Bravo Juma Msuya wa TANESCO Makao Makuu, asante JamiiForums

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
Habari tena wadau wa JF,

Nilitaka nitoe uzi uhuu, kama mrejesho kwa ule nilioutoa asubuhi ya leo kuhusu Tanesco Mkuranga baada ya kuomba mwenye namba ya mtumishi yeyote wa Takukuru ili anipe pesa zao nikatumbue jipu pale Tanesco Mkuranga.

Ndani ya masaa mawili tu nimepokea simu kutoka kwa Mtu wa Tanesco aliyetambulisha kama Juma Msuya wa Tanesco makao makuu, ameniomba radhi kwa kuchelewa kuunganishia umeme, na ameiahidi kulishugulikia tatizo ili kwa umakini.

Kwa kweli nimefarijika sana, kuona simu ya huyu kijana zaidi nimefarijika alivyoniomba radhi, na kuniambia kuwa si watumishi wote wa Tanesco wana tabia hizo, nami nakiri kabisa kuwa hapo si wote ila pale Mkuranga kuna tatzo kubwa sana, Meneja Tanesco Mkuranga anafanya kazi kwa mazoea sana.

Zaidi, naendelea kumpongeza huyu kijana kwa utendaji wake uliotukuka, ninaahidi ushirikiano mkubwa sana ili kuhakikisha watendaji wa namna hii wanaacha kulichafua shirika la umma, na kulipotezea fedha kwani kitendo cha mteja kulipia umeme, halafu haunganishiwi umeme kinasababishia shirika kukosa mapato kwa mwezi.

Natanguliza shukurani kwa uongozi wa JF (JamiiForums), uliowezesha sauti yangu kusikika panapo husika, lakini pia nitumie fursa hii kuwaasa watumishi wengine wa umma, kuwa mnaposoma taarifa hapa JF, zifanyieni kazi kama walivyofanya hawa Tanesco kwani wamekosa nini?

Wamenipigia simu, na nilichowaambia ndicho walichokuta kwenye mtandao wao, pili wameshauri nichukue hatua za kuvihusisha vyombo vya usalama katika kuhakikisha haki inatendeka.

Mimi nitumie fursa hii, kuwashukuru Tanesco makao Mkauu hata kama sijapata huduma yao, kitendo cha kunipigia simu kimenitia hamasa kuwa kweli ni watu walio tayari kusikiliza maoni ya watu.

Meneja Tanesco mkoa wa pwani hana budi, kueleza kurugenzi ya utawala makao makuu anaupungufu wa nini mpaka haicheleweshe serikali kuingiza fedha, jiulize kam angeungansha umeme miezi miwili iliyopita je serikali ingekuwa imeingiza shilingi ngapi kupitia kununua luku?

Pia nitumie fursa hii, kumtaka Juma Msuya anilinde maana hao vijana wakijua kuwa nimewasemea wanaweza unganisha ovyo umeme na kuniletea shida badae, kama wakiweza baada ya kuunganisha umeme waniruhusu nilete private technician ili akague, ndo wauwashe.

Kila la heri Msuya kwa kazi njema nadhani vijana kama nyinyi ndio tunao wahitaji katika ujenzi wa taifa. Maana staki niamini kuwa meneja wa Mkuranga, hakuona uzi wangu, atakuwa ameuona, ila amedharau kama ambavyo amekuwa akijibu kuwa watakuja ila hajali, wala hafanyii kazi anachokisema.

Sina ugomvi na meneja huyo ila anahitajika kutumikia umma kwa kujua kuwa yeye ni mtumishi wa umma na si bosi wa umma, analipwa na kodi zetu iweje asitutumikie kwa wakati?

Asante Kijana uliyenipigia simu kutoka Tanesco makao makuu.
 
huyo meneja wa hapo mkuranga atimuliwe tu hayo ndio majipu tatizo mkurugenzi wa tanesco ni mlokole mpole sana ndio maana wanamchezea
 
Pole sana na hongera kwa kufanikiwa.

Mi nimelipia kuunganishwa na huduma hii kijijini kwangu toka mwezi wa pili mpaka sasa sijaona hata fundi au gari likikatiza mtaani kwangu..

Cha kunistaajabisha zaidi nimelipia nguzo moja ili umeme ufike nyumbani wakati nyumba ipo katikati ya nguzo mbili yaani kulia na kushoto. Niliuliza nikaambiwa walikosea wakati wa kuweka nguzo! Je, kosa la Tanesco kwanini aumizwe mteja?

