Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,754
Eti akina Rage(Mwizi na Tapeli) ndio watu wa mpira.....Mtu wa mpira alikuwa Hassan Dallali,unakumbuka Simba walibeba ubingwa bila hata kupoteza mechi na wakati ule Yanga alikuwa mteja wa Simba.Tangu waje hao watu wa mpira (Rage na wenzie) wamefanya nini la maana baada ya kuona Yanga wamemuajiri Timbe na wao wakamuajiri Bassena .Yanga walivyomtimua Timbe na kurudisha Papic na wao wakamrudisha Milovan
Tatizo Simba wanaigaiga sana....Yanga walivyorudisha Papic eti nao wakamtimua Basena na kumrudisha Milovan.....Halafu walivyokuwa dhulumati wakamdhurumu Basena fedha zake zote za kuvunja mkataba kwa kisingizio hana cheti(ina maana walikuwa wakimtumia wakijua ni kanjanja?).....