Mbunge wa Karagwe, Mheshimiwa G Blandes, amepata mpinzani katika kugombea kiti cha Karagwe. Mpinzani wake ambaye ni Mweka Hazina wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Karagwe, Karim Amil.
Karim Amil, ni mtoto wa Marehemu Amri Amil, ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mheshimiwa Blandes. Uchaguzi wa 2005, magari ya ya Marehemu Amri, yalitumika kumfanyia kampini Mheshimiwa Blandes. Kijana Karim, ndiye alikuwa kiongozi wa msafara katika kampeni za Mheshimiwa Blandes.
Swali la kujiuliza ni kwanini Karim, ameamua kumgeuka Blandes? Majibu ni mengi! Je Karim, anaweza? Kisomo chake ni mashaka! Lakini pia ile ali yake ya kuwa na asili ya Uarabuni, inaweza kumletea shida.
Hata hivyo kuna watu wengine, kupitia chama Cha Mapinduzi, wanaojiandaa kupambana na Blandes. Bwana Karugaba, mstaafu wa shirika la reli naye ana mpango wa kugombea. Amejaribu mara nyingi bila ya mafanikio. Profesa Innocent Ngalinda, naye ameonyesha nia ya kugombea.
Chadema, inajipanga pia kuweka mgombea. Kwa ufupi ni kwamba Mheshimiwa Blandes, ana wakati mgumu sana katika jimbo la Karagwe. Inasemekana 2005, alisaidiwa na Sir G Kahama. Je atamsaidia na mwaka huu? Kuna habari kwamba Sir G Kahama, bado anataka kiti hicho kiwe cha familia. Eti, anamshawishi mke wake agombee, akikataa basi mtoto wake anayeifahmu Karagwe, kwenye ramani, atagombea. Jeuri yafedha itafanya kazi hata kama Mtoto wake hafahamiki vizuri kule Karagwe, kutokana na tabia ya Sir G Kahama, kutopenda kuileta familia yake Karagwe.
Karim Amil, ni mtoto wa Marehemu Amri Amil, ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mheshimiwa Blandes. Uchaguzi wa 2005, magari ya ya Marehemu Amri, yalitumika kumfanyia kampini Mheshimiwa Blandes. Kijana Karim, ndiye alikuwa kiongozi wa msafara katika kampeni za Mheshimiwa Blandes.
Swali la kujiuliza ni kwanini Karim, ameamua kumgeuka Blandes? Majibu ni mengi! Je Karim, anaweza? Kisomo chake ni mashaka! Lakini pia ile ali yake ya kuwa na asili ya Uarabuni, inaweza kumletea shida.
Hata hivyo kuna watu wengine, kupitia chama Cha Mapinduzi, wanaojiandaa kupambana na Blandes. Bwana Karugaba, mstaafu wa shirika la reli naye ana mpango wa kugombea. Amejaribu mara nyingi bila ya mafanikio. Profesa Innocent Ngalinda, naye ameonyesha nia ya kugombea.
Chadema, inajipanga pia kuweka mgombea. Kwa ufupi ni kwamba Mheshimiwa Blandes, ana wakati mgumu sana katika jimbo la Karagwe. Inasemekana 2005, alisaidiwa na Sir G Kahama. Je atamsaidia na mwaka huu? Kuna habari kwamba Sir G Kahama, bado anataka kiti hicho kiwe cha familia. Eti, anamshawishi mke wake agombee, akikataa basi mtoto wake anayeifahmu Karagwe, kwenye ramani, atagombea. Jeuri yafedha itafanya kazi hata kama Mtoto wake hafahamiki vizuri kule Karagwe, kutokana na tabia ya Sir G Kahama, kutopenda kuileta familia yake Karagwe.