Bundle za internet zenye gharama nafuu

Hapa unakuta una dakika mpaka unachanganyikiwa,niliangalia nikakuta kama dk 28000 haotel tu halotel plus 1500 mitandao yote.Unapiga tu simu,halotel kiboko kwa hilo.Sio unakutana na sijui jaza sijui..2000 kwa week unapewa dk 60 na MB10(Hizi Mb ukipiga chafya tu ya data zimeisha zote).
 
Dah...

Watu wanaxingua humu.

Mbona hamuonyeshi jinsi ya kujiunga.
 

HABARI,
"Nanoli,
Pole sana kwa hilo jaribu TTCL najua huduma za data hapa kwetu Tanzania zimekuwa kama anasa ila kuna nchi hapa Africa huduma hizo ni rahisi sana,Nashindwa kuelewa kwanini hilo linatokea wakati tuna Fiber cable ila ninatoa ushauri kwa TTCL kuongeza juhudi na kutoa data ya ujazo mkubwa kwa bei rahisi zaidi hilo litawavutia wateja wengi kujiunga nao.Tukaachan na hao wanaotuibia,Unanunua bando la 500MB una download kitu cha 150MB wanakwambia bando limekwisha TCRA mulikeni hilo kunawinzi mkubwa kwenye hii mitandao ya simu.

LUMUMBA
 
Mm niko zangu natumia bidhaa za ndani za kitanzania Ttcl,nina lain ya chuo yaan n full gb maongezi usiseme.ila sasa vocha ndo shughuli kuzipata.
 
Tumia zantel kitu kina kasi mbaya

Line zao zote za sasa ni za chuo.

Sh. 500--- mb 500 wiki
Sh.1500--- 1.5GB wiki
Sh.10000--- 10.5 GB nwezi
Upo Tanzania visiwani Mkuu?, maana Tanzania visiwani ndiko Zantel inapokubali.
Huku Dodoma Zantel haisomi hata mtandao, vocha zenyewe madukani hazipo.
 
Mkuu, toka nianze kutumia Halotel kwa upande Wa Mb na muda Wa maongezi sijawahi kujutia line ya Halotel kiukweli.

Sema tu sina mashabiki wanaotumia Halotel ila huwa najikuta nina zaidi ya dk 29000 Halotel to Halotel na hizi za mitandao yote ndizo ninazofaidi maana nazitumia zenyewe.

Labda wanitibue ndipo nitakapowahama. Ila kwasasa sina mpango Wa kutoka hapa.
 
mi
mie washanitibua nmetupa line yao hao halotel, Gb 6 kwa elfu 10? pumbafu
 
Mm niko zangu natumia bidhaa za ndani za kitanzania Ttcl,nina lain ya chuo yaan n full gb maongezi usiseme.ila sasa vocha ndo shughuli kuzipata.

HABARI
"dullah lakumo burra,
Safi sana ila TTCL wameanza kubadilika ila wanatakiwa kuongeza kasi sana hata hiyo ya matangazo HALOTEL walikuja na wamewapita sasa kuna tatizo hapo ila kwa sasa wanajitahidi waongeze matangazo ya kutosha.

LUMUMBA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…