Tanesco wilaya ya Mwanga na nyie ni Tambazi.
 
Nahisi kama chezo flani hapa!!!!!! Huyo msuya ukute ana ID mbili sasa anajipigia promo, maana haiingii akilini akubali uje kumsifia humu wakati punde ulikuwa na shida inamaana umetengeneza mwenyewe hii kitu. Najua watu kwa serikali hii wanaipelekesha ili wapate sifa tu.
 
nataman na wewe ndugu yangu usaidiwe ebu kama huyo kijana aliyenipigia sm, kama unaweza soma hapa weka no yako ili watu, wakupigie uwasaidie kama ulivyonisaidia mimi.
 
Nahisi kama chezo flani hapa!!!!!! Huyo msuya ukute ana ID mbili sasa anajipigia promo, maana haiingii akilini akubali uje kumsifia humu wakati punde ulikuwa na shida inamaana umetengeneza mwenyewe hii kitu. Najua watu kwa serikali hii wanaipelekesha ili wapate sifa tu.
Bondpost, si kira andiko ni la kukiritisaiz , kama huna la kuandika basi unaweza soma na ukapotezea, ndugu mimi ni mwananchi wa kawaida, kama una akili timamu soma uzi, na uelewe, mimi natumia sifieleo wara huyo kijana hajaja hapa, JF, mimi nimetupia uzi, na yeye hakunijibu kupitia hapa, amenipigia sim yangu ya mkononi, na kunisikiliza, mbona watu mnakuwa na negative mind mda wte? ninaaza kuamini kuwa mimba zote zinazotungwa usiku, hata kma mtoto akizaliwa mchana, basi anakuwa na negative mind kwa kira jambo, binafsi naendelea kumpongeza huyo kijana hata kama Tanesco hawajaja, ila najua na nina amini maneno yake, kuwa watakuja kuliko maneno ya meneja wa mkuranga ambae amekuwa akinimbia watakuja, uku siku zikizid enda, yani mkuranga mpaka kongowe, ni karbu sana , yani utendanji huu ni sawa wa ule wa MSD, dawa kutoka keko mpka mhimbili kwa mwaka mmoja bira kufika mhimbili.Bravo Msuya hata wasemeje ukweli utabaki kama ulivyo , hunijui sikujui wara hatujuani. tenda kazi.
 
Wewe nawe ujielewi sasa una mpongeza kwa kukupigia simu iyo ni kazi yao kma customer care nipe namba yako nikubeep unipongezi
 
Namimi nampongeza huyo kijana? kwanini meneja Wa mkuranga hakuchukua HATUA? Au alikuwa anatengeneza mazingira ya Rushwa?
 
Wewe nawe ujielewi sasa una mpongeza kwa kukupigia simu iyo ni kazi yao kma customer care nipe namba yako nikubeep unipongezi
unaitwa nani? nakuja tena? usije tena, koma wewe domo chafu hivyo ukija tena utakuja na ualo, naisi wewe utakuwa vijana wa Lumumba, mtu akitenda jema mpongeze paka shume wewe.
 
Wewe ni great thinker !! Hyo post ya huyu jamaa ya asubh sikuiona, naomba kuuliza hivi aliweka namba yake ya simu? Au jf ndio waliomtafuta ? Siyo ugomvi ila mleta Uzi tufahamishe tujue vema
Nahisi kama chezo flani hapa!!!!!! Huyo msuya ukute ana ID mbili sasa anajipigia promo, maana haiingii akilini akubali uje kumsifia humu wakati punde ulikuwa na shida inamaana umetengeneza mwenyewe hii kitu. Najua watu kwa serikali hii wanaipelekesha ili wapate sifa tu.
 
Mkuu asubh namba yako ya simu uliiweka katika Uzi wako? Halafu mkuu una hakika gani kama huyu Msuya ni mtumishi wa Tanesco? Kama umechezewa mchezo na muhuni Fulani tu? Kwanini usingesubiri vitendo kwanza ndio uje umsifie kiasi hichi.

