malimi katoro
JF-Expert Member
- Mar 31, 2015
- 358
- 154
Habari zenu wanaJF,
Mwaka jana nilipokuwa JKT kwa mujibu wa sheria nilikutana na binti toka Iringa ambaye ni mhehe,kiufupi binti si mrembo kivile ila kilichonivutia kwake ni ule ukaribu alionesha kwangu kipindi chote cha mafunzo.Pia ni mcha mungu a.k.a mlokole kitu ambacho mi napenda sana.
Sikusita kumtamkia kuwa nampenda sana na hata kumuoa nilikuwa tayari,tofauti na matarajio yangu alinijbu kuwa ana mpenzi wake,kwa vile mi king'anganizi nilizidi kuchokoza fikra zake lakini alizidi kunibania eti ana jamaa mwingne na hawezi kuvua chupi yake kwa mtu mwingine.
Baada ya muda wa mafunzo ya JKT kuisha kila mtu alienda kwao ila niliendelea kumkumbusha ombi langu.
Siku moja ambayo sikutegemea kabisa nilipokea namba ya simu kwa namba mpya na jamaa kujitambulisha kuwa ni boyfriend wa binti ambaye mimi nilikuwa namtongoza,jamaa alikuwa msatarabu tu alinisihi nisimfuatilie yule binti,ok sikuwa na hiana nikaamua kumuacha na sikuwasiliana tena na yule binti.
Bada ya kutoka ajira binti yule alinipigia simu na kunijulisha kuwa kapangiwa mkoa fulani na hapo ilikuwa ni baada ya kutowasiliana naye kwa muda wa miezi mitatu,na tangu hapo alianza kunipigia simu na kuchati kwa kila namna,wakati mwingine ananipigia simu lakini anakuwa hana hata cha maana cha kunieleza.
Muda umeenda uvumilivu umemshinda imebidi aniambie kuwa eti ombi langu amelikubali na alikuwa akinipima uvumilivu na imani yangu sasa ameridhia kuolewa na mimi na anadai ananipenda sana.
Juzi kanitumia elfu 50,000/= eti ya vocha,sasa niko njia panda. Je, nifanye nini wadau?
Je, huyu mdada ananipenda kweli au ni maigizo tu?
Vipi kuhusu jamaa yake aliyenipigia simu na kunisihi nimwache na yeye(binti) ndio alimpa namba zangu anipigie?
Karibuni kwa ushauri!
Mwaka jana nilipokuwa JKT kwa mujibu wa sheria nilikutana na binti toka Iringa ambaye ni mhehe,kiufupi binti si mrembo kivile ila kilichonivutia kwake ni ule ukaribu alionesha kwangu kipindi chote cha mafunzo.Pia ni mcha mungu a.k.a mlokole kitu ambacho mi napenda sana.
Sikusita kumtamkia kuwa nampenda sana na hata kumuoa nilikuwa tayari,tofauti na matarajio yangu alinijbu kuwa ana mpenzi wake,kwa vile mi king'anganizi nilizidi kuchokoza fikra zake lakini alizidi kunibania eti ana jamaa mwingne na hawezi kuvua chupi yake kwa mtu mwingine.
Baada ya muda wa mafunzo ya JKT kuisha kila mtu alienda kwao ila niliendelea kumkumbusha ombi langu.
Siku moja ambayo sikutegemea kabisa nilipokea namba ya simu kwa namba mpya na jamaa kujitambulisha kuwa ni boyfriend wa binti ambaye mimi nilikuwa namtongoza,jamaa alikuwa msatarabu tu alinisihi nisimfuatilie yule binti,ok sikuwa na hiana nikaamua kumuacha na sikuwasiliana tena na yule binti.
Bada ya kutoka ajira binti yule alinipigia simu na kunijulisha kuwa kapangiwa mkoa fulani na hapo ilikuwa ni baada ya kutowasiliana naye kwa muda wa miezi mitatu,na tangu hapo alianza kunipigia simu na kuchati kwa kila namna,wakati mwingine ananipigia simu lakini anakuwa hana hata cha maana cha kunieleza.
Muda umeenda uvumilivu umemshinda imebidi aniambie kuwa eti ombi langu amelikubali na alikuwa akinipima uvumilivu na imani yangu sasa ameridhia kuolewa na mimi na anadai ananipenda sana.
Juzi kanitumia elfu 50,000/= eti ya vocha,sasa niko njia panda. Je, nifanye nini wadau?
Je, huyu mdada ananipenda kweli au ni maigizo tu?
Vipi kuhusu jamaa yake aliyenipigia simu na kunisihi nimwache na yeye(binti) ndio alimpa namba zangu anipigie?
Karibuni kwa ushauri!