Boti zazama Jibuti

Boti zazama Jibuti

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,618
Reaction score
9,607
Zaidi ya watu 130 hawajulikani walipo huku maiti 5 zikiokolewa baada ya boti mbili kuzama Bahari ya Sham
Boti mbili za wahamiaji haramu zazama baharini nchini Jibuti
Wahamiaji haramu 5 wamepotez maisha na wengine 130 hawajulikani walipo baada ya boti 2 walizokuwa wakisafiria nazo kuzama katika bahari ya shamu nchini Jibut.

Kwa mujibu wa taarifa ya maandishi iliyotolewa na shirika la wakimbizi la kimataifa (IOM), Ajali hiyo ilitokea jana asubuhi kaskazini mashariki mwa nchi hio katika eneo la Obock katika mkondo bahari wa Godorya.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo wakaazi wa eneo hilo walitoa taarifa hizo za kuzama kwa boti hizo polisi, timu za uokoaji za polisi ziliokoa watu 2, ziliokoa pia maiti 3 za wanawake na 2 za wanaume.

Imefahamishwa kwamba kwa uchache wahamiaji 130 hawajulikani walipo kutokana na ajali hiyo.

Kwa mujibu wa habari za ndani boti hizo zilikumbwa na dhoruba na kuzama kutokana na kuzidisha uzito.

Moja katika watu waliookolewa wakiwa hai katika dhoruba hiyo kijana mwene miaka 18, alisema katika moja ya boti hizo zilizozama walikuwamo watu 130. Hakufahamu boti nyingine ilikuwa na watu wangapi. Kijana huyo jina lake halikutajwa.

TRT
 
Pole yao!!
Kwanini wahamiaji haramu hawaishi na kila siku wanakufa?Je ni Africa ndio hakukaliki au Ulaya ndio inaokekana kuna nafuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole yao!!
Kwanini wahamiaji haramu hawaishi na kila siku wanakufa?Je ni Africa ndio hakukaliki au Ulaya ndio inaokekana kuna nafuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wengine wanazamishwa makusudi na wazungu..... hawa wahamiaji wajinga kweli hawajui hayo maisha mazuri wanayo yakimbilia yalijengwa na wazungu kwa jasho na damu sasa sisi waafrica badala ya kuijenga Africa tuwe kama wao sisi tunakimbilia nchi zetu
 
Back
Top Bottom