security guard
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 799
- 603
Vijana waendesha pikipiki za abiria maarufu kama bodaboda mkoani Arusha wafanya maandamano ya Amani kuelekea katika ofisi za jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na kuomba kukutana na kiongozi wake ambapo walimueleza kero zao na changamoto wanazokabiliana nazo katika kazi zao hasa kero ya usumbufu na uonevu kutoka kwa Askari wa barabarani (trafic).
Kiongozi wa UVCCM Mkoa wa Arusha Ndugu Robinson Meitinyiku amepokea maandamano hayo ofisini kwake na kuzungumza na vijana hao waendesha boda boda na kuwahakikishia kuwa suala lao atalitafutia ufumbuzi kwa haraka na wa kudumu.
Suala na bodaboda limeendelea kuwa gumzo nchini hasa katika miji mikubwa kama Dar es salaam, Mwanza, Arusha na Mbeya, ambapo Vyombo vya usalama likiwemo jeshi la polisi mkoani Dar es salaam limepiga marufuku pikipiki kuingia maeneo ya katikati ya jiji kwa kile kilichodaiwa kupunguza matukio ya uharifu hasa wa kutumia bunduki za moto na kusababisha ajali za mara kwa mara baina ya magari na pikipiki hizo.
Chama Cha Mapinduzi kimeendelea kuwa kimbilio la Vijana wa kada mbalimbali hapa nchini, kuanzia wasomi, waajiriwa, na wale waliojiajiri pamoja na wasio na ajira rasmi na wasio na ajira kabisa. Tayari viongozi wa Chama wakiwemo wabunge mkoani Dar es salaam wanafuatilia kwa Umakini hatua za kiutaratibu ambazo zinatumiwa na jeshi la polisi katika kuendeleza operesheni zao bila kuathiri kipato na biashara ya boda boda nchini.
Kiongozi wa UVCCM Mkoa wa Arusha Ndugu Robinson Meitinyiku amepokea maandamano hayo ofisini kwake na kuzungumza na vijana hao waendesha boda boda na kuwahakikishia kuwa suala lao atalitafutia ufumbuzi kwa haraka na wa kudumu.
Suala na bodaboda limeendelea kuwa gumzo nchini hasa katika miji mikubwa kama Dar es salaam, Mwanza, Arusha na Mbeya, ambapo Vyombo vya usalama likiwemo jeshi la polisi mkoani Dar es salaam limepiga marufuku pikipiki kuingia maeneo ya katikati ya jiji kwa kile kilichodaiwa kupunguza matukio ya uharifu hasa wa kutumia bunduki za moto na kusababisha ajali za mara kwa mara baina ya magari na pikipiki hizo.
Chama Cha Mapinduzi kimeendelea kuwa kimbilio la Vijana wa kada mbalimbali hapa nchini, kuanzia wasomi, waajiriwa, na wale waliojiajiri pamoja na wasio na ajira rasmi na wasio na ajira kabisa. Tayari viongozi wa Chama wakiwemo wabunge mkoani Dar es salaam wanafuatilia kwa Umakini hatua za kiutaratibu ambazo zinatumiwa na jeshi la polisi katika kuendeleza operesheni zao bila kuathiri kipato na biashara ya boda boda nchini.