Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,789
- 47,984
Niende moja kwa moja kwenye mada yangu. Kuna tabia za hawa jamaa wa bodaboda zinaudhi au kutusumbua, nazifafanua hapa chini.
1. Boda wakikuona tu unakuja wanaanza kupiga honi na wakati mwingine anawasha pikipiki anakufuata, sasa mnadhani sisi ni vipofu? Kama ninahitaji pikipiki nitakuita au kukufuata
2. Unapita zako mjini karibu na kituo chao wanakuita "oi brother twende" wengine wanapiga honi kabisa
3. Mtu upo mjini kwenye mizunguko yako boda anatoka huko speed kali sana alafu wanapiga yowe kabisa "uwiiiii" huku wanafanya pikipiki zinatoa sauti fulani ya kushtua sana kama baruti
4. Boda anakukuta unatembea kwa miguu unafanya mazoezi siku hyo anapunguza speed "brother twende" na anaona kabisa una kitambi na jioni hiyo hakuna jua kali
5. Boda anakuona umebeba ki mzigo chako kidogo tu umeenda mjini ana assume hujaja na usafiri na huwaoni kituo chao mpaka wakuite
Bodaboda, kuna wanasiasa waliwateteeni kwamba mtafutiwe ajira rasmi hiyo haina pesa na ni hatari mlikuja juu kwamba mnapata Tsh 1m+ kwa mwezi, basi acheni kutusumbua
NB: Kwa ambao mtakuja kusema ninunue gari, nawajibu in advance kuna vi-baby walker vya watu huwa ninaazima kufanyia mizunguko hivo sio kwamba natembea kila muda kwa mguu
Na lengo hasa la kuandika hapa, kuna mmoja jioni ya leo nimepita mjini kituoni kwao akaniita nilikuwa namsikiliza mtu kwenye simu sikugeuka nikamsikia anatoa kauli kama vile "anajidai hasikii"
1. Boda wakikuona tu unakuja wanaanza kupiga honi na wakati mwingine anawasha pikipiki anakufuata, sasa mnadhani sisi ni vipofu? Kama ninahitaji pikipiki nitakuita au kukufuata
2. Unapita zako mjini karibu na kituo chao wanakuita "oi brother twende" wengine wanapiga honi kabisa
3. Mtu upo mjini kwenye mizunguko yako boda anatoka huko speed kali sana alafu wanapiga yowe kabisa "uwiiiii" huku wanafanya pikipiki zinatoa sauti fulani ya kushtua sana kama baruti
4. Boda anakukuta unatembea kwa miguu unafanya mazoezi siku hyo anapunguza speed "brother twende" na anaona kabisa una kitambi na jioni hiyo hakuna jua kali
5. Boda anakuona umebeba ki mzigo chako kidogo tu umeenda mjini ana assume hujaja na usafiri na huwaoni kituo chao mpaka wakuite
Bodaboda, kuna wanasiasa waliwateteeni kwamba mtafutiwe ajira rasmi hiyo haina pesa na ni hatari mlikuja juu kwamba mnapata Tsh 1m+ kwa mwezi, basi acheni kutusumbua
NB: Kwa ambao mtakuja kusema ninunue gari, nawajibu in advance kuna vi-baby walker vya watu huwa ninaazima kufanyia mizunguko hivo sio kwamba natembea kila muda kwa mguu
Na lengo hasa la kuandika hapa, kuna mmoja jioni ya leo nimepita mjini kituoni kwao akaniita nilikuwa namsikiliza mtu kwenye simu sikugeuka nikamsikia anatoa kauli kama vile "anajidai hasikii"
itabidi nifanye hivo, ki ukweli ninachukia sana hizo tabia