Mimi nahisi una visa tu na meneja wa Tanesco mkuranga
Bondpost, si kira andiko ni la kukiritisaiz , kama huna la kuandika basi unaweza soma na ukapotezea, ndugu mimi ni mwananchi wa kawaida, kama una akili timamu soma uzi, na uelewe, mimi natumia sifieleo wara huyo kijana hajaja hapa, JF, mimi nimetupia uzi, na yeye hakunijibu kupitia hapa, amenipigia sim yangu ya mkononi, na kunisikiliza, mbona watu mnakuwa na negative mind mda wte? ninaaza kuamini kuwa mimba zote zinazotungwa usiku, hata kma mtoto akizaliwa mchana, basi anakuwa na negative mind kwa kira jambo, binafsi naendelea kumpongeza huyo kijana hata kama Tanesco hawajaja, ila najua na nina amini maneno yake, kuwa watakuja kuliko maneno ya meneja wa mkuranga ambae amekuwa akinimbia watakuja, uku siku zikizid enda, yani mkuranga mpaka kongowe, ni karbu sana , yani utendanji huu ni sawa wa ule wa MSD, dawa kutoka keko mpka mhimbili kwa mwaka mmoja bira kufika mhimbili.Bravo Msuya hata wasemeje ukweli utabaki kama ulivyo , hunijui sikujui wara hatujuani. tenda kazi.
 
Acha matusi wewe Binti, jibu maswali unayoulizwa. Halaf jifunze kiswahili, sijui umetoka Geita Jana.
unaitwa nani? nakuja tena? usije tena, koma wewe domo chafu hivyo ukija tena utakuja na ualo, naisi wewe utakuwa vijana wa Lumumba, mtu akitenda jema mpongeze paka shume wewe.
 
Acha matusi wewe Binti, jibu maswali unayoulizwa. Halaf jifunze kiswahili, sijui umetoka Geita Jana.
ebooo! nimekuwa binti tena? jiheshim kijana kusoma hjui hata pc ouni kwenye avator, angalia kijana kama wewe ni miongoni mwa waume wa dar sema sisi wakurya hatuchagui tunawatemebezea mkoko tu.
 
Kwenye avatar naona pic ya mc mreembo. Kumbe ndio wewe ? Si bure umeamua kumsifia Msuya humu.
Fine mkuu, turudi kwenye hoja sasa, jibu maswali yetu basi
ebooo! nimekuwa binti tena? jiheshim kijana kusoma hjui hata pc ouni kwenye avator, angalia kijana kama wewe ni miongoni mwa waume wa dar sema sisi wakurya hatuchagui tunawatemebezea mkoko tu.
 
Hongera... Leo umepigiwa simu na mangi Juma? Of coz huyu jamaa ni mtu mzuri sana na msomi mwenye shahada ya uzamili anayezijua vizuri 'hujuma' za wateja... Natumai hawa ndio watakuwa viongozi bora wa shirika wa baadaye...

Mangi.jpg
 
Accused, hujaelewa nini mbona uzi wangu upo very clear, niliweka uzi leo asubuhi na kuomba mwana jf yyte anipe no ya mfanya kazi yyte wa takukuru wilaya mkuranga ili wanipe fedha zao niende nikawape watumishi watanesco ofisi zile, katika uzi wangu niliomba mwenye uwezekano anitumie kwenye no yangu ya sim ndani ya masaaa mawili anilipigia hyo kijana nadhani unalingana nae wewe, mimi ni naweza kuwa babako kijna wangu usione tunawsiliana kama wte ni makinda, akanitaka radhi kwa kire nilicho kitaka kukifanya na kuniambia nisirudi nyuma huyo kijana akaniadi kunisaidia kutimiza wajibu wake kuakikisha kuwa napata umeme wiki inayoanza kesho. nini nimeksea kijana wangu Accused bahati nzuri ninakujua? nampongeza huyu kijana sana sana, kwa kire alicho kifanya na kama ni huyo aliyewekwa hapo juu kweny pc, basi mungu akubariki kijana wangu, nmesikitika unaniambia mimi ni MC Mrembo baba yako ananiheshimu sana nashangaa wewe kijana hunieshimu hivi hujui kwa nini nimesema mimba za kutungwa usiku zina kuwaga na negative mind all the time? i know you. bye
 
Inawezekana una ugomvi na meneja wa TANESCO Mkuranga.

Wale jamaa ni wachapa kazi. Mimi waliniunganishia umeme sehemu mbili tofauti na tena ni umeme mkubwa na hawakuniomba hata senti tano.

Zamu yako ikifika wanakuunganishia bila matatizo yoyote.
 
Back
Top Bottom