Bomani Committee hiding the truth?

Ripoti ya Tume imewasilishwa bungeni. Therefore it is public. Please note that the summary I posted is the unofficial version of a popularised summary of the report. It is NOT the full report. The final popular version (with cartoons) will be posted on www.policyforum.or.tz some time next week.
 
Sheria mpya ya madini kuanza kutumika ramsi Aprili mwakani
Na Kizitto Noya

WAZIRI wa Nishati na Madini William Ngeleja amesema sheria mpya ya madini itakamilika na kuanza rasmi kutumika Aprili mwakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri Ngeleja alisema kwa sasa izara yake inakamilisha sera ya sheria hiyo kabla ya kutengeneza muswada na kuufikisha bungeni kwa ajili ya kutungwa sheria.

"Bado tuko katika mchakato wa kukamilisha sera, lakini ni mategemeo yetu kwamba zoezi hili tutalikamilisha mwishoni mwa mwaka huu na sheria nyenyewe iwe tayari ifikapo Aprili mwakani,"alisema.

Waziri Ngeleja alisema hayo alipokuwa akijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari aliowaita ofisini kwake kuzungumzia hatma ya mgodi wa almasi wa Williamson Limited (Mwadui).

Alisema katika sheria hiyo mpya, serikali inapitia vipengele mbalimbali kuhakikisha haiwabani kukindi cha watu na kuwapa unafuu wengine bali iwe ni sheria inayojali maslahi ya taifa kwa kuhakikisha matumizi ya rasilimali zake yanakuwa kwa faida ya wananchi.

Maandalizi ya sheria hiyo mpya ya madini yametokana na kazi ya kamati aliyoiunda Rais Jakaya Kikwete Novemba 12 mwaka jana kupitia mikataba yote ya madini na kupendekeza maboresho ili rasilimali hiyo ya taifa ivunwe kwa manufaa ya nchi.

Rais Kikwete aliiagiza kamati hiyo iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta ya madini na kupitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali.

Kamati hiyo ambayo awali ilitakiwa kukamilisha kazi hiyo ndani ya miezi mitatu, ilikuwa na jukumu la kukutana na taasisi zinazosimamia madini na wadau wengine, kupitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zitakazohusu migodi mikubwa nchini.

Mbali na Jaji Bomani, wajumbe wengine walioteuliwa katika kamati hiyo ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe na Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo.

Wajumbe wengine ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Rais pia alimteua Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWater Coopers, David Tarimo ambaye ni mtaalam wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo kushirikiana na wenzao hao katika kazi hiyo.

Kuundwa kwa Kamati hiyo kunafuatia hoja binafsi ya Zitto Kabwe aliyoitoa bungeni kutaka kuundwa kwa Kamati Teule yakuchunguza mazingira ya kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi huko Uingereza na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi Februari mwaka huu.

Baada ya kuwasilisha hoja hiyo, Kabwe alifungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi hapo Januari mwakani. Hatua hiyo ya Bunge iliibua mjadala mkubwa miongoni mwa makundi mbalimbali wakihoji sababu za kumfungia mbunge huyo kijana. Hivi karibuni wakati Rais Kikwete akihutubia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi katika Ukumbi wa Kizota , mjini Dodoma aliahidi kuunda kamati hiyo itakayojumuisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuangalia mikataba mipya ya madini.
Tuma maoni kwa Mhariri
Facebook
 
Yaani Waziri anaconfirm kabisa kwamba bunge la Tanzania ni rubber stamp, hivi wabunge wanajisikiaje wakisoma maneno kama haya.


Anaongea kama it is a foregone conclusion sio tu kwamba itapita bungeni, bali anayo mpaka timeframe kwamba itakuwa tayari kutumika by April.

This is another jewel in our supposedly checking and balancing high drama.

