Leo Bajeti ya Ofisi ya Rais, imepita! Hata hivyo ilikuwa wazi kwamba ingepita. Ni kupoteza fedha za walipakodi kujadili "Ndiyo". Mnyika,Lisu na wengine wamejitahidi kuondoa Shilingi, kwa hoja nzito ambazo ni za kulisaidia Taifa letu, lakini Wabunge wa CCM ni wengi na kazi yao ni kuimba "Ndiyo". Inavyoelekea hata Hoja ya kuruhusu madawa ya kulevya ikiletwa Bungeni, itapitishwa! Wabunge wetu vijana wa CHADEMA na wale NCCR, wasikate tamaa. Historia inaandikwa na vizazi vijavyo vitaona nani alikuwa mkweli na ni nani alikuwa akitekeleza ya tumbo lake. Bunge letu ni la chama Kimoja, na haliwezi kuleta maendeleo kwa kushangilia "Ndiyo" hata kama ni kuliangamiza taifa. Tafakari!