Bodi ya Mikopo (HESLB) wanasemaje kuhusu huu utata?

Bodi ya Mikopo (HESLB) wanasemaje kuhusu huu utata?

PRINCEd

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2015
Posts
862
Reaction score
625
Kuna sintofahamu ( taharuki) kwa wanafunzi wanaondelea (continues) baada ya Bodi ya Mikopo kupunguza kiasi cha malipo au mikopo katika ada na huduma nyinginezo ukiacha ile chakula na malazi.

Mfano mdogo wangu alikuwa analipiwa 530,000 kwa mwaka lakini cha kushangaza amekuta halipiwii kitu chochote mpaka sasa.

Nawaza...

1. Kwanini hakuna tamko rasmi kutoka Bodi ya Mikopo kuhusu utata huu?

2. Hali hii inatoa maoni gani kwa serikali na wanufaika wa Mikopo hii?

3. Je, Serikali imeishiwa pesa kiasi cha kutoweza kuendelea kuwahudumia?

4. Huu si mkataba iweje ukiukwe?

5. Inakuaje jambo nyeti kama hili linakuwa na muonekano wa kufanyika kienyeji?

6. Kuna mahali nimesikia kuwa ni technical issue ila je, iweje ni kwa ada na huduma nyinginezo na chakula na malazi ibaki kama ilivyo?

Karibuni kwa mawazo na mwenye kujua kwa undani jambo hili, tafadhali unakaribishwa.
 
Kila kitu ni uvumilivu,mkuu ni wewe na si mdogo wako..but Mwaka hujaisha kumbuka pia 1st year ndo uwa kipaumbele.but naamini kila kitu kitakua sawa
 
Wanyonge tulieni tumalize kujenga Stiglerz Gorge,SGR tutawaangalia tukimaliza projects hizo.
 
Kila kitu ni uvumilivu,mkuu ni wewe na si mdogo wako..but Mwaka hujaisha kumbuka pia 1st year ndo uwa kipaumbele.but naamini kila kitu kitakua sawa
Muhimu tuambiwe ukweli ili tujipange
 
Harusi mnachangia zaid ya 530,000/= ila kusoma BA Kiswahili au BA Fine & Performing Arts mnataka mlipiwe?
 
Harusi mnachangia zaid ya 530,000/= ila kusoma BA Kiswahili au BA Fine & Performing Arts mnataka mlipiwe?
Kama huna hoja sometimes ni bora kunyamaza kama mimi nilivyonyamaza sio kujitia ujuaji usio na maana...
 
Hivi usipolipa huo mkopo wao wanaweza kukufanya nini?
 
Mkuu wamerudisha hela zilzokatwa,,
Ata mimi nilikuwa kwenye huo mkasa ila leo nimefungua aris yangu mambo yako sawa
 
Back
Top Bottom