Hakuna hata kuwastahi wabunge kwa kusema "tunatarajia" or any of that sensitivity nonsense, the bunge is out b.i and it will pass this shy by April, full stop. And this is a direct quote, so no "lost in translation" excuse.

Circuses without bread!
 
Walikuwa wanasubiri wakubwa waipitie kwanza hiy sheria kuona kama inawafaa kwa matumizi yao
 

Wabunge wanajisikia poa tu walichofuata bungeni ni posho na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. As long as bunge ni la chama kimoja litabaki kuwa mchezo wa kuigiza tu. Wanavuta vuta muda waendelee kula vi ten percent vyao, Ikifika mwaka wa uchaguzi ndio wa take action. Swali la kujiuliza ni Watanzania tunajisikiaje kudanganyika kila mwaka?


.
 
wabunge wanatakiwa kumtaka Waziri aombe msamaha kwa kauli yake hiyo iliyo presumptive, na angalau atoe statement kwamba hiyo ni projection inayotegemea kama bunge itaupitisha muswada kuwa sheria.

Otherwise watakuwa wamekubali kwamba wao ni rubber stamp, and this include the opposition.
 
Waziri wa Nishati na Madini, Mh. William Ngeleja alitamka hapo October 2009 mbele ya waandishi wa habari kuwa sheria mpya ya madini itakamilika na itaanza kutumika April mwaka huu, 2010. Kama ilivyokawaida ya viongozi wetu kutamka mambo wakiwa na uhakika (kwa mambo ambayo hayajapitishwa kisheria - hata kama); Mh. Ngeleja alitamka hayo akiwa na uhakika kwamba sheria itapitishwa na Bunge, jambo lililo jema kwa matarajio ya wengi wetu.

Sasa kwa vile mwezi Aprili hauko mbali, na ili kujaribu kuepuka 'korogo' jingine Bungeni kama ilivyotokea kwenye muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa uliowakilishwa na Mh. Sophia Simba hivi karibuni; kwa walio karibu na mabadiliko tutarajiayo katika kulinufaisha Taifa letu, tafadhali tusaidieni kujibu swali moja la msingi - Je, ni asilimia ngapi Watanzania tutanufaika nayo kutoka kwenye uchimbaji wa madini unaofanywa na kampuni za kigeni?


Steve Dii
 
Hii ripoti ya Jaji Bomani Haikufanyiwa kazi
 
Aliwahi kusema Rais Ali Hassan Mwinyi - Ruksa : Tanzania ni kichwa cha Mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa. That is what I said insanity is just doing the same thing over and over again expecting different results. Hiyo tume ingekuwa ya Bunge au ya Kimahakama ingekuwa na independence na ingepaswa kutoa findings hadharani! Kwa kuwa hiyo Kamati imetokana na utashi at he pleasure of the president it has to dance to his tunes. Who pays the piper chooses the music. Kwa uharaka wa kamati it is apparent hata hizo hadidu za rejea ni za Voda Fasta. Why are we always in hurry kwanini hatatitaki kushirikisha Ubongo? A very serious matter being done without a clear strategy? Kwani kamati ingeundwa taking on board cross cutting stakeholders kungekuwa na ubaya gani au ni kule kukurupuka which is a default approach by CCM?
 
Duh imenikumbusha porojo zao viongozi waliojiamulia lolote.

Bora tuna Dr. Magufuli awamu hii.
 
Hii sheria ya madini bado night mbaya kwa kuwa ilishindwa kufuata maadhimio mengi ya kamati ya Bomani. Kwa mfano, haiondoi usiri wa mikataba ya maďini pamoja na malipo kwa serikali.
 
Hii sheria ya madini bado night mbaya kwa kuwa ilishindwa kufuata maadhimio mengi ya kamati ya Bomani. Kwa mfano, haiondoi usiri wa mikataba ya maďini pamoja na malipo kwa serikali.

Sheria inasemaje kuhusu uchenjuaji na usafishaji madini nje ya nchi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…