Bukoba ya leo

Egwugu

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2011
Posts
17,558
Reaction score
8,555
Ni furaha yangu na kwa wote walioweza kuingia mwaka mpya salama lakn pia natoa pole kwa wale wote ambao kwa namna moja ama nyingne wamekutana na vikwazo katika kuumaliza na kuingia mwaka mpya 2012,inshallah Mungu azidi kuwabariki

Ni mda kdogo toka nimepotea hapa jamvini na kikubwa ni kutokana na kuwa safarini Kagera ambako nilipata pia nafasi ya kuhitimisha sikukuu zote mbili za mwisho wa mwaka nikiwa huko,safari yangu hii iliniwezesha kupitia baadhi ya maeneo na mitaa na mambo mengi yakiwemo mazuri bila kuyasahau na mabaya pia katika nyanja mbalmbal za kmaisha kama ifuatavyo

Barabara:Ni jambo la kujivunia kwa wanakagera kwa kuweza kuwa na barabara nzuri na zenye lami kuanzia za kuingia mpaka za mitaani na kwa kiasi kikubwa zikiwa safi
Biashara:Mkoa wa Kagera bado haujafanya vya kutosha katika kuimarisha biashara na kutumia nafasi zilizopo kwa ajiri ya kuwaendeleza wakazi wake,mfano,nimeshangaa kuona mpaka leo hapana kituo cha mabasi chenye hadhi ya kuitwa stand ya mabus kwa maana bado stand ni ndogo na bado ni ya matope,pale kuna connection ya nchi kama 4 na wasafiri wanakutana pale kwenda Uganda,Rwanda,Burundi na hata Kenya..mkoa unahitaji kuliona hili mapema kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Bukoba mjini

Kilimo:katika hili nimevutiwa na kuona wananchi wameamua kuwekeza katika kilimo cha miti ya mbao almaarufu 'mipines',ili linaonekana kuwa pozeo la kupungua kwa uzalishaji wa ndizi na mibuni katika kurekebisha hali ya uchumi na kipato kwa ujumla wananchi sasa wanaona huyu pines ndo mkombozi wao kwa sasa

Habari,Mawasaliano na Burudani:Katika burudani nimependa kuona kuna nyimbo nyingi na nzuri zinazoimbwa na wasanii wa huko na ambazo hazipatikani kwingine bado,hili ni tatzo la kukosa mapromota na wabunifu wa kukuza sanaa,binafsi nimerudi na nyimbo nyingi kias kama atahtaji mtu humu ndani basi anipm,sehemu za kumbi za disco 'night club' bado chache sana japo kdogo zilizopo ni nzuri,nimefurahi kuona kuna vituo vya matangazo 'redio' kama v3 japo naona kuna haja ya kuongeza vingine kama itawezekana pia
 
Mkuu ulifika Linas night club? Ni club ndogo lakini ya kisasa na ukiingia huwezi amini upo BK the way watu wanavyo enjoy! Nimemiss Kuku wa kienyeji wa kuchoma pale Bukoba Club,jamaa wanachoma kuku sijawahi ona! Vp supu nzito ya Sato na ndizi juu kwa 1500 tu! Bukoba ni sehemu nzuri ya kupumzika kwakweli maana nilitoka shavu dodo ndani ya wiki!
 
Hakuna mkoa uliopakana na nchi nyingi kama Kagera tatizo hazijachukuliwa hatua za makusudi ili pawe kitovu cha biashara!
 
Hakuna mkoa uliopakana na nchi nyingi kama Kagera tatizo hazijachukuliwa hatua za makusudi ili pawe kitovu cha biashara!

Ni kweli mkuu nimeweza kuingia pale Linas Night Club siku ya mkesha wa X-mas palikuwa na SumaLee pamoja na akina Wema japo mie nilijichanganya kwenye disco,hapa dar nimebahatika kutembea clubs kama Savanna,Bills na nyingine nyingi lakini ile Linas kusema kweli niliipa ufagio hadi kumpa taharfa mshkaji wangu m1 kwamba 'niko kiwanja kikali sijapata ona ova mamtoni'pako poa kinoma na pembeni yake kuna club nyingne kuna waganda wanacheza nusu uchi hadi dawn

mkuu ni mengi lakini ntamalizia nikja na part2 ya taharifa hii
 
Nakupongeza, vipi kuhusu usafi wa mji kwa ujumla, linganisha na miji kama moshi?
bidhaa zinapatikana madukani kwa bei zipi?

tuambie pia uchangamfu wa watu wanachangamka au kale kaugonjwa bado kana leta zahama mjini?
 

do not judge a book by its cover mkuu.Mkoa wa Kagera una matatizo lukuki sasa wewe umeongelea mjini tu lakini hata mjini mtatatizo mengi.
Mf.sokoni kuchafu saana kwani takataka zinamaliza siku kibao bila kuondolewa.
Mji wa Bk hauna barabara ata moja yenye miti na maua,nyumba nyingi ni za zamani hazifanyiwi ukarabati ata kupaka rangi hamna,bei ya vitu hiko juu kuliko sehemu nyingine mfano mafuta,sukari etc
Rushwa nikama halali hasa maaskari polisi na traffic,vijana wengi hawana kazi maarum,elimu ndo usiseme shule za kata nyingi hazina walimu na vyumba vya maadarasa mf.wanafunzi wakidato cha kwanza wengi wataenda shule mwezi wa nne baada ya january.
Mkuu hii kasumba ya kujisifia hakina nshomire haina nafasi tena wakati matatizo ni chungu nzima.
 

