Boda boda : Usalama wa barabarani

shickland

Senior Member
Dec 7, 2015
143
123
Na angalia Chanel 10 hapa naona majadiliano baina ya polisi na boda boda, hoja ni usalama wa barabarani baina ya madereva wa boda boda naabiria wao kuvaa helmet ⛑.

Police wanataka boda boda wasipakie abiria akiwa hana helmet ⛑, madereva wanasema kuwa wao wanavaa abiria hataki sasa, kosa ni la abiria na sio dereva.

Maoni yangu

Nimetembea nchi za Ulaya sana zaidi ya arabuni na Asia, sheria zao Ulaya ikiwa abiria hatafunga mkanda au kuvaa helmet ni kosa la abiria, abiria huyo akiwa na umri wa miaka zaidi ya 18 kama under age 18 ni kosa la driver.

Sasa tukija hapa kwetu nadhani ni wakati wa kuangalia upya hizi sheria, kwa sababu unaweza kukuta driver anafata sheria lakini abiria hataki,je amfanye nini abiria..

Tujadili hili suala
 
Back
Top Bottom