Wanafunzi wa elimu ya juu wanaanza masomo jumatatu. Cha kushangaza bodi ya mikopo inaendelea kupitia maombi ya mikopo kwa waombaji wa mwaka wa kwanza wapatao elfu 12. Wengi wao wameshafika vyuoni, hawana ada na pesa za kujikimu na vyuo vinasema mwanafunzi hasajiliwi bila kulipa ada kuanza 60%. Je, ni kwa nini bodi ya mikopo haimalizi kazi yake kabla ya masomo kuanza?