GE2025 Brenda, Magere wa CHADEMA waachiliwa kwa dhamana

GE2025 Brenda, Magere wa CHADEMA waachiliwa kwa dhamana

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Elias Msuya

Senior Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
173
Reaction score
671
255b07af-50c7-41e8-bd83-0e5707bf0a79.jpg

DAR. Mkurugenzi wetu wa Mawasiliano na Uenezi, Brenda Rupia, pamoja na Mtaalamu wa Rasilimali, Miradi na Uwekezaji Leonard Magere, wameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi na wametakiwa wametakiwa kuripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi kati, Dar es Salaam, kesho Julai 16, 2025.

Soma pia: Brenda Rupia akamatwa na Polisi

Brenda alikamatwa Julai 12, 2025 akiwa katika mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea nchini Kenya na baadae alitegemea kusafiri kulekea nchini Ujerumani, wakati Magere naye alikamatwa siku hiyo hiyo katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) akielekea nchini Uingereza.

Soma pia: Polisi wakiri kumshikilia Magere

Taarifa iliyotolewa na CHADEMA leo Julai 15, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Diaspora, John Kitoka imesema chama hicho kinafuatilia kwa karibu mwenendo wa jambo hilo wakitaka haki, uwazi katika mchakato mzima.

“Tunaishukuru jamii ya Watanzania, wanachama na wapenzi wa Chadema kwa mshikamano na uungwaji mkono mnaoendelea kuonyesha katika kipindi hiki kigumu.”
 
View attachment 3406835
DAR. Mkurugenzi wetu wa Mawasiliano na Uenezi, Brenda Rupia, pamoja na Mtaalamu wa Rasilimali, Miradi na Uwekezaji Leonard Magere, wameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi na wametakiwa wametakiwa kuripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi kati, Dar es Salaam, kesho Julai 16, 2025.

Soma pia: Brenda Rupia akamatwa na Polisi
Brenda alikamatwa Julai 12, 2025 akiwa katika mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea nchini Kenya na baadae alitegemea kusafiri kulekea nchini Ujerumani, wakati Magere naye alikamatwa siku hiyo hiyo katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) akielekea nchini Uingereza.
Soma pia: Polisi wakiri kumshikilia Magere

Taarifa iliyotolewa na CHADEMA leo Julai 15, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Diaspora, John Kitoka imesema chama hicho kinafuatilia kwa karibu mwenendo wa jambo hilo wakitaka haki, uwazi katika mchakato mzima.

“Tunaishukuru jamii ya Watanzania, wanachama na wapenzi wa Chadema kwa mshikamano na uungwaji mkono mnaoendelea kuonyesha katika kipindi hiki kigumu.”
Hawajawafanya ya Atuhaile na Boniface

Boniface Mwangi, Agather Atuhaire: We were sexually assaulted by Tanzanian captors​


1752586482913.png
 
Back
Top Bottom