ambulance iwekwe standby sokoni Kariakoo wewe unataka iwekwe nje ya vyumba vya mikutano ya wabunge!!! Au kwa sababu wanaopata matatizo ya kiafya ghafla sokoni Kariakoo hawapigwi picha na kuwekwa kwenye blogs?

katika waliopost wote wewe pekee ndo umeandika jambo la maana. hao ni wafilisi wakubwa wataifa hili. wajilipie wenyewe hiyo first aid na sio kodi zetu. ambulences zikakae pale kariakoo.
 
Back
Top Bottom