Hapana mkuu sina haja ya kusifia tu na ndo maana nimetangulia kusema nimeyaona mabaya na mazuri na tayari nimefanya kukosoa mfano upande wa biashara nimeweka wazi kuwa bado jitihada ni hafifu na nikagusia ubaya mwingine wa stand ya mabus ilvyokuwa ya matope,si kweli?nakusudia kuelezea ukweli mtupu na kimsingi hapa umeongelea mambo ambayo bado sijayagusia k.v Huduma za jamii, mazingira,usafiri wa maji n.k ambavyo pamoja na mengine vitakuwa kwnye sehemu ya pili ya taharifa hii

Nimekupata mkuu,pamoja sana!
 
watoto wa huko ulifanikisha kuwaonja?
 
mkuu mimi Bukoba club nilikua napapendea ulimi wa kuchoma na sato wa kuchoma we acha tu, linas usiseme bado hujafika q bar nk, nili enjoy sana nilipokuwa huko
 
watoto wa huko ulifanikisha kuwaonja?

Haahaaa!mkuu Chappaa sasa hapa wataka nisielewane na shemejio...kama vp nitafute private tuongee mtu wangu
 
mkuu mimi Bukoba club nilikua napapendea ulimi wa kuchoma na sato wa kuchoma we acha tu, linas usiseme bado hujafika q bar nk, nili enjoy sana nilipokuwa huko
Mkuu kweli sikuwa shabiki wa ulimi lakini jamaa wa Bukoba club ni mabingwa wa ulimi wa kuchoma! Ukitaka samaki wa kuchoma aliye hai kabisa unaenda baa moja inaitwa Yasila iko ufukweni kabisa,unalamba samaki wa kuchoma fresh from water!! Pale Q club kuna totoz za Kiganda zimejitoa akili kabisaaa! Inaweza wekwa nyimbo ya Beyonce inavyochezwa sasa! Mbaya zaidi wanachojoa mpaka nguo! Kuna RPC aliwapiga marufuku wamiliki kuleta hao waganda cha kushangaza vijana wa mjini wakamaindi ile mbaya! Nasikia waganda bado wanakuja kama kawa! Mji mdogo lakini una mambo ule!
 
mkuu mimi Bukoba club nilikua napapendea ulimi wa kuchoma na sato wa kuchoma we acha tu, linas usiseme bado hujafika q bar nk, nili enjoy sana nilipokuwa huko

Mkuu sato ndo supu maalum sana pale mjini na ukipata sehemu inatengezwa kwa ustadi unaweza kushangaa unachonga mtumbwi wako na ww,vyakula viko chini sana hata huku mahotelini pia bei siyo tight sana khvyo...utaenjoy sana!
 
watoto wa huko ulifanikisha kuwaonja?

Haahaaa!mkuu Chappaa sasa hapa wataka nisielewane na shemejio...kama vp nitafute private tuongee mtu wangu
 

Umenikumbusha Q club mzazi,pale kuna totozi za kiganda znatema sumu kwa kganda alafu wazuri kinyama...mara 'eisanyu lyawe',mara 'nkwagala nyo sebo' mara 'wanji' duuh!...ule mji ni mtamu mda wa ucku wkenda waweza kuchizi na mambo yake mazee
 
kuhusu nyimbo kwakweli tunaazina ya kutosha kuna wasanii kama 'nshomile kwakweli ni gumzo..tena balaa tena ni hipo hop like..kuna shemela n.k nawapenda sana hawa jamaa..mipaini imepandwa kwa kasi sana huko bukoba labda kuliko sehemu yoyote hap tz..kuhusu radio station niliziacha mbili za bukoba mjini yaani kasibante na vision na kule karagwe mbili ambazo ni FADEKO na karagwe fm..
 
watoto wa huko ulifanikisha kuwaonja?

Haahaaa!mkuu Chappaa sasa hapa wataka nisielewane na shemejio...kama vp nitafute private tuongee mtu wangu
 
Kilimo cha migomba na kahawa kmeanza kusongwa sana make nimekuta kuna ugonjwa unaitwa 'mnyauko' kwa kiasi kikubwa unaharibu sana uchumi wa hawa watu

Kweli pia suala la redio nimezisikia na kwa kweli naamini zitawasaidia kutoa na kupokea taharifa mbalimbali ambazo zitachochea maendeleo,mfano nimeenda vijijini nikawakuta watoto wanaweza kuongea kiswahili walau sentensi mbili tofauti na wakati wa enzi zetu

Nimeongelea barabara za kuingia na kutoka hata za mjini zote ni lami tofauti na maeneo mengine kama Tabora,Singda n.k,ambazo hata lami hazina

Biashara siyo kubwa sana isitoshe ya usafirishaji kwani malori makubwa ni machache kdogo bukoba tofauti na sehemu kama Tanga,moshi n.k,sasa sielewi ni meli ama viwanda bado havipo vya kutosha kuchochea usafirishaji
 
safi sana mkuu,je vipi uwanja wa ndege,sukari ya mgao!

Nilibahatika kukiona kiwanja cha ndege kwa mbali kdogo ila bado upanuzi unaendelea na ukizingatia kitarudi nyuma hata kufanya maeneo ya zamzam kubomolewa pia..tatzo naloliona ni sehemu yenyewe kuwa ndogo na kama ni kwa baadae panahtajika sehemu tofauti ambayo itakuwa pana zaidi hata kama ni nje ya mji kama ilvyo ilemela-Mwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…