Miss Halima
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 221
- 487
Baada ya kukaa mahabusu kwa siku 1,324, hatimaye Mkurugenzi wa Kampuni ya Jatu Public Limited Company (PLC), Peter Gesaya, ameachiwa huru katika kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Gesaya na wenzake wanne, Nicholaus Fuime, Esther Kiya, Mariam Mrutu pamoja na Kampuni ya Jatu PLC wameachiwa baada ya kumalizana na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa utaratibu wa kisheria wa majadiliano na kufikia makubaliano ya plea bargaining ya namna ya kumaliza kesi hiyo.
Gesaya alikaa mahabusu kuanzia Disemba 29, 2022 hadi Agosti 14, 2026, siku ya Ijumaa ambapo aliachiwa pamoja na wenzake hao.
Gesaya na wenzake hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Disemba 29, 2022 na tangu wakati huo walikuwa wakishikiliwa mahabusu hadi walipoachiwa jana.
Soma Pia: Mkurugenzi wa JATU PLC aendelea kusota Gerezani kwa zaidi ya siku 690
Wakati Gesaya na wenzake hao wakimalizana na DPP na kumaliza kesi dhidi yao kwa utaratibu huo, Washtakiwa wengine watatu, Habiba Magero, Mariam Kusaja na Lucy Izengo, wataendelea na kesi yao ambayo imepangwa kutajwa Agosti 20, 2026.
Gesaya na wenzake wanne, Nicholaus Fuime, Esther Kiya, Mariam Mrutu pamoja na Kampuni ya Jatu PLC wameachiwa baada ya kumalizana na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa utaratibu wa kisheria wa majadiliano na kufikia makubaliano ya plea bargaining ya namna ya kumaliza kesi hiyo.
Gesaya alikaa mahabusu kuanzia Disemba 29, 2022 hadi Agosti 14, 2026, siku ya Ijumaa ambapo aliachiwa pamoja na wenzake hao.
Gesaya na wenzake hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Disemba 29, 2022 na tangu wakati huo walikuwa wakishikiliwa mahabusu hadi walipoachiwa jana.
Soma Pia: Mkurugenzi wa JATU PLC aendelea kusota Gerezani kwa zaidi ya siku 690
Wakati Gesaya na wenzake hao wakimalizana na DPP na kumaliza kesi dhidi yao kwa utaratibu huo, Washtakiwa wengine watatu, Habiba Magero, Mariam Kusaja na Lucy Izengo, wataendelea na kesi yao ambayo imepangwa kutajwa Agosti 20, 2026.