Bora kufa kuliko hivi!

Mkuu kwanza badilisha hiyo title ya thread yako, nothing is worth dying for except your own freedom. Ukishabadilisha title nitarudi nikupe ushauri.
 
shukuru kwa kujua mapema kabla ya kitanzi ndoa, ndoa za mikataba na zije
 
usife ndugu yangu wanawake ni kama siti ya gari ukikosa siti namba moja utakaa siti namba mbili,hivyo ushukuru mungu kuwa hujapata nafasi ya kumwoa na ikiwezekana nenda kapime VVU na baada ya hapo mpime mtoto DNA kisha tulia kwa mda bila kuwa na mpenzi ili uweze kufanya maamuzi sahihi

mambo ya kufa achana nayo,kila kitu kitokeacho hapa duniani kina maana yake,kuna kitu umeepushiwa mkuu
 
bora nusu shari kuliko shari kamili afadhali umeyajua mapema kuliko ungekuja yajua siku kadhaa after kufunga ndoa. ndiyo dunia usilalamike sana kwani matatizo yameumbwa kwa ajili yetu sisi wanadamu na inabidi tuyachukue kama yalivyo.
piga moyo konde maisha uyashinde kwani we ukiendelea kuwaza sana utapoteza muelekeo wa maisha na afya yako kwa ujumla wakati mwenzako anazidi kula raha tu. just let it go stand up na uchukue uamuzi mgumu wa kusonga mbele ili baadaye aje kutambua kwamba you can make it on your own and love goes on but remember what goes around comes around.
 
Huyo wala ha deserve kuwa na wewe. Mwache atange na dunia. Nachoona huruma ni mwanao kuwa na such a mother. Anyway there is a beautiful and faithful girl out there waiting for you! Wanawake wengi sana nina amini with your experience now you will make informed decision next time.
 
unajua wanawake walio wengi ni wapumbavu sana hawajui kama midume huwa inawatamani kwa sababu wapo kwa mtu fulani(mme),akishatoka kwa mme wake kama huyo wako na njemba huwa zianaingia mitini,shenzi zake huyo coz wamewatia aibu hadi familia yake ambayo haisikii kabsa kwa upuuzi wake ,shenzi kbsa.cha kufanya bro unatakiwa utulize akili ikiwezekana chukua hata likizo ukapumzike kijijini for my be 1mnth,utarudi na akili mpya na usifanye haraka kutafuta mwingine.
 

...e bana hebu acha kuulilia mlango uliofungwa nyuma yako, mbele yako kuna milango na madirisha ya kutokea.
piga moyo konde, maisha yaendelee.... unatamani kufa, nani atamlea mwanao?
mwanao amekukosea nini mpaka umkoseshe baba kwa maisha yake yote hapa duniani?

kwani tangu umezaliwa uliahidiwa mwanamke huyo huyo tu ndio utayekuja kumuoa?
hebu jifikirie huyo mwanamke umekutana nae lini maishani?
hivi wewe, humpendi mtu mwingine yeyote duniani zaidi ya huyo mwanamke kiasi kwamba maisha
hayana tena thamani bila yeye?

wake up man!...unatamani kufa? kuna wenzio wapo mahututi mahospitalini wanatamani uzima uliokuwa nao...
haya, piga moyo konde maisha yaendeleee....achana na ndoto za 'alinacha!'
 
Pole sana . Likuepukalo una heri nalo.
 

Wacha kujuta rafiki, wala usiumwe. Mshukuru Mungu umegundua hivyo kabla ya ndoa. Huyo ni hakufahi na hata asingeweza kuwa mwaminifu ndani ya ndoa. Msahau, Muombe Mungu utapata wa ukweli.
 
Asanteni sana kwa ushauri wenu mzuri. Kwa kweli mmenitia moyo hata baada ya kula lunch nimekaa nikatafari ushauri wenu roho yangu imetulia kidogo.
 
Halafu umenikwaza sana yaan ukawaona wanatoka gest ukawaacha bila kuwajeruhi angalau kidogo tu. Mura unatakiwa kuwa serious damu ingemwagika hata kidogo usingetaman kufa. But anyway waungwana wanasema mke mwema hutoka kwa Mungu, so huyo hakuwa mwema kwako, keep waiting utampata atakayekufaa.
 
We nawe ufe wakati umeepushwa na matatizo???

Sema asante Mungu and move on!
 
Kwanza unabahati ya mtende umeshtukia MUVI mapema!Pili acha kutamani kufa sababu ya mwanamke,,,there are millions of women in this world.Anza upya,,yape nafasi maisha yaendelee,,pole sana,
 
huu ushauri utaleta hasara kwa mtoto acha tu mlee dogo coz shetani ni mama yake sio dogo.

mimi nadhani hapo ndio italeta hali ya kutokuwepo na upendo, bora kufanya DNA hii itamsaidia kuwa moto au baridi. Sioni hatari ya kumlea mtoto asiyekuwa wako lkn pia akiwa anafahamu kuwa ni damu yake itapendeza zaidi.
 
Bora kufa? Mbona unamkufuru Mungu wako aliekupa uhai na kukuepusha na matatizo? Yaani ufe kwa ajili ya raha za mwingine? Kwani we haustahili mwanamke mzuri zaidi ya huyo mwenye tabia mbaya? Kabla hujawaza kufa ulifikiria adhabu ambayo ungemuachia mwanao? Piga magoti na umshukuru Muumba wako!
 
maisha yalivo matamu hivo. sipati picha kuna mtu anataka kufa sababu ya nonino
halafu hata haina thamani ya kuifia
 
Kuna haja gani ya kuoa kama mambo yenyewe ndo haya? Ndo maana mimi huwa naamua kuwachinja tu then nakaa zangu kando.
 
pole ila ya kawaida hayo siku hizi ndugu ila mshukuru mungu sana
 
Pole sana mkuu hata hivyo ni bora ulivyojua mapema. Ingekuwa vipi hilo dudu kama lingekuja kukutema siku ya harusi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…