Bunge: Sasa 'soap-opera' kubwa nchini

Bunge: Sasa 'soap-opera' kubwa nchini

Iga

Senior Member
Joined
Dec 17, 2007
Posts
112
Reaction score
6
YALE yanayooneshwa katika TBC yamefanikiwa kukifanya kipindi laivu cha bunge kuwa 'soap-opera' bora nchini. Hivi sasa, hasa, kukiwa na hoja moto inayompa spika ujeuri na jazba na hali kadhalika 'young turks' wa opposition-Zitto Kabwe na Tundu Lissu bila kumsahau Mh. Kafulila.

Baadhi ya watu wanasema hili ndio angalau robo ya aina ya bunge tunalotaka kuliona au kulisikia.
 
Sina uhakika kama ndivyo tunavyotaka wabunge wetu watende mambo ya nchi kwa namna wanavyofanya sasa.Hata hivyo ni maoni ya kila mmoja wetu binafsi! Hata hivyo mambo kama:
  1. Kulala fofofoooooooo na mpaka kumwaga denda bungeni... Tena kwa mbunge kama Steven Wassira, anayetoka jimbo masikini kabisa Tanzania, Waziri wa Nchi - Ofisi ya Raisi; na wakati huo ndiye kiongozi wa Serikali Bungeni (HAIKUBALIKI)
  2. Kuzodoana, kashfa, kuzomeana na hata matusi ya kiaina - Hivi kweli tumemtuma mbunge pale kumwita mbunge tuliyemchagua kuwa MNAFIKI.
  3. kUPITISHA HOJA BILA MIJADALA YA MAANA NA BAADALA YAKE KWA KUZOMEA TU ndiyooooooooooooo!
  4. Kuchangia hoja za msingi kwa kuonesha namna ambavyo mpango na bajeti ni mbovu lakini anamalizia kwa kuunga mkono hoja kwa 100% na kuwazomea wanaoikataa.
  5. Kupenda na kujitwalia posho bila huruma kwa wasionacho, n.k
  6. Aaaaaghhhhh nimechoka kuorodhesha......
  7. Kung'atuka au kujivua gamba na kujidai unawaonea huruma wapiga kura wakati umeshiriki wizi wa kutupwa na hata hujachangiua lolote kwa maana ya mijadala hai bungeni kwa zaidi ya miaka 18 n.k

Mi sijui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom