Bodi ya mikopo msitusahau

Bodi ya mikopo msitusahau

Vicin

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2017
Posts
676
Reaction score
295
Habari za muda huu.
Bodi ya mikopo walitoa tamko kwamba hadi tarehe 10/10 watakuwa wamekwishatoa majina ya waliochaguliwa kupata mkopo. Siku chache zilizopita mama ndali alisema kuwa hadi katikati ya mwezi wa kumi watakuwa wamekwishatoa majina.

Ni ombi langu kwamba wangetoa majina mapema tujijue kama tumepata ama laa. Ili kama ni ada na gharama nyingine tuanze kujua tunajichangaje, maana ada na hosteli na chakula si chini ya millioni mbili, kwa usawa huu ni hela nyingi sana kuliko miaka mitatu iliyopita.

Pili, msituache kabisa basi angalau hata hela ya chakula mtusaidie. (0%).

Tatu, tulioomba mkopo tupeane updates, na pia tusisahau kujiombea na kuwaombea ambao bado hawajapata chuo.

Nakaribisha maoni zaidi, mawazo, michango na UPDATES......
================================
>>>>> TCU wametoa tangazo kwamba, hakikisha umethibitisha kuwa unaenda chuo flani kwa ambao walikuwa na multiple admission.
Usipothibitisha kuwa utaenda chuo flani, matokeo yake ni kwamba utakosa mkopo. Kwakuwa bodi ya mikopo itashindwa kujua unaenda chuo gani. Zaidi sana tuwe wavumilivu na wenye subira.



Kwa wale ambao wamepata mkopo, hongereni. Ambao hatujapata bado tusikate tamaa. Mungu yupo.
Tumwamini Yeye aliyetumwa na Yeye.
 
nyie peanen moyo tu siku mkikuta neno

“you are not allocated”

ndo mtajua maana ya Amen. mwaka jana na mm nlikua na sema Amen lkn sikupata hata 0% kitu kilicho nipelekea kuanza biashara huku nasoma nakujikuta niki swagwa Polisi na pingu kwa mara yangu ya kwanza Maishan kwa sanabu ya wema wangu.

pia hawawez kutoa majina yamkopo kabla hawajatoa ya walio kosea taarifa so bado bado ckilizien wazee.
 
nyie peanen moyo tu siku mkikuta neno

“you are not allocated”

ndo mtajua maana ya Amen. mwaka jana na mm nlikua na sema Amen lkn sikupata hata 0% kitu kilicho nipelekea kuanza biashara huku nasoma nakujikuta niki swagwa Polisi na pingu kwa mara yangu ya kwanza Maishan kwa sanabu ya wema wangu.

pia hawawez kutoa majina yamkopo kabla hawajatoa ya walio kosea taarifa so bado bado ckilizien wazee.
Mtu hunena yaujazayo moyo wake. Btw, kama maombi ya mkopo tumeshatuma tunasubiri selection. Anaejua nani atapata na nani atakosa, ni Mungu pekee.
Sisi tunazidi kumuomba Mungu tupate wote wenye vigezo na waliomba. Amen amen amen.
 
Kweli kabisa..vyuo vimemaliza kazi yao sasa tunawasubiri wao..tuombe aliye juu asimamie hili nalo ili tusome bila stress za kiuchumi.
 
Hawawezi toa kabla vyuo havijamaliza uchaguzi
 
Huenda ikawa wanasubiri kesho ipite watu watakaoconfirm vyuo ndio wapewe first selection na ambao watakuwa wameaply second batch watakaopata chuo itatoka second selection.
Ni mawazo yangu lakini.
 
Kuna kelele nyingi mitandaoni kuhusu majina ya waliochaguliwa kupata mkopo. ni uzushi.
 
Stress inahamia heslb! Wawahi isije tokea kama mwaka Jana MTU kasharipoti tayari halafu anakosa mkopo na kulazimika kufungasha mizigo kurudi nyumbani! Watoe mapema ili MTU aamue kusuka au kunyoa! Tatizo LA watanzania ni kuwa MTU akipewa dhamana anajifanya kana kwamba anatoa pesa mfukoni kwake, wakati ni kodi yetu hiyo!
 
hawa HESLB,NACTE,TCU,MOE,TIE hawajawahi toa ahadi ikatekelezeka kwa muda hiyo tarhe 10 itafika 20
 
Back
Top Bottom