Bunge kama chombo cha kutunga sheria

samurai

JF-Expert Member
Oct 16, 2010
11,495
24,222
Wadau na wajuzi wamambo naombeni msaada au labda tulijadili hili.

1. hivi inawezekanaje bunge letu tukaliita chombo cha kutunga sheria huku asilimia kubwa ya hao watunga sheria ni darasa la saba na wengine elimu za kuungaunga?.

2. tunalitegemea bunge letu kujadili baadhi ya mikataba tena ya kimataifa huku asilimia kubwa ya hao tunaowategemea ni vilaza.

3. tunalitegemea bunge letu kuisimamia na kuishauri serikali huku asilimia kubwa ya hao wabunge uwezo kiakili na kitaluuma tunaona hauko sawa.

Wadau tujaribu kulijadiri hili kwa kina na mapana ni kweli bunge hili linaweza kututoa hapa? au linyimwe meno na kuwe na think tanks somewhere ambao watasaidia kufikiri na kubuni mbinu mbali mbali za kututoa hapa?
 
Kwa nchi za Kiafrica (labda ukiiondoa Africa Kusini kidogo) sionagi sana kazi za hicho chombo; kinatumikaga kama stamp tu ya serikali.
 
Back
Top